Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Sunday, February 26, 2012

Talaka ikitolewa huathiri wote hata wale tusiowaona!

Mahusiano ni kazi (hardwork), migogoro hujitokeza, msongo wa mawazo haukosekani, matarajio huyeyuka hata hivyo kila mmoja ana ufahamu na uwezo tofauti wa kukabiliana na hizi challenges.
Jambo moja la msingi ni kwamba matatizo yote ya ndoa huweza kuwa fixed na talaka huweza kuzuilika kama wawili wakiamua.
Hata hivyo ni muhimu kujua maafa ya uamuzi wa kupeana talaka ili kama unawaza talaka ni muhimu kufahamu ili uweze kubadilisha mtazamo wako ambao unaudanganyifu uliokithiri.
Moja:
TALAKA HUVUNJA NYUMBA
Familia iliyoanzishwa na wawili walioana huharibiwa muda wote ambao wahusika wataishi chini ya jua.
Kunakuwa na kovu (scar) ambalo huambatana na wahusika na kamwe haliwezi kufutika.
Talaka huvunja nyumba familia ambayo ingekuwa Baraka kwa mama, baba na watoto/mtoto.
Mbili:
TALAKA HUSABABISHA MIOYO KUTOA DAMU (ngeu)
Talaka haiathiri wahusika tu (yaani mke na mume) bali huathiri familia, ndugu, jamii na taifa kwa ujumla.
Talaka husababisha marafiki na ndugu kuomboleza kwa machozi ya damu bila kusema lolote.
Tatu:
TALAKA HUATHIRI WATOTO
Watoto huchanganyikiwa na kitendo cha wazazi kuachana na hakuna mtu duniani anayeweza kufahamu ugumu na uchungu ambao huwakuta watoto katika mioyo na akili zao.
Kila mtoto anaufahamu wa kwamba anahitaji kupata upendo wa baba na mama pamoja na anaona hata kwa watoto wenzake.
Mtoto huchanganyikiwa mno pale wazazi wakitalikiana.
Nne:
TALAKA HUHARIBU USHUHUDA

Kila anayepewa talaka au kutoa talaka hujiwekea alama (mark/label) katika maisha yake na watu huisoma hiyo alama kwamba “Huyu ni failure” na huweza kusababisha kukosa acceptance kwa watu wengine bila sababu ya msingi, kisa talaka!
Tano:
TALAKA NI KUKANA KIAPO
Wakati wa kufunga ndoa wahusika walitoa ahadi zao (vows) kukubali na kuahidi kwamba wataishi pamoja katika afya na uzima, raha na shida hadi kifo kitakapowatenganisha.
Walitoa ahadi mbele za Mungu na mashahidi.
Je, walikuwa hawamaanishi?
Je, kichwani akili zilihama?
Je, walikuwa wanatania?
Je, ilikuwa kweli au uwongo?
Talaka ni kukana kiapo na pia kuikana Biblia.


Chanzo: mbilinyi blo

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.