Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Saturday, October 27, 2012

Mbunge ala mamiloni! Awauzia TANESCO matairi 300 alipwa fedha ya matairi 600

 


SIKU chache kabla ya kikao cha Bunge kuanza mjini Dodoma, zimeibuka taarifa kwamba mmoja wa wabunge aliyekuwa mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa alishiriki kikamilifu kuendesha biashara na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ambalo kimsingi anapaswa kulisimamia.

Taarifa hizo zimekuja huku tayari habari zilizovuja na kuandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari kudai kwamba uchunguzi wa kamati ya ndogo chini ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Maadili iliyokuwa chini ya Mbunge wa Mlalo, Brigedia Jenerali (mstaafu), Hassan Ngwilizi haikuwatia hatiani wabunge waliokuwa wakituhumiwa.


Hao walikuwa ni wabunge wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa na Spika Anne Makinda, waliokuwa wakituhumiwa kushiriki vitendo vinavyoashiria rushwa ndani ya TANESCO, kampuni ambayo aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wake, William Mhando amesimamishwa kwa tuhuma mbalimbali.


Taarifa za karibuni zaidi zinaonyesha kwamba mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo, Sarah Msafiri, alikuwa na uhusiano na Kampuni ya M/S Sharrif’s Services & General Supply iliyokuwa ikifanya biashara na TANESCO na yeye kusimamia malipo yenye utata kutoka shirika hilo ambalo mbunge huyo analisimamia.


Kampuni hiyo ilikuwa inasambaza matairi ya magari kwa TANESCO ikiwa na mkataba wa matairi yenye thamani ya shilingi milioni 387.


Anasema mtoa taarifa wetu kuhusu biashara hiyo ya matairi: “Yule mbunge ndiye aliyekuwa akija TANESCO wakati wa kufunga mkataba. Mkataba ulikuwa awali wa matairi 652. Baadaye idadi hiyo ilipungua yakaletwa matairi 356, lakini pamoja na matairi kupungua, kiasi cha pesa zilizolipwa kilibaki kilekile”.


Lakini wakati hayo yakiendelea, zipo pia taarifa kwamba uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini na hasa Waziri, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu Eliakim Maswi, umekuwa ukifuatilia kwa karibu taarifa zilizovuja za Kamati ya Ngwilizi zinazoonyesha kwamba ripoti ya Kamati hiyo imeukandamiza uongozi huo kwenye sakata linalouhusisha na tuhuma za rushwa za wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini.


Anasema mtoa habari wetu: “Baada ya kuanza kuvuja kwa ripoti hiyo walikutana kwa nia ya kutaka kujua kwanza kwamba kweli ripoti ya kamati ile imewatuhumu na hali ikiwa ni hiyo wafanye nini, maana wao si wanasiasa, achilia mbali kwamba Profesa Muhongo ni Mbunge wa Kuteuliwa.


“Hilo la kwamba wamekwenda kumwona Rais kumwambia kwamba wanataka kuondoka sijalisikia. Ninachojua ni kwamba walikutana. Na hiyo inatokana na ukweli kwamba hawa ni watu wawili wanaoshirikiana kwa karibu katika kuendesha wizara, hivyo mmoja akiondoka sioni uwezekano wa mwingine kubaki.


“Wizara hii pamoja na taasisi zake inahitaji watu waliojitoa kusaidia nchi. Na hawa huwezi kuwalinganisha na ile timu iliyoondoka. Wanapishana sana kwa malengo na maono. Sijui maisha yao yalivyo, lakini nawaona kama watu wasio na makubwa na wasiokuwa na tamaa ya mali.


“Kwa hali ya kiwango cha ufisadi tulichofikia kama nchi unahitaji ujasiri mkubwa, kwa mfano, kusema waziwazi kwamba sasa hapatakuwa na mgawo wa umeme tena.


“Kusema hivyo maana yake unajitangazia vita na matajiri na wanasiasa wapenda mali. Lakini hawa wamesema, na wamerudia mara kadhaa, kwamba mgawo uliokuwapo ulikuwa wa kutungwa, hata hotuba ya Waziri wakati wa Bunge la bajeti ilieleza hivyo. Hiyo si kazi rahisi. Lazima watapigwa vita.


“Hivi unafikiri Kamati ya Bunge ni ya malaika? Ile ilikuwa sawa na kesi ya nyani unampelekea ngedere”.


Katika mkutano ujao wa Bunge matokeo ya uchunguzi wa kamati iliyoundwa kuchunguza sakata zima la wabunge kuhongwa na wengine kuwa na maslahi katika TANESCO licha ya kuwa wao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, yatawasilishwa kwa Spika na baadaye kuwekwa wazi kwa wabunge.


Wabunge walijikuta katika mpasuko miongoni mwao hasa baada ya kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TANESCO, William Mhando na wenzake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu zilizokuwa zikiwakabili.


Tayari katika uchunguzi wa Mhando na wenzake zimebainika kasoro lukuki kuhusu mwenendo wao kama viongozi wa TANESCO. Hali pia si swari kwa upande wa Bodi ya TANESCO inayoongozwa na Jenerali (mstaafu) Robert Mboma, ikielezwa kuwa bodi hiyo kwa namna fulani ni sehemu ya uozo uliokuwa ukiendelea TANESCO ikiwa ni pamoja na kulea kile kinachoelezwa kuwa mgawo wa umeme wa kutengeneza ‘mezani.’


Na bado kachaguliwa CCM-NEC ?


CHANZO: Raia Mwema | 24 Oct 2012
        

WANAWAKE WANAVYOIVAA MIKENGE KWENYE NDOA..............!

 



Ngoja leo niyadadavue makosa yanayofanywa na wanawake wengi pale wanapoamua ni nani wa kuoana naye:

1. Kosa la kwanza, unaolewa na mtu ambaye unajua kabisa ni dhaifu na mkorofi, ukitarajia kwamba ataondoa kasoro zake akiwa ndani ya ndoa. Hili ni kosa kubwa. Kama huna furaha sasa na mtu kabla hujaoana naye, usikubali kuingia huo mkenge. Huwezi kutegemea mtu kuadilika aiwa ndani ya ndoa.

