Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Saturday, October 27, 2012

Mbunge ala mamiloni! Awauzia TANESCO matairi 300 alipwa fedha ya matairi 600

 


SIKU chache kabla ya kikao cha Bunge kuanza mjini Dodoma, zimeibuka taarifa kwamba mmoja wa wabunge aliyekuwa mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa alishiriki kikamilifu kuendesha biashara na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ambalo kimsingi anapaswa kulisimamia.

Taarifa hizo zimekuja huku tayari habari zilizovuja na kuandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari kudai kwamba uchunguzi wa kamati ya ndogo chini ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Maadili iliyokuwa chini ya Mbunge wa Mlalo, Brigedia Jenerali (mstaafu), Hassan Ngwilizi haikuwatia hatiani wabunge waliokuwa wakituhumiwa.


Hao walikuwa ni wabunge wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa na Spika Anne Makinda, waliokuwa wakituhumiwa kushiriki vitendo vinavyoashiria rushwa ndani ya TANESCO, kampuni ambayo aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wake, William Mhando amesimamishwa kwa tuhuma mbalimbali.


Taarifa za karibuni zaidi zinaonyesha kwamba mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo, Sarah Msafiri, alikuwa na uhusiano na Kampuni ya M/S Sharrif’s Services & General Supply iliyokuwa ikifanya biashara na TANESCO na yeye kusimamia malipo yenye utata kutoka shirika hilo ambalo mbunge huyo analisimamia.


Kampuni hiyo ilikuwa inasambaza matairi ya magari kwa TANESCO ikiwa na mkataba wa matairi yenye thamani ya shilingi milioni 387.


Anasema mtoa taarifa wetu kuhusu biashara hiyo ya matairi: “Yule mbunge ndiye aliyekuwa akija TANESCO wakati wa kufunga mkataba. Mkataba ulikuwa awali wa matairi 652. Baadaye idadi hiyo ilipungua yakaletwa matairi 356, lakini pamoja na matairi kupungua, kiasi cha pesa zilizolipwa kilibaki kilekile”.


Lakini wakati hayo yakiendelea, zipo pia taarifa kwamba uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini na hasa Waziri, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu Eliakim Maswi, umekuwa ukifuatilia kwa karibu taarifa zilizovuja za Kamati ya Ngwilizi zinazoonyesha kwamba ripoti ya Kamati hiyo imeukandamiza uongozi huo kwenye sakata linalouhusisha na tuhuma za rushwa za wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini.


Anasema mtoa habari wetu: “Baada ya kuanza kuvuja kwa ripoti hiyo walikutana kwa nia ya kutaka kujua kwanza kwamba kweli ripoti ya kamati ile imewatuhumu na hali ikiwa ni hiyo wafanye nini, maana wao si wanasiasa, achilia mbali kwamba Profesa Muhongo ni Mbunge wa Kuteuliwa.


“Hilo la kwamba wamekwenda kumwona Rais kumwambia kwamba wanataka kuondoka sijalisikia. Ninachojua ni kwamba walikutana. Na hiyo inatokana na ukweli kwamba hawa ni watu wawili wanaoshirikiana kwa karibu katika kuendesha wizara, hivyo mmoja akiondoka sioni uwezekano wa mwingine kubaki.


“Wizara hii pamoja na taasisi zake inahitaji watu waliojitoa kusaidia nchi. Na hawa huwezi kuwalinganisha na ile timu iliyoondoka. Wanapishana sana kwa malengo na maono. Sijui maisha yao yalivyo, lakini nawaona kama watu wasio na makubwa na wasiokuwa na tamaa ya mali.


“Kwa hali ya kiwango cha ufisadi tulichofikia kama nchi unahitaji ujasiri mkubwa, kwa mfano, kusema waziwazi kwamba sasa hapatakuwa na mgawo wa umeme tena.


“Kusema hivyo maana yake unajitangazia vita na matajiri na wanasiasa wapenda mali. Lakini hawa wamesema, na wamerudia mara kadhaa, kwamba mgawo uliokuwapo ulikuwa wa kutungwa, hata hotuba ya Waziri wakati wa Bunge la bajeti ilieleza hivyo. Hiyo si kazi rahisi. Lazima watapigwa vita.


“Hivi unafikiri Kamati ya Bunge ni ya malaika? Ile ilikuwa sawa na kesi ya nyani unampelekea ngedere”.


