Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Tuesday, February 14, 2012

Zambia wapokelewa kwa shangwe Lusaka






 Mabingwa wapya wa soka wa Afrika, Chipolopolo wa Zambia wamepokelewa kwa shangwe katika mji mkuu Lusaka.
Mwandishi wa BBC anasema mashabiki waliokuwa wakisubiri, walilipuka kwa kelele za shangwe, wakati nahodha Christopher Katongo alipotoka kwenye ndege akiwa amelibeba Kombe la dhahabu la Mataifa ya Afrika.
Zambia waliwashinda Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 8-7, katika mchezo wenye msisimko hasa baada ya dakika za kawaida na za nyongeza kumalizika.
"Hakutukata kuondoka mikono mitupu "Kennedy Mweene
Ushindi huu una umuhimu wa kipekee hasa kwa sababu miaka 19 iliyopita karibu kikosi kizima cha Zambia kiliteketea katika ajali ya ndege nchini Gabon.
Mwandishi wa BBC Mutuna Chanda anasema barabara ya kwenda uwanja wa ndege wa Lusaka imetapakaa rangi ya ijani, nyekundu, machungwa na nyeusi, huku maelfu ya mashabiki wakijipanga kutaka kuwaona wachezaji wakirejea rasmi.
Kutakuwa na sherehe katika viwanja vya wazi mjini Lusaka.

Kutuza

Takriban watu 1,000, wengi wao wakiwa wametembea kilomita 25, walikuwepo uwanjani kuwalaki wachezaji wa timu ya taifa.
Shughuli hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na rais wa zamani Rupiah Banda na Kenneth Kaunda, ambao wote ni mashabiki wakubwa wa kandanda.
Wananchi wengi wa Zambia wamejipa likizo hii leo ili kusherekea ushindi wa kwanza kabisa wa Zambia wa Kombe la Mataifa ya Afrika.
Kikosi hiki kilichoibuka na ushindi, kiliondoka katika uwanja ule ule wa ndege wa Libreville, ambao ndege ya kijeshi iliongeza mafuta ikielekea Senegal kwa ajili ya mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia mwezi Machi 1993 - na ndege hiyo kuanguka muda mfupi baada ya kupaa.
Wachezaji wa Zambia, maarufu kama Chipolopolo Boys (yaani risasi za shaba), walitoa heshima zao kwa wachezaji 18 waliokufa katika ajali hiyo ya ndege - na kutuza ushindi huu kwa kikosi hicho kilichopotea.

Amani

"Wachezaji waliokufa katika ajali ya ndege nchini Gabon ndio walitupa hamasa, na nguvu katika michuano hiyo," amesema golikipa Kennedy Mweene akiwaambia waandishi wa habari kabla ya kuondoka Libreville.
"Hatukutaka kuondoka mikono mitupu," alisema.
Winga Felix Katongo aliwaambia waandishi wa habari: "Tulitaka kushinda kombe hili ili wananchi wa Zambia wajivunie na kwa wale waliokufa, kupumzika kwa amani. Sasa roho zao zitakuwa na amani."
Source:BBC

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.