2. Kosa la pili, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu ya msisimko wa mwili kimapenzi lakini si kwa sababu ya tabia zake. Kuwa mwangalifu na neno “Nakupenda” neno hili mara nyingi maana yake ni “Nina uchu nawe.” Ndiyo amevutiwa nawekimaumbile, lakini undani wa tabia yake unaujua? Hapa kuna mambo manne… Kwanza, Je anapenda kutomfanyia binadamu mwenzie mabaya kama mabavyo yeye hataki kufanyiwa? Pili, anaishi vipi na watu wengine? Anaishi vipi na watu ambao ana uadui nao, Anawasamehe au analipiza visasi? Je anatoa misaada kwa masikini? Tatu, je ni mkweli, anachokisema ndicho anachokifanya? Je anaaminika? Majukumu anayoahidi kuyafanya anayatimiza? Nne, je anajipenda? Je ni mtu ambaye yuko imara kimapenzi au ni mtu wa kuyumbayumba na asiye na msimamo? Sio mtu akishauriwa na marafiki zake au ndugu zake huko, anakuja na maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu

3. Kosa la tatu, unaolewa na mtu ambaye hamna malengo na vipaumbele vya aina moja vya maisha. Je mna utashi wa aina moja? Kwa mfano ni vyema mwanamuziki akaolewa na mwanamuziki mwenzie kwa kuwa anajua mzingira ya kazi ya mwenzie ili kupunguza wivu wa kupindukia usio wa lazima

4. Kosa la nne, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu mnakutana kimwili mapema mno. Kukutana kimwili kabla ya ndoa kunaweza kuleta matatizo makubwa mno. Tendo la ndoa kabla ya ndoa hufunika uwezo wa mtu kufikiri. Mtu anabaki kufaidi na kubaki kujali mapenzi ya kimwili na kusahau kukuna ubongo juu ya mambo mengine. Ni lazima mwanamke akune ubongo ili kujua kama huyo mpenzi anakidhi vigezo vyote vya mume mtarajiwa.

5. Kosa la tano, unaolewa na mtu ambaye huna msisimko wa kimwili umwonapo. Kuna uwezekano mkubwa mwanamke akavutiwa na mwanaume kwa sababu ya aina ya gari analomiliki. Hapa hakuna msisimko wa kimwili bali mwanamke kavutwa na gari au rasilimali alizo nazo mwanaume huyo.

6. Kosa la sita, unaolewa na mwanaume anayependa kudhibiti. kuwa na tabia ya kudhibiti wenzako ni ya dalili za mtu jeuri na mwenye kujisikia na mfujaji. Naomba kutofautisha kati ya “kudhibiti” na “kutoa mawazo.” Mtu anayekupa mawazo ni kwa faida yako, lakini anayekudhibiti ni kwa faida yake.

7. Kosa la saba, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu unakimbia matatizo uliyo nayo. Unaweza kuwa hujaolewa na huna raha wala amani na ukataka kuolewa. Ndo haiwezi kukutatulia matatizo yako binafsi ya kisaikolojia nay a kimapenzi. Badala a kuyapunguza matatizo hayo, ndoa itayaoneza. Kama huna amani na huyafuahii maisha, chukua jukumu la kurekebisha matatizo hayo sasa kabla hujaolewa. Itakuwa ni faida kwako na kwa mmeo mtarajiwa.

8. Kosa la nane, unaolewa na mtu asiya sahihi kwa kuwa yuko ndani ya pembe tatu. Mtu ambaye anaishi na wazazi wake ni moja ya mfano wa mtu anayeishi katika pembe tatu. Watu wengine wanaoweza wakawa wanaishi ndani ya pembe tatu ni kama wanaofanya kazi saa 24! Huyu mtu halali? Watu wengine walio katika pembe tatu ni watu wanaotumia madawa ya kulevya, mtu anayetawaliwa na “hobbie” zake, anapenda sana michezo (Mpira), kuperuzi mitandao ya kijamii na anapenda sana fedha. Hakikisha kwamba wewe na mpenzi wako , nyote hamtawaliwi na pembe tatu. Mtu ambaye anatawaliwa na pembe tatu hawezi kumtimizia mpenzi wake haja ya upendo atakapokuwa anahitaji. Kama mpenzi wako anatawaliwa na pembe tatu kwa kiasi kikubwa, wewe huwezi kuwa kipaumbele chake.
 

WANAUME NA WANAWAKE WANAPOLALAMIKA ...........!


 



Ngoja niyadadavue malalamiko ya wanawake kwanza hapa chini:

1. Wanawake wanalalamika kwamba wanaume sio waelewa wazuri, yaani huwa wanatafsiri mambo tofauti na isivyo.

2. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawajali hisia za wapenzi wao wala hawajali pia kuhusu mahitaji yao.

3. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawajui kuonesha upendo , yaani hata wanapopenda inakuwa kama vile wanajisumbua tu, kiasi kwamba mwanamke anaweza kuhisi kwamba hapendwi.

4. Wanalalamika kwamba wanaume huwa hawana muda wa kucheza na wapenzi wao kabla hawajafanya nao mapenzi yaani hawawaandai kabla ya tendo, wao huwarukia tu na kumaliza haja zao haraka na kugeuka ukutani kabla ya wao (wanawake) hawajaridhika.

5. Wanalalamika kwamba wanaume hawana mawasiliano, huwa hawajui kueleza hisia zao na mawazo yao, bali ni watu wa kunyamaza na kujifungia kwenye dunia yao wenyewe. Wanahisi kama kuelezea hisia zao na mawazo yao ni kuwa dhaifu.