Katika mkutano ujao wa Bunge matokeo ya uchunguzi wa kamati iliyoundwa kuchunguza sakata zima la wabunge kuhongwa na wengine kuwa na maslahi katika TANESCO licha ya kuwa wao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, yatawasilishwa kwa Spika na baadaye kuwekwa wazi kwa wabunge.


Wabunge walijikuta katika mpasuko miongoni mwao hasa baada ya kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TANESCO, William Mhando na wenzake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu zilizokuwa zikiwakabili.


Tayari katika uchunguzi wa Mhando na wenzake zimebainika kasoro lukuki kuhusu mwenendo wao kama viongozi wa TANESCO. Hali pia si swari kwa upande wa Bodi ya TANESCO inayoongozwa na Jenerali (mstaafu) Robert Mboma, ikielezwa kuwa bodi hiyo kwa namna fulani ni sehemu ya uozo uliokuwa ukiendelea TANESCO ikiwa ni pamoja na kulea kile kinachoelezwa kuwa mgawo wa umeme wa kutengeneza ‘mezani.’


Na bado kachaguliwa CCM-NEC ?


CHANZO: Raia Mwema | 24 Oct 2012
        

WANAWAKE WANAVYOIVAA MIKENGE KWENYE NDOA..............!

 



Ngoja leo niyadadavue makosa yanayofanywa na wanawake wengi pale wanapoamua ni nani wa kuoana naye:

1. Kosa la kwanza, unaolewa na mtu ambaye unajua kabisa ni dhaifu na mkorofi, ukitarajia kwamba ataondoa kasoro zake akiwa ndani ya ndoa. Hili ni kosa kubwa. Kama huna furaha sasa na mtu kabla hujaoana naye, usikubali kuingia huo mkenge. Huwezi kutegemea mtu kuadilika aiwa ndani ya ndoa.

2. Kosa la pili, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu ya msisimko wa mwili kimapenzi lakini si kwa sababu ya tabia zake. Kuwa mwangalifu na neno “Nakupenda” neno hili mara nyingi maana yake ni “Nina uchu nawe.” Ndiyo amevutiwa nawekimaumbile, lakini undani wa tabia yake unaujua? Hapa kuna mambo manne… Kwanza, Je anapenda kutomfanyia binadamu mwenzie mabaya kama mabavyo yeye hataki kufanyiwa? Pili, anaishi vipi na watu wengine? Anaishi vipi na watu ambao ana uadui nao, Anawasamehe au analipiza visasi? Je anatoa misaada kwa masikini? Tatu, je ni mkweli, anachokisema ndicho anachokifanya? Je anaaminika? Majukumu anayoahidi kuyafanya anayatimiza? Nne, je anajipenda? Je ni mtu ambaye yuko imara kimapenzi au ni mtu wa kuyumbayumba na asiye na msimamo? Sio mtu akishauriwa na marafiki zake au ndugu zake huko, anakuja na maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu

3. Kosa la tatu, unaolewa na mtu ambaye hamna malengo na vipaumbele vya aina moja vya maisha. Je mna utashi wa aina moja? Kwa mfano ni vyema mwanamuziki akaolewa na mwanamuziki mwenzie kwa kuwa anajua mzingira ya kazi ya mwenzie ili kupunguza wivu wa kupindukia usio wa lazima

4. Kosa la nne, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu mnakutana kimwili mapema mno. Kukutana kimwili kabla ya ndoa kunaweza kuleta matatizo makubwa mno. Tendo la ndoa kabla ya ndoa hufunika uwezo wa mtu kufikiri. Mtu anabaki kufaidi na kubaki kujali mapenzi ya kimwili na kusahau kukuna ubongo juu ya mambo mengine. Ni lazima mwanamke akune ubongo ili kujua kama huyo mpenzi anakidhi vigezo vyote vya mume mtarajiwa.

5. Kosa la tano, unaolewa na mtu ambaye huna msisimko wa kimwili umwonapo. Kuna uwezekano mkubwa mwanamke akavutiwa na mwanaume kwa sababu ya aina ya gari analomiliki. Hapa hakuna msisimko wa kimwili bali mwanamke kavutwa na gari au rasilimali alizo nazo mwanaume huyo.

