Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Tuesday, February 14, 2012

Kimbunga chaathiri Madagascar

Kimbunga Giovanna
Kimbunga Giovanna
Kimbunga chenye upepo mkali wa mwendo wa kilomita 194 kwa saa kimeathiri kisiwa cha Madagascar kwa kung'oa miti na vifaa vya kusafirisha umeme.
Kimbunga hicho, ambacho kimepewa jina Giovanna kilianza kwa kuathiri mji wa Toamasina, mashariki mwa kisiwa hicho.
Magari ya huduma za dharura yameonekana jijini Antananarivo yakiondoa vifusi.
Wataalam wa masuala ya hali ya hewa wanaonya kwamba uharibifu katika kisiwa hicho huenda ukawa mbaya kama ule wa 1994 , wakati kimbunga kilipowaua watu 200 na kuwaacha wengine 40,000 bila makaazi.
Afisa mmoja wa serikali ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba Takriban mtu mmoja amefariki dunia katika mji wa Brickaville baada ya kuangukiwa na nguzo ya umeme.
Watu wamebakia majumbani mwao kwa sababu ofisi, shule na biashara zimefungwa na umeme umekatika.

BBC

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.