6. Wanawake hulalamika kwamba, wanaume hawana muda wa kukaa nyumbani na familia zao, kwa sehemu kubwa ni watu wa nje tu.

7. Wanawake pia wanawalaumu wanaume kwamba, hawajali mustakabali wa usafi au kupendeza kwa nyumba.

8. Wanawake wanawalalamika kwamba, wanaume huwa wanafanya maamuzi yao bila kujali kuwa wanawake wapo na wanaweza kuwa na michango mizuri sana kwa hicho wanachotaka kukifanya. Huamua kama kwamba wanawake siyo sehemu ya familia.

9. Wanalaumu kwamba, wanaume ndiyo wanaoanzisha au kuendekeza kutoka nje ya ndoa ukilinganisha na wao wanawake.



Malalamiko ya wanaume nayo nayadadavua kama ifuatavyo…..

1. Wanaume wanalalamika kwamba wanawake ni watu wa kulalamika, kukosoa na wenye vijineno vya hapa na pale visivyo na maana na vyenye kukera.

2. Wanaume wanalalamika kwamba wanawake wanajaribu sana kuwadhibiti na kuwakandamiza pale wanapoachiwa nafasi kidogo.

3. Wanaume wanadai kwamba wanawake huwa hawana furaha, mara nyingi wanaonekana kama vile wako kwenye simanzi fulani na wanapenda sana kununanuna hasa pale wanaume wanaposhindwa kuwatekelezea kile walichotaka hata kama hakina umuhimu kwa wakati ule.

4. Wanaume wanalalamika sana kwamba wanawake wanawanyima unyumba kama adhabu ya kuwakomoa. Siyo kuwakomoa tu, bali huwa wanafanya hivyo kwa lengo la kuwashurutisha wakubaliane na utashi wao fulani.

5. Lalamiko lingine la wanaume kuhusu wanawake ni lile la kwamba, huwa hawafikirii kwa mantiki, bali mara nyingi kufikiri kwao huwa kunakumbwa na mhemko. Kwa hiyo, uamuzi wao mwingi hauangalii mantiki bali hujali zaidi hisia zao.

6. Wanawake wanalalamikiwa na wanaume kwamba, hali zao za kihisia huwa hazitabiriki. Yaani huwa zinabadilika kufuatana na mabadiliko ya miili yao ya kihomoni miilini mwao nyakati kama zile za siku zao(hedhi), nyakati za ujauzito na hata wanapokoma kuziona siku zao(menopause) .

7. Wanaume wanawalalamikia wanawake kwa tabia yao ya umbea, kwamba midomo yao huwasha sana hadi waseme kile walichokiona au kukisikia hata kama si lazima na pengine ni hatari.

8. Wanawake wanalalamikiwa pia na wanaume kwamba, huwa wanatoka nje ya ndoa, hasa wanapohisi kukosewa upendo ndani, jambo ambalo haliwezi kuleta suluhu kwa tatizo hilo.

Kama wewe ni mwanaume na umegundua kwamba moja au baadhi ya malalamiko ya wanawake yanakugusa inabidi ubadilike na kufanya kinyume chake. Kama wewe ni mwanamke pia hali ni kama hiyo. Kama kweli una mdomo mwingi kwa mfano, ujue wanaume hawapendi tabia hiyo, hivyo huna budi kubadilika.
 

Chanzo cha kuchokana katika mahusiano/ndoa na ushauri wa kukabiliana na tatizo hili

Je unahisi umeshaanza kumchoka mmeo ama mkeo????!!!!


Imeandikwa na Shams Elmi (Abu 'Ilmi)

Takriban katika maisha ya wanandoa walio wengi kama sio wote, ndoa zao hupitia katika vipindi tofauti. Kama ulivyo umri wa Binadamu, ndoa hupitia katika kipindi cha utoto, ujana na uzee, na kila kipindi kina mambo yake na taratibu zake ambazo kama wanandoa watashindwa kuzifuata basi huenda ndoa hiyo ikakumbwa na mtihani mkubwa, nao ni mtihani wa kuchokana.

Utoto wa Ndoa:

Wengine hukiita kipindi hiki (Honey Moon) mwezi wa asali, kipindi cha raha, utulivu, mapenzi, maelewano baina ya wanandoa. Si lazima kiwe mwezi mmoja kama watu wengi wanavyoamini, bali kinaweza kikawa chini ya mwezi mmoja au zaidi ya mwezi mmoja.


Ujana wa Ndoa:

Hiki ni kipindi kinachofuatia baada tu ya utoto wa ndoa, ni kipindi ambacho kila mmoja miongoni mwa wanandoa anakuwa tayari ameshamtambua mwenzake katika shaksia yake (personality) kwa maana ya jinsi anavyoangalia mambo, jinsi anavyofikiri, mitazamo yake, mielekeo yake na matarajio yake.

Uzee wa Ndoa:

Kipindi hiki ni kipindi ambacho wanandoa wanakuwa tayari wameishaingia katika majukumu ya kulea kwa kupata matunda ya ndoa yao ambayo ni mtoto au watoto.

Kuchokana kwa wanandoa ni tatizo ambalo linatokea kwa familia nyingi, na kusababisha migogoro mingi na hata kufikia familia kuvunjika au kuishi kwa ajili tu ya kulea watoto na si vinginevyo.