6. Kosa la sita, unaolewa na mwanaume anayependa kudhibiti. kuwa na tabia ya kudhibiti wenzako ni ya dalili za mtu jeuri na mwenye kujisikia na mfujaji. Naomba kutofautisha kati ya “kudhibiti” na “kutoa mawazo.” Mtu anayekupa mawazo ni kwa faida yako, lakini anayekudhibiti ni kwa faida yake.

7. Kosa la saba, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu unakimbia matatizo uliyo nayo. Unaweza kuwa hujaolewa na huna raha wala amani na ukataka kuolewa. Ndo haiwezi kukutatulia matatizo yako binafsi ya kisaikolojia nay a kimapenzi. Badala a kuyapunguza matatizo hayo, ndoa itayaoneza. Kama huna amani na huyafuahii maisha, chukua jukumu la kurekebisha matatizo hayo sasa kabla hujaolewa. Itakuwa ni faida kwako na kwa mmeo mtarajiwa.

8. Kosa la nane, unaolewa na mtu asiya sahihi kwa kuwa yuko ndani ya pembe tatu. Mtu ambaye anaishi na wazazi wake ni moja ya mfano wa mtu anayeishi katika pembe tatu. Watu wengine wanaoweza wakawa wanaishi ndani ya pembe tatu ni kama wanaofanya kazi saa 24! Huyu mtu halali? Watu wengine walio katika pembe tatu ni watu wanaotumia madawa ya kulevya, mtu anayetawaliwa na “hobbie” zake, anapenda sana michezo (Mpira), kuperuzi mitandao ya kijamii na anapenda sana fedha. Hakikisha kwamba wewe na mpenzi wako , nyote hamtawaliwi na pembe tatu. Mtu ambaye anatawaliwa na pembe tatu hawezi kumtimizia mpenzi wake haja ya upendo atakapokuwa anahitaji. Kama mpenzi wako anatawaliwa na pembe tatu kwa kiasi kikubwa, wewe huwezi kuwa kipaumbele chake.
 

WANAUME NA WANAWAKE WANAPOLALAMIKA ...........!


 



Ngoja niyadadavue malalamiko ya wanawake kwanza hapa chini:

1. Wanawake wanalalamika kwamba wanaume sio waelewa wazuri, yaani huwa wanatafsiri mambo tofauti na isivyo.

2. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawajali hisia za wapenzi wao wala hawajali pia kuhusu mahitaji yao.

3. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawajui kuonesha upendo , yaani hata wanapopenda inakuwa kama vile wanajisumbua tu, kiasi kwamba mwanamke anaweza kuhisi kwamba hapendwi.

4. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawana muda wa kucheza na wapenzi wao kabla hawajafanya nao mapenzi yaani hawawaandai kabla ya tendo, wao huwarukia tu na kumaliza haja zao haraka na kugeuka ukutani kabla ya wao (wanawake) hawajaridhika.

5. Wanalalamika kwamba wanaume hawana mawasiliano, huwa hawajui kueleza hisia zao na mawazo yao, bali ni watu wa kunyamaza na kujifungia kwenye dunia yao wenyewe. Wanahisi kama kuelezea hisia zao na mawazo yao ni kuwa dhaifu.

6. Wanawake hulalamika kwamba, wanaume hawana muda wa kukaa nyumbani na familia zao, kwa sehemu kubwa ni watu wa nje tu.

7. Wanawake pia wanawalaumu wanaume kwamba, hawajali mustakabali wa usafi au kupendeza kwa nyumba.

8. Wanawake wanawalalamika kwamba, wanaume huwa wanafanya maamuzi yao bila kujali kuwa wanawake wapo na wanaweza kuwa na michango mizuri sana kwa hicho wanachotaka kukifanya. Huamua kama kwamba wanawake siyo sehemu ya familia.

9. Wanalaumu kwamba, wanaume ndiyo wanaoanzisha au kuendekeza kutoka nje ya ndoa ukilinganisha na wao wanawake.



Malalamiko ya wanaume nayo nayadadavua kama ifuatavyo…..

1. Wanaume wanalalamika kwamba wanawake ni watu wa kulalamika, kukosoa na wenye vijineno vya hapa na pale visivyo na maana na vyenye kukera.

2. Wanaume wanalalamika kwamba wanawake wanajaribu sana kuwadhibiti na kuwakandamiza pale wanapoachiwa nafasi kidogo.

3. Wanaume wanadai kwamba wanawake huwa hawana furaha, mara nyingi wanaonekana kama vile wako kwenye simanzi fulani na wanapenda sana kununanuna hasa pale wanaume wanaposhindwa kuwatekelezea kile walichotaka hata kama hakina umuhimu kwa wakati ule.