Utakuta katika baadhi ya familia, Baba na Mama wanaishi katika nyumba moja, ukiwaona utadhani ni mume na mke wanaopendana, kumbe wanaishi kwa ajili tu ya kuwalea watoto wao na kuogopea maneno ya watu, hali hii ni hali ya talaka ya kimapenzi (emotional Divorce) na ni hali mbaya ambayo mara nyingi humpa msukumo mwanamume wa kuoa mke wa pili katika harakati za kutafuta utulivu na sehemu ya kukimbilia

Tatizo hili la kuchokana kwa wanandoa linasababishwa na wanandoa wote wawili kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya haki za mume na mke.
Hivyo basi, sababu kubwa ya wanandoa kuchokana, au kuzeeka kwa ndoa kunasababishwa na mwanamke, pale ambapo atashindwa kutumia nafasi yake na vipawa alivyopewa kuleta utulivu katika ndoa yao, na hapa nitajaribu kujadili baadhi ya visababishi vinavyopelekea kuzeeka kwa ndoa au kuchokana visababishi ambavyo huwa vinadharaulika na kuonekana vitu vidogo vidogo hususan kwa wanawake wengi.

a) Kuzoeana: kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususan kwa upande wa mwanamke kwa kutojali usafi wake, mavazi anayovaa, chakula anchopika, nidhamu ya nyumba na mpangilio kwa ujumla. Matatizo mengi ndani ya nyumba yanaweza kusababishwa na moja au baadhi ya tabia hizo, ambazo huenda ikawa hazitokani na dharau, bali kuzoeana, kwa mfano: siku za utoto wa ndoa mwanamke huwa anajali sana usafi wa mwili wake, umaridadi wa nguo anazovaa, usafi wa nyumba na nidhamu ya hali ya juu, upishi wa chakula unaozingatia vionjo na ubunifu, mapokezi yenye bashasha na wakati mwingine hata kumkumbatia mumewe arudipo kutoka kazini. Lakini baada ya kuzoeana yote hayo hubadilika, mwanamke huhisi kuwa hana jipya la kumuonyesha mumewe, hujiona wameishakuwa watu wazima sasa, na mara nyingi utakuta mwanamke huyu anashinda na sare (uniform) moja kuanzia asubuhi hadi anapopanda kitandani usiku, mambo ya Hinna, nguo za fashion, salon, manukato, kujipamba na dhahabu huyafanya pale anapotoka kwenda harusini na sio nyumbani. Huku ndio kuzoena, na tafsiri sahihi ni kudharau.

b) Mazungumzo: Mazungumzo ni njia muhimu ya kujenga ndoa na kuiimarisha , aidha ni njia ya mkato ya kuchokana na kuchukiana. Mwanamke ambaye hajui wakati gani aseme nini na wakati gani asiseme, hujikuta katika wakati mgumu ndani ya ndoa yake. Kwa mfano: Mwanamke ambaye kila anapoongea na mume wake huanza mazungumzo yake na matatizo na lawama humfanya mumewe awe na woga kila anaposikia sauti yake, na kuiona nyumba chungu, kwa sababu hakuna binadamu anayependa kusikia matatizo tu wakati wote. Mwanamke wa aina hii huwa anamsubiri mumewe kwa hamu kubwa, na anapofika tu na kabla hata ya kupata rizki, anaanza kumsomea orodha ya matatizo; watoto wamerudishwa shule, karo haijalipwa, shangazi yako amepiga simu mjomba kalazwa Hospitali na kadhalika na kadhalika. Nyumba ya aina hii huzeeka haraka na wanandoa kuchokana.

c) Kusomana Tabia: ni udhaifu mkubwa kwa wanandoa ambao wana mwaka mmoja katika ndoa yao wakawa bado hawajasomana tabia, au wakawa wameishasomana tabia, lakini kila mmoja akawa anataka tabia zake ndio ziwe dira. Kwa mwanamke mwenye busara na mwenye kuithamini ndoa yake, husoma tabia za mumewe na kuangalia jinsi gani anavyoweza kuzioanisha na zile zake ili kuepusha migongano, aidha hutafuta fursa muafaka ya kumkinaisha mumewe juu ya fikra fulani au tabia fulani ambayo yeye haridhiki nayo. Ni muhimu kwa mwanaume vilevile kuzisoma tabia za mke wake, vitu gani vinamuudhi, na vitu gani vinamfurahisha.

d) Kutamka na kudhihirisha mapenzi: Ni muhimu sana kwa wanandoa ili kuyaimarisha mapenzi yao yasiote mvi, kutamkiana hisia zao za kupendana bila utangulizi wowote, kwa mume au mke kumwambia mwenzake NAKUPENDA kuna athari nzuri katika nafsi kuliko hata ungemletea zawadi ya kitu cha gharama.

e) Kupeana zawadi: Zawadi ni njia nzuri ya kudhihirisha mapenzi yako na nafasi ya mwenzako katika maisha yako, na zawadi ambayo mtu huitoa kwa mwenzake bila ya utangulizi au mnasaba maalum huleta athari njema na huimarisha mapenzi. Na katika zoezi hili la kupeana zawadi, ni vema kila mmoja akaelewa anachokipenda mwengine ili zawadi iwe na athari inayotarajiwa, na iwe ni zawadi maalum kwa mlengwa, isiwe zawadi ambayo mtoaji naye atafaidika na zawadi hiyo, kwa mfano, si vema kwa mwanamme kumletea mkewe zawadi ya sufuria, microwave, pazia, Dinner set, hiyo haitaitwa zawadi, lakini ni juu yake kumletea manukato ayapandayo, hereni, bangili, mkufu au pete ya dhahabu, na vitu ambavyo ni maalumu kwa matumizi yake binafsi. Hali kadhalika kwa mwanamke kumzawadia mumewe achunge vigezo hivyo.

f) Kualikana vyakula: Inaweza kushangaza kuwa vipi wanandoa wataalikana chakula wakati wenyewe ni mume na mke, na ni lazima wale pamoja?! Ni vema ikaeleweka kuwa, kubadili mazingira na kufanya vitu makhsusi kwa kushtukizana, huwafanya wanandoa kutozoeana na kuchokana, kwani maisha yenye mtindo na mtiririko mmoja kila siku humfanya mtu kuyachoka, ni vema wanandoa na hasa mwanamke kuwa mbunifu katika kuyapaka rangi mpya maisha yao kwa kubuni vitu vitakavyo tia ladha mpya katika nyumba, njia mojawapo ni hiyo ya kumualika chakula maalum mumewe peke yake, na hata kama itamlazimu kununua au kuagiza aina tofauti ya chakula basi afanye hivyo, na ampe mwaliko mumewe wa kutokosa kuhudhuria katika mnasaba huo. Aidha mwanamume naye anaweza kumualika mkewe katika hoteli ya heshima mlo wa mchana au usiku na kupata nafasi ya kujikumbusha mambo mazuri yaliopita.

g) Kubadilisha mpangilio wa nyumba: Wanawake wengi huwalalamikia waume zao kwa kutopenda kukaa nyumbani na badala yake kumaliza muda wao kwenye migahawa na kwa marafiki zao. Mke mwerevu huwa anafanya kila juhudi za kumnasa mumewe apende kukaa nyumbani wakati wa nafasi yake kwa kumbadilishia mazingira ya nyumba, kwani mazingira ya nyumba yanapokuwa ni yale yale tangu ndoa ilipofungwa hadi wanakuwa na watoto watatu, kochi lipo palepale kama kisiki cha mti, saa ya ukutani tangu imetundikwa mpaka imeshikana na ukuta, mapazia yaleyale na kama yanabadilishwa basi rangi ni zilezile, hali hii humfukuza mwanamume ndani ya nyumba na kumfanya arudi kuja kulala tu, na huu ndio mwanzo wa kuchokana na kuichoka nyumba.

h) Usafi wa mwili na mavazi: Moja miongoni mwa mambo yanayokera kwa wanandoa ni uchafu wa mmoja wao, uchafu ni sifa isiyovumilika hususan kwa mwanamke, baadhi ya wanawake hudhani kuwa manukato, vipodozi ndio usafi, utakuta anapitisha masiku bila kuoga kikamilifu, bali anapitisha pitisha maji na sabuni tu katika maeneo fulani, kisha kujijaza manukato, lotion na mafuta mengine, bila kuelewa kuwa, anapokuwa karibu zaidi na mumewe harufu ya asili hujitokeza na kuleta mchanganyiko wa harufu mbaya, hali kama hii si rahisi kwa mwanaume mstaarabu kuizungumzia kwa mkewe, atakaa nayo na atavumilia, lakini mwisho wake ni kumchoka mke huyu. Wanaume nao hudhani kuwa kwao wanaume ndio wamepewa kibali cha kuwa wachafu, kwa mfano wanaume wengi huona ni jambo la kawaida kunuka jasho, na wengine wana matatizo sugu ya kunuka miguu, huu ni uchafu ambao hauvumiliki kwa mwanamke msafi, aidha baadhi ya wanaume hawana vionjo katika mavazi yao, na jinsi wanavyojiweka, jambo ambalo linaweza kumsababishia mke maudhi, na hata kujihisi aibu kunasibishwa na mume wake.

i) Kufanya Ibada kwa pamoja: Nguzo muhimu na mhimili wa maisha ya ndoa ni kumcha Mungu/Allaah, Sala za usiku humkurubisha mja karibu zaidi na Mungu, hivyo mume na mke kuhimizana kufanya ibada hii pamoja huwazidishia imani na mapenzi baina yao na kuifanya ndoa yao kuwa imara zaidi.

 
Chanzo:  http://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/78716-chanzo-cha-kuchokana-katika-mahusiano-ndoa-na-ushauri-wa-kukabiliana-na-tatizo-hili.html

Tips for Your Long Distance Relationship

1. Use a web cam
A web cam is a great way to interact with your mate while you are apart. Connect your web cam to your computer and use your favorite messaging utility (MSN, Yahoo, AOL, etc.) and not only will you be able to hear your mate, but you will also be able to see your mate.

2. Take pictures of everyday activities and send them to your mate
A picture is worth a thousand words and can help you and your mate feel closer together in your long distance relationship. Today, with most cell phones equipped with a digital camera and cameras small enough to fit in your pocket, it’s very easy and convenient to take pictures and email them to your mate. With pictures, your mate can easily know what you are talking about when you describe the great party you went to or the new hairstyle that you just got. Some other examples of when you can take a picture are listed below:

* New outfit that your have purchased.
* Family or friends get together.
* Changes to your bedroom.
* Changes to your physical appearance (hairstyle, piercing, etc.)
*Pictures of your office or cubicle.

3. Send gifts to your mate’s from their local country or city
You can save a lot of money by searching the Internet for local companies to buy from and deliver your gifts. For example, if you are living in the United States and your mate is from Italy, find an Italian company that has the great gift that you want to send to your mate. In most cases, you will save on international shipping costs and you might even save on the currency exchange rate. Also, a local company will be able to deliver a gift much quicker for those last minute shoppers.

4. Use text-messaging capability to keep in touch more frequently
Text messaging can be a simple was to keep in touch with your mate in a long distance relationship. For those across the border relationships, this can also be an inexpensive way to communicate. It’s not always convenient to call, so text messages are a good alternative. You can send good night messages or little love notes throughout the day.

5. Trust your mate
Ideas of mistrust can easily seep into the minds of those involved in a long distance relationship because you don’t get to physically see your mate. They may be saying that they are not seeing anyone else, but how do you know that for sure hundreds or even thousands of miles away? This mistrust can ultimately lead to the relationship ending. You should approach the trust issue in a long distance relationship the same way as you would in a normal relationship. If there is no indication or evidence of cheating, it is most likely not happening.

6. Use Skype to call your mate and talk for free
Invest in a headset or a Skype phone to make free PC to PC calls anywhere in the world. If you would prefer to call a regular phone or a cell phone, Skype had very low and reasonable rates. Skype can save you and your mate a lot of money without a lot of hassle and technical setup. Just download the software for free from Skype and plug in your headset and now you are ready to talk for free.

7. Introduce your mate to your friends and family
How many times have you been out with your friends and you bring up your mate into conversation and your friends don’t believe he/she even exists? It is typical in a long distance relationship when two people visit each other they spend time only with each other. Although it is necessary to have time together, it is also necessary for your mate to experience other aspects of your life. Introduce him/her to your friends and family, so they can get to know your mate. It will only broaden your relationship and it will have a greater chance to succeed.