4. Wanaume wanalalamika sana kwamba wanawake wanawanyima unyumba kama adhabu ya kuwakomoa. Siyo kuwakomoa tu, bali huwa wanafanya hivyo kwa lengo la kuwashurutisha wakubaliane na utashi wao fulani.

5. Lalamiko lingine la wanaume kuhusu wanawake ni lile la kwamba, huwa hawafikirii kwa mantiki, bali mara nyingi kufikiri kwao huwa kunakumbwa na mhemko. Kwa hiyo, uamuzi wao mwingi hauangalii mantiki bali hujali zaidi hisia zao.

6. Wanawake wanalalamikiwa na wanaume kwamba, hali zao za kihisia huwa hazitabiriki. Yaani huwa zinabadilika kufuatana na mabadiliko ya miili yao ya kihomoni miilini mwao nyakati kama zile za siku zao(hedhi), nyakati za ujauzito na hata wanapokoma kuziona siku zao(menopause) .

7. Wanaume wanawalalamikia wanawake kwa tabia yao ya umbea, kwamba midomo yao huwasha sana hadi waseme kile walichokiona au kukisikia hata kama si lazima na pengine ni hatari.

8. Wanawake wanalalamikiwa pia na wanaume kwamba, huwa wanatoka nje ya ndoa, hasa wanapohisi kukosewa upendo ndani, jambo ambalo haliwezi kuleta suluhu kwa tatizo hilo.

Kama wewe ni mwanaume na umegundua kwamba moja au baadhi ya malalamiko ya wanawake yanakugusa inabidi ubadilike na kufanya kinyume chake. Kama wewe ni mwanamke pia hali ni kama hiyo. Kama kweli una mdomo mwingi kwa mfano, ujue wanaume hawapendi tabia hiyo, hivyo huna budi kubadilika.
 

Chanzo cha kuchokana katika mahusiano/ndoa na ushauri wa kukabiliana na tatizo hili

Je unahisi umeshaanza kumchoka mmeo ama mkeo????!!!!


Imeandikwa na Shams Elmi (Abu 'Ilmi)

Takriban katika maisha ya wanandoa walio wengi kama sio wote, ndoa zao hupitia katika vipindi tofauti. Kama ulivyo umri wa Binadamu, ndoa hupitia katika kipindi cha utoto, ujana na uzee, na kila kipindi kina mambo yake na taratibu zake ambazo kama wanandoa watashindwa kuzifuata basi huenda ndoa hiyo ikakumbwa na mtihani mkubwa, nao ni mtihani wa kuchokana.

Utoto wa Ndoa:

Wengine hukiita kipindi hiki (Honey Moon) mwezi wa asali, kipindi cha raha, utulivu, mapenzi, maelewano baina ya wanandoa. Si lazima kiwe mwezi mmoja kama watu wengi wanavyoamini, bali kinaweza kikawa chini ya mwezi mmoja au zaidi ya mwezi mmoja.


Ujana wa Ndoa:

Hiki ni kipindi kinachofuatia baada tu ya utoto wa ndoa, ni kipindi ambacho kila mmoja miongoni mwa wanandoa anakuwa tayari ameshamtambua mwenzake katika shaksia yake (personality) kwa maana ya jinsi anavyoangalia mambo, jinsi anavyofikiri, mitazamo yake, mielekeo yake na matarajio yake.

Uzee wa Ndoa:

Kipindi hiki ni kipindi ambacho wanandoa wanakuwa tayari wameishaingia katika majukumu ya kulea kwa kupata matunda ya ndoa yao ambayo ni mtoto au watoto.

Kuchokana kwa wanandoa ni tatizo ambalo linatokea kwa familia nyingi, na kusababisha migogoro mingi na hata kufikia familia kuvunjika au kuishi kwa ajili tu ya kulea watoto na si vinginevyo.