8. Visit each other frequently
This is not really a tip for a long distance relationship to be successful, but rather a requirement. To keep your long distance relationship going, you need to have in your mind the feeling and emotions of being with your mate. What keeps you together while you are apart is the idea of eventually being together. This can only be achieved by visiting each other whenever you have a chance.

9. Ease into being together
It can sometimes be difficult for two people who are involved in a long distance relationship to connect easily when they are together with their mate. Yes, you probably know everything about each other and talk everyday, but that is not a substitute for real contact. Both of you will need some time to adjust to being in each other’s presence. Be aware that it may take your mate longer than you and you should allow them that time.

10. Write letters and send cards
Nothing is more romantic than a handwritten letter or card that you send to your mate for no reason at all. Variety in a long distance relationship will help keep things new and fresh. Your mate will appreciate the fact that you took time out to write such a wonderful letter or sent a card.

Friday, April 6, 2012

Poleni watu wa Mtera kwa kuanguka mikononi mwa chizi

 
Mbunge wa Mtera CCM, Livingstone Lusinde aka Kichaa akirapu rapu zake za matusi  ya nguoni kule Arumeru Mashariki hivi karibuni.

KAMPENI zilizopita za uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, zilifichua mambo mengi hasa uhovyo wa siasa na viongozi wetu. Mambo yalianza na wazee wazima Benjamin Mkapa, rais mstaafu, kujivua nguo kwa kujifanya msemaji wa ukoo wa marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye alimtengeneza na kumnadi Mkapa lakini baadaye akamwangusha vibaya kiasi cha kufa akiwa analilia Watanzania wake.

Nani mara hii kasahau maneno ya mke wa marehemu, Mama Maria Nyerere aliyesema kuwa maneno ya mwisho ya mumewe yalikuwa, "Nawalilia Watanzania wangu"?

Hii maana yake Mwalimu alikufa na roho iliyojikunja; ikizingatiwa Watanzania aliokuwa akiwalilia walikuwa kwenye mikono ya mtu wake lakini aliyeonyesha wazi kuwa wa hovyo kisera.

Mwingine aliyejivua nguo ni mzee Stephen Wassira, Waziri wa Uhusiano na Uratibu Ofisi ya Rais ambaye alianzisha ligi ya matusi na uongo kwenye kampeni kiasi cha kugeuka kuwa uwanja wa wahuni wa chama chake kuja kuonyesha uhuni na uhovyo wao. Wassiara alikaririwa akimtuhumu katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa kula pesa ya maandalizi ya ujio wa Papa John Paul II mwaka 1990, madai ambayo yalipingwa vikali na Kanisa Katoliki ambalo bosi wake ndiye alikuwa akitembelea Tanzania.

Rais wa TEC, Askofu Mkuu Juda Thaddeus Ruwa'ichi alimjibu Wassira kwa maneno haya, “Ukiona mwanasiasa anakurupuka na kuanza kumchafua mwenzake ujue amefilisika, vitendo hivyo vinaonyesha udhaifu kwa nchi katika nyanja za siasa,”

Hayo ya Mkapa na Wassira yalikuwa cha mtoto au tuseme ufunguzi tu. Maana baba yao katika ligi hii ya matusi, Mbunge Livingstone Lusinde wa Mtera (CCM) alikuwa hajaja kumaliza kazi hii aliyotumwa na chama chake. Alikaririwa akitamka maneno ambayo si vizuri kuyarudia na wala hayafanani na mtu wa umri na wadhifa wake kama mbunge mwakilishi wa wananchi. Hivi mtu anayeweza kusimama kwenye jukwaa la siasa kutangaza sera akatangaza matusi tena kwa kuiga maneno ya vikundi vya maigizo, umuweke kundi gani? Zamani wengi tulikuwa tukikwazwa na salamu za Mkapa za kihuni za “MAMBO” bila kujua kuwa kumbe kuna wahuni zaidi.

Lusinde alikaririwa akisema kuwa kama CHADEMA ni vichaa wa kurogwa basi yeye ni wa kuzaliwa. Ni bahati mbaya na hasara kuwa na viongozi aina ya Lusinde. Je, ilikuwaje watu wa Mtera wakamchagua chizi anayekiri kuwa chizi tena tangu kuzaliwa? Je, alipitaje kwenye mchujo au ni yale yale ya wananchi kuchoka utawala wa mtu mmoja na wa kurithishana kutokana na ukweli kuwa mbunge wao wa zamani John Malecela alikuwa amewachosha kwa kukaa madarakani kwa muda mrefu?

Nashindwa kujua mantiki ya kumchagua mtu wa hovyo na kichaa kama huyu anayeweza kusimama jukwaani na kuwadhalilisha wenzake tena mbele ya watoto wadogo akionyesha uhodari wa kuchambua mavazi ya wenzake badala ya matatizo ya anaowawakilisha?
Hivi mbunge anaposimama jukwaani na kugeuza mdomo wake sehemu ya kutolea uchafu, tena mbele ya kadamnasi na watoto, anajenga picha gani? Je, huu si ushahidi tosha kuwa CCM imeishiwa kiasi cha kushabikia uhuni na mipasho ya kipumbavu? Je hii si kuigeuza CCM kuwa Chama Cha Matusi? Hata waimbaji wa taarabu za matusi na hata rap wana afadhali kwa vile wayafanyayo ni saizi yao.

Sijui kama Lusinde anasoma hata magazeti zaidi ya yale ya udaku kama alivyothibitisha kwa kauli zake za kichovu na kiwendawazimu. Je, maneno na tabia vya Lusinde vinakisaidiaje chama chake zaidi ya kukibomoa? Maana ukiangalia kuzodolewa, kwa mfano, kwa Wassira hata Mkapa ni ushahidi tosha kuwa CCM iko pabaya na imeishiwa.

Je yote haya ni matokeo ya kuua maadili na kuingiza madili kwenye nafasi yake? Maana kwa nchi yenye kufuata sheria na kanuni za maadili, tume ya uchaguzi (NEC) ilipaswa kutoa tamko hata karipio mara moja Lusinde alipogeuza kampeni uwanja wa kushindanisha ukichaa na matusi ya nguoni.

Hivi mtu anayeweza kuwaita wanaume wenzake mashoga na wajawazito ana akili kweli? Heri angeishia pale. Wenye mtindio wa akili wenzake wangedhani amewajibu wapinzani japo siyo. Nani mara hii alivyowaambia wapiga kura kuwa yeyote ambaye hataichagua CCM ni mjamzito? Je, ujauzito ni ugonjwa? Hivi bila ujauzito mama yake angemzaa kweli? Je kutukana watu kwa kutumia ujauzito si kuwadhalilisha wanawake na mama yake akiwamo? Maana huo ujauzito usio na baba maana yake ni umalaya.

Maneno ya Lusinde ni ushahidi kuwa hakupata malezi mema wala elimu ya kutosha kiasi cha kujenga taswira kuwa huenda alizaliwa mitaani. Maana hata tofauti na wahuni wanaopiga debe kwenye mabasi ya daladala wala wauza mitumba Mtaa wa Kongo. Heri ya wao wamefukarishwa na akina Lusinde kuliko Lusinde anayelipwa kodi ya wananchi kwa kuchafua maadili akilinda na kutetea uozo na mgando wa mawazo. Tena uoza wenyewe utawala wa kurithishana kama walivyoonyesha kwenye kuteua wabunge wa Jumuia ya Afrika Mashariki!

Kama siyo CHADEMA kuchelea kukimbizana na kichaa, ilifaa afunguliwe mashitaka. Hata hivyo, kwa kauli za watajwa watatu, kama CHADEMA watashindwa basi wana kila sababu ya kwenda mahakamani na kudai uchaguzi haukuwa huru na wa haki. Maana haki na uhuru ni heshima na si kashfa tena za kuzua na matusi. Laiti Lusinde angewatuhumu CHADEMA mambo ya kweli, hakuna ambaye angehangaika naye. Litakuwa jambo la ajabu na hatari kama CCM na Tume ya Uchaguzi hawatamchukulia hatua za kinidhamu tena za wazi Lusinde.

Kuna haja ya wachambuzi wa mambo kudodosa na kupata historia ya Lusinde ili apewe msaada na wale waliofanya kosa kumwamini wadhifa wa heshima kama ubunge. Kimsingi lugha na matusi ya Lusinde yamewadhalilisha wabunge wote hasa wa chama chake na uongozi mzima. Hivi kama Lusinde ana mke na watoto hata wazazi wake sijui amewaumiza kiasi gani kwa kujivua nguo hadharani hivyo? Poleni sana watu wa Mtera. Huenda ni yale yale kuwa atukanaye wakubwa haishii na mmoja.

Alimtukana John Malecela akazoea sasa anataka kumtukana kila apitaye. Si ajabu akitofautiana hata na mwenyekiti wake hatakosa kumfurumshia mitusi ya nguoni kama alivyozoeshwa na chama chake. Poleni wapiga kura wa Mtera kwa kudhalilishwa na Lusinde ambaye aliwakilisha matusi badala ya heshima na matatizo yenu.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 4, 2012.

Mbunge ‘Chichim’ alivyomwaga mitusi Arumeru

LEO tumeamua kukaa kikao cha wanakijiwe wote ili kumjibu chizi mmoja aitwaye mheshimiwa japo sisi si machizi. Kama mkituona machizi shauri yenu. Tunaweza kuonekana walevi kutokana na kunywa kahawa na shida nyingi lakini bado si machizi kama Leavingstorm Lushinde chizi nambari wani wa Chama Cha Machizi (CCM).

Mie kama mwenyekiti naanzisha mjadala.
Nilikohoa kidogo na kuanza, “Waheshimiwa wanywa kahawa, kwanza naona mmechukia kutokana na matusi yalivurumishwa na mbunge wa ndugu yetu na rafiki yetu Mbwamwitu ambaye ni mpiga kura wa jimbo la Mtela,”

Wote kwa pamoja wanatikisa vichwa wakiashiria kukubaliana na pwenti yangu. Naendelea, “Mie leo si msemaji bali mwezeshaji. Hivyo naomba rasmi nifungue kikao hiki kitukufu ambacho licha ya kumjadilli huyu bwana kitatoa maazimio.”

Mbwamwitu anaamsha mkono na ninamruhusu arambe mic. Anaanza, “Ndugu zangu nashukuru sana kwa kuliona hili na pole zenu nimezipokea ingawa bado roho inaniuma. Hata hivyo msishangae sana. huyu jamaa kama alivyosema kweli ni chizi na aliwahi kukamatwa mara nyingi kwa makosa ya kuvuta bangi, udokozi na mazambe mengine mengi. Hivyo nina wasi wasi alipokuwa akiwekwa ndani mara nyingi, huenda lolote limemtokea na ndiyo maana anawasingizia wenzake kufanyiwa mchezo mbaya kama alivyowahi kufanyiwa.”

Kabla ya kuendelea Mchunguliaji anakula mic, “Hakuna kitu kimenikera kama jamaa kuwaita wenzake mashoga kiasi cha kutufanya tuamini yeye ndiye. Halafu anawatukana watu eti wana mimba, kwani mama yake alimzaa bila kubeba hiyo mimba? Huyu jamaa inaonekana anawadhalilisha akina mama akiwamo mama yake wallahi,”

Wakati Mchunguliaji akimwaga usongo wake, Mzee Kidevu anadandia, “Huyu jamaa kweli chizi nimeamini. Kwanza, huyu chizi kihiyo hajui hata Kiswahili. Mnakumbuka aliposema eti dokta Silaha aliposema ana uchungu na nchi hii eti alimshagaa mwanaume anawezaje kuwa na uchungu? Kwani uchungu ni wa kuzaa tu?”