Utakuta katika baadhi ya familia, Baba na Mama wanaishi katika nyumba moja, ukiwaona utadhani ni mume na mke wanaopendana, kumbe wanaishi kwa ajili tu ya kuwalea watoto wao na kuogopea maneno ya watu, hali hii ni hali ya talaka ya kimapenzi (emotional Divorce) na ni hali mbaya ambayo mara nyingi humpa msukumo mwanamume wa kuoa mke wa pili katika harakati za kutafuta utulivu na sehemu ya kukimbilia

Tatizo hili la kuchokana kwa wanandoa linasababishwa na wanandoa wote wawili kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya haki za mume na mke.
Hivyo basi, sababu kubwa ya wanandoa kuchokana, au kuzeeka kwa ndoa kunasababishwa na mwanamke, pale ambapo atashindwa kutumia nafasi yake na vipawa alivyopewa kuleta utulivu katika ndoa yao, na hapa nitajaribu kujadili baadhi ya visababishi vinavyopelekea kuzeeka kwa ndoa au kuchokana visababishi ambavyo huwa vinadharaulika na kuonekana vitu vidogo vidogo hususan kwa wanawake wengi.

a) Kuzoeana: kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususan kwa upande wa mwanamke kwa kutojali usafi wake, mavazi anayovaa, chakula anchopika, nidhamu ya nyumba na mpangilio kwa ujumla. Matatizo mengi ndani ya nyumba yanaweza kusababishwa na moja au baadhi ya tabia hizo, ambazo huenda ikawa hazitokani na dharau, bali kuzoeana, kwa mfano: siku za utoto wa ndoa mwanamke huwa anajali sana usafi wa mwili wake, umaridadi wa nguo anazovaa, usafi wa nyumba na nidhamu ya hali ya juu, upishi wa chakula unaozingatia vionjo na ubunifu, mapokezi yenye bashasha na wakati mwingine hata kumkumbatia mumewe arudipo kutoka kazini. Lakini baada ya kuzoeana yote hayo hubadilika, mwanamke huhisi kuwa hana jipya la kumuonyesha mumewe, hujiona wameishakuwa watu wazima sasa, na mara nyingi utakuta mwanamke huyu anashinda na sare (uniform) moja kuanzia asubuhi hadi anapopanda kitandani usiku, mambo ya Hinna, nguo za fashion, salon, manukato, kujipamba na dhahabu huyafanya pale anapotoka kwenda harusini na sio nyumbani. Huku ndio kuzoena, na tafsiri sahihi ni kudharau.

b) Mazungumzo: Mazungumzo ni njia muhimu ya kujenga ndoa na kuiimarisha , aidha ni njia ya mkato ya kuchokana na kuchukiana. Mwanamke ambaye hajui wakati gani aseme nini na wakati gani asiseme, hujikuta katika wakati mgumu ndani ya ndoa yake. Kwa mfano: Mwanamke ambaye kila anapoongea na mume wake huanza mazungumzo yake na matatizo na lawama humfanya mumewe awe na woga kila anaposikia sauti yake, na kuiona nyumba chungu, kwa sababu hakuna binadamu anayependa kusikia matatizo tu wakati wote. Mwanamke wa aina hii huwa anamsubiri mumewe kwa hamu kubwa, na anapofika tu na kabla hata ya kupata rizki, anaanza kumsomea orodha ya matatizo; watoto wamerudishwa shule, karo haijalipwa, shangazi yako amepiga simu mjomba kalazwa Hospitali na kadhalika na kadhalika. Nyumba ya aina hii huzeeka haraka na wanandoa kuchokana.

c) Kusomana Tabia: ni udhaifu mkubwa kwa wanandoa ambao wana mwaka mmoja katika ndoa yao wakawa bado hawajasomana tabia, au wakawa wameishasomana tabia, lakini kila mmoja akawa anataka tabia zake ndio ziwe dira. Kwa mwanamke mwenye busara na mwenye kuithamini ndoa yake, husoma tabia za mumewe na kuangalia jinsi gani anavyoweza kuzioanisha na zile zake ili kuepusha migongano, aidha hutafuta fursa muafaka ya kumkinaisha mumewe juu ya fikra fulani au tabia fulani ambayo yeye haridhiki nayo. Ni muhimu kwa mwanaume vilevile kuzisoma tabia za mke wake, vitu gani vinamuudhi, na vitu gani vinamfurahisha.

d) Kutamka na kudhihirisha mapenzi: Ni muhimu sana kwa wanandoa ili kuyaimarisha mapenzi yao yasiote mvi, kutamkiana hisia zao za kupendana bila utangulizi wowote, kwa mume au mke kumwambia mwenzake NAKUPENDA kuna athari nzuri katika nafsi kuliko hata ungemletea zawadi ya kitu cha gharama.

e) Kupeana zawadi: Zawadi ni njia nzuri ya kudhihirisha mapenzi yako na nafasi ya mwenzako katika maisha yako, na zawadi ambayo mtu huitoa kwa mwenzake bila ya utangulizi au mnasaba maalum huleta athari njema na huimarisha mapenzi. Na katika zoezi hili la kupeana zawadi, ni vema kila mmoja akaelewa anachokipenda mwengine ili zawadi iwe na athari inayotarajiwa, na iwe ni zawadi maalum kwa mlengwa, isiwe zawadi ambayo mtoaji naye atafaidika na zawadi hiyo, kwa mfano, si vema kwa mwanamme kumletea mkewe zawadi ya sufuria, microwave, pazia, Dinner set, hiyo haitaitwa zawadi, lakini ni juu yake kumletea manukato ayapandayo, hereni, bangili, mkufu au pete ya dhahabu, na vitu ambavyo ni maalumu kwa matumizi yake binafsi. Hali kadhalika kwa mwanamke kumzawadia mumewe achunge vigezo hivyo.

f) Kualikana vyakula: Inaweza kushangaza kuwa vipi wanandoa wataalikana chakula wakati wenyewe ni mume na mke, na ni lazima wale pamoja?! Ni vema ikaeleweka kuwa, kubadili mazingira na kufanya vitu makhsusi kwa kushtukizana, huwafanya wanandoa kutozoeana na kuchokana, kwani maisha yenye mtindo na mtiririko mmoja kila siku humfanya mtu kuyachoka, ni vema wanandoa na hasa mwanamke kuwa mbunifu katika kuyapaka rangi mpya maisha yao kwa kubuni vitu vitakavyo tia ladha mpya katika nyumba, njia mojawapo ni hiyo ya kumualika chakula maalum mumewe peke yake, na hata kama itamlazimu kununua au kuagiza aina tofauti ya chakula basi afanye hivyo, na ampe mwaliko mumewe wa kutokosa kuhudhuria katika mnasaba huo. Aidha mwanamume naye anaweza kumualika mkewe katika hoteli ya heshima mlo wa mchana au usiku na kupata nafasi ya kujikumbusha mambo mazuri yaliopita.

g) Kubadilisha mpangilio wa nyumba: Wanawake wengi huwalalamikia waume zao kwa kutopenda kukaa nyumbani na badala yake kumaliza muda wao kwenye migahawa na kwa marafiki zao. Mke mwerevu huwa anafanya kila juhudi za kumnasa mumewe apende kukaa nyumbani wakati wa nafasi yake kwa kumbadilishia mazingira ya nyumba, kwani mazingira ya nyumba yanapokuwa ni yale yale tangu ndoa ilipofungwa hadi wanakuwa na watoto watatu, kochi lipo palepale kama kisiki cha mti, saa ya ukutani tangu imetundikwa mpaka imeshikana na ukuta, mapazia yaleyale na kama yanabadilishwa basi rangi ni zilezile, hali hii humfukuza mwanamume ndani ya nyumba na kumfanya arudi kuja kulala tu, na huu ndio mwanzo wa kuchokana na kuichoka nyumba.

h) Usafi wa mwili na mavazi: Moja miongoni mwa mambo yanayokera kwa wanandoa ni uchafu wa mmoja wao, uchafu ni sifa isiyovumilika hususan kwa mwanamke, baadhi ya wanawake hudhani kuwa manukato, vipodozi ndio usafi, utakuta anapitisha masiku bila kuoga kikamilifu, bali anapitisha pitisha maji na sabuni tu katika maeneo fulani, kisha kujijaza manukato, lotion na mafuta mengine, bila kuelewa kuwa, anapokuwa karibu zaidi na mumewe harufu ya asili hujitokeza na kuleta mchanganyiko wa harufu mbaya, hali kama hii si rahisi kwa mwanaume mstaarabu kuizungumzia kwa mkewe, atakaa nayo na atavumilia, lakini mwisho wake ni kumchoka mke huyu. Wanaume nao hudhani kuwa kwao wanaume ndio wamepewa kibali cha kuwa wachafu, kwa mfano wanaume wengi huona ni jambo la kawaida kunuka jasho, na wengine wana matatizo sugu ya kunuka miguu, huu ni uchafu ambao hauvumiliki kwa mwanamke msafi, aidha baadhi ya wanaume hawana vionjo katika mavazi yao, na jinsi wanavyojiweka, jambo ambalo linaweza kumsababishia mke maudhi, na hata kujihisi aibu kunasibishwa na mume wake.

i) Kufanya Ibada kwa pamoja: Nguzo muhimu na mhimili wa maisha ya ndoa ni kumcha Mungu/Allaah, Sala za usiku humkurubisha mja karibu zaidi na Mungu, hivyo mume na mke kuhimizana kufanya ibada hii pamoja huwazidishia imani na mapenzi baina yao na kuifanya ndoa yao kuwa imara zaidi.