Mara Mipawa anachomekea, “Jamaa ana ugomvi na mimba huyu. Huenda kichaa chake kinachukia mimba.”

Watu hawana mbavu wanacheka ingawa habari yenyewe si ya kuchekesha zaidi ya kuhuzunisha. Mara Mbwamwitu anakatua mic tena, “Basi mwenzenu nina uchungu naye. Laiti nikikutana naye kwenye kiza ataipata hiyo mimba anayowapa wenzake. Huyu inaonakana anataka kupewa mimba.”

Msomi Mkatatamaa aliyekuwa kimya muda wote aliamua kutia guu, “Jamani msijipasue vichwa. Kimsingi, Lushinde alichofanya ni kuthibitisha madai ya siku nyingi kuwa chama chake kimeishiwa sera. Kilianza na usanii, kikachemsha. Kilidandia uongo, kimechemsha. sasa kimeona haitoshi kimedandia matusi.” anavuta kombe lake na kubwia kahawa na kuendelea, “Matusi ya Lushinde kimsingi si ya kuwahuzunisha wala kuwalenga wapinzani bali chama chake na viongozi wake waliokuwa wakichekelea alipokuwa akitumia mdomo wake kutoa haja kubwa. This annoyed me to death so to speak.”

Anakatua kashata na kuendelea. “Kila mtu kwake shoga. Inakuwa vigumu kujua huyu bwana kwanini anapenda sana ushoga na kuchukia mimba,” Msomi Mkatatamaa alizidi kuchanja mbuga kwa taaluma na busara zake baada ya wazee kumwambia apunguze hasira kuongea kikameruni hata kama alikuwa akiongelea habari za mkameruni mhishimiwa.

Aliendelea, “Hakika wazazi wake, mke wake, watoto wa Mkameruni Lushinde wamekula hasara. Anavyowatia aibu sina hamu. Hata yule mheshimiwa Sonko wa Nonihino huvuta bangi, kunywa gongo na kupayuka lakini hajawahi kuona mdomo choo kama wa Lushinde. Maana kama sera basi chama chake cha Matusi (CCM) kimepata mpiga debe. Ila itakuwa muujiza kama walengwa wa makombora ya Lushinde wasipomfikisha mhakamani. Sisi kijiweni ukimtukana mjumbe au mwenyekiti tunasema umetukana kijiwe kizima. Hivi Lushinde anapotukana wabunge si kama anatukana jimbo zima?”

Nami sikujivunga. Nilichomekea, “Namkaribisha Lusenge sorry Lushinde aende Kijiweni Mwenge akapige debe au akiweza aende zake gerezani akauze unga. Namshauri Lushinde aje nimuonyesha picha niliyopiga na mzee Matonya ili aone tofauti ya masikio yaliyotobolewa kimila na haya ya kishoga.” wanakijiwe hawana mbavu.

Mgosi Machungi naye hataki kikao kiishe bila kukifunga. Anakula mic, “Mie sikujua kuwa kumbe Ushinde na wenzake wamechanjwa makalioni tena na poofesa Maji Mafupi. Angejua aipotoka kwao N’koogwe akaja Ushoto kue Irente kutafuta wachawi kioo chake kiivunjika akarudi kwa haraka.”

Mpemba “Yaelekea huyu jamaa ashafungwa sana na kufanyia nchezo mbaya kiasi cha kudhani kila aendaye jela afanyiwa nchezo kama alofanyiwa,” kijiwe hakina mbavu.

Mchunguliaji. Msomi mkatatamaa anaamua kurejea ili kutoa usomi na busara zake. Tunamheshimu na kumtegemea sana maana huwa hana mdomo mchafu ingawa leo ameudhika kiasi cha kuvunja mwiko na kutoa lugha ya ukali. Anakatua mic, “Nilipokuwa masomoni ulaya nilizoea kusikia watu wenye midomo mibovu kama hivi wakiitwa Chiwawa yaani vijimbwa vidogo vinavyobweka sana vikimuona mtu lakini akivikaribia vinafyata mkia na kutoka mkuku,”

Anakunywa kahawa yake na kuendelea, “Kwa hiyo sitashangaa kama Chakudema hawatamchukulia hatua chiwawa huyu maana wanajua chiwawa ni chiwawa hata ukimpeleka mahakani bado hakimu atamuachia kwa vile ni chiwawa.”

Mzee Kidevu anatuacha hoi. Anasema, “Ingawa mie sijawahi kwenda Ulaya, anawajua hawa mbwa ambao Kiswahili huitwa kusiri. Hivyo, tuna bahati mbaya kuwa na mbu… samahani simalizii mwenye tabia kama za kusiri. Je, tuseme hiki ni chama cha Makusiri?

Wanakijiwe tunaangaliana kuonyesha jinsi mzee mwenzetu alivyochomekea kitu kingine kwani Kusiri na Chiwawa ingawa wote ni mbwa. Wanakutana kwenye sifa moja yaani uchizi wa kubweka bweka hovyo.

Mpemba ambaye alikuwa akibofyabofya simu yake kiasi cha kuachwa nyuma kimaongezi anastuka na kula mic, “ Yakhe mie naona kama huyu jamaa ashaingiliwa na popobawa. Maana popobawa siku zote aja wakati wa uchaguzi na apenda sana wao wa chama cha Machizi kwani naye chizi.”

Wajumbe hawana mbavu. Wakati tukijiandaa kuendelea na kikao si chizi Lushinde alipita na mshangingi wake. Tuliinuka na kumtoa nje tayari kumfanyizia ili tumpige picha na kuonyesha umma alivyo chakula. Usimwambie mtu, kuwa kweli jamaa si riziki.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 4, 2012.

HOTUBA YA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MH. EZEKIEL MAIGE (MB) KATIKA UZINDUZI WA BODI YA WAKURUGENZI YA BODI YA UTALII TANZANIA (TTB)

Mhe.Ezekiel Maige
Ndugu Mwenyekiti wa Bodi, Balozi Charles A. Sanga;