 
Chanzo:  http://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/78716-chanzo-cha-kuchokana-katika-mahusiano-ndoa-na-ushauri-wa-kukabiliana-na-tatizo-hili.html

Tips for Your Long Distance Relationship

1. Use a web cam
A web cam is a great way to interact with your mate while you are apart. Connect your web cam to your computer and use your favorite messaging utility (MSN, Yahoo, AOL, etc.) and not only will you be able to hear your mate, but you will also be able to see your mate.

2. Take pictures of everyday activities and send them to your mate
A picture is worth a thousand words and can help you and your mate feel closer together in your long distance relationship. Today, with most cell phones equipped with a digital camera and cameras small enough to fit in your pocket, it’s very easy and convenient to take pictures and email them to your mate. With pictures, your mate can easily know what you are talking about when you describe the great party you went to or the new hairstyle that you just got. Some other examples of when you can take a picture are listed below:

* New outfit that your have purchased.
* Family or friends get together.
* Changes to your bedroom.
* Changes to your physical appearance (hairstyle, piercing, etc.)
*Pictures of your office or cubicle.

3. Send gifts to your mate’s from their local country or city
You can save a lot of money by searching the Internet for local companies to buy from and deliver your gifts. For example, if you are living in the United States and your mate is from Italy, find an Italian company that has the great gift that you want to send to your mate. In most cases, you will save on international shipping costs and you might even save on the currency exchange rate. Also, a local company will be able to deliver a gift much quicker for those last minute shoppers.

4. Use text-messaging capability to keep in touch more frequently
Text messaging can be a simple was to keep in touch with your mate in a long distance relationship. For those across the border relationships, this can also be an inexpensive way to communicate. It’s not always convenient to call, so text messages are a good alternative. You can send good night messages or little love notes throughout the day.

5. Trust your mate
Ideas of mistrust can easily seep into the minds of those involved in a long distance relationship because you don’t get to physically see your mate. They may be saying that they are not seeing anyone else, but how do you know that for sure hundreds or even thousands of miles away? This mistrust can ultimately lead to the relationship ending. You should approach the trust issue in a long distance relationship the same way as you would in a normal relationship. If there is no indication or evidence of cheating, it is most likely not happening.

6. Use Skype to call your mate and talk for free
Invest in a headset or a Skype phone to make free PC to PC calls anywhere in the world. If you would prefer to call a regular phone or a cell phone, Skype had very low and reasonable rates. Skype can save you and your mate a lot of money without a lot of hassle and technical setup. Just download the software for free from Skype and plug in your headset and now you are ready to talk for free.

7. Introduce your mate to your friends and family
How many times have you been out with your friends and you bring up your mate into conversation and your friends don’t believe he/she even exists? It is typical in a long distance relationship when two people visit each other they spend time only with each other. Although it is necessary to have time together, it is also necessary for your mate to experience other aspects of your life. Introduce him/her to your friends and family, so they can get to know your mate. It will only broaden your relationship and it will have a greater chance to succeed.

8. Visit each other frequently
This is not really a tip for a long distance relationship to be successful, but rather a requirement. To keep your long distance relationship going, you need to have in your mind the feeling and emotions of being with your mate. What keeps you together while you are apart is the idea of eventually being together. This can only be achieved by visiting each other whenever you have a chance.

9. Ease into being together
It can sometimes be difficult for two people who are involved in a long distance relationship to connect easily when they are together with their mate. Yes, you probably know everything about each other and talk everyday, but that is not a substitute for real contact. Both of you will need some time to adjust to being in each other’s presence. Be aware that it may take your mate longer than you and you should allow them that time.

10. Write letters and send cards
Nothing is more romantic than a handwritten letter or card that you send to your mate for no reason at all. Variety in a long distance relationship will help keep things new and fresh. Your mate will appreciate the fact that you took time out to write such a wonderful letter or sent a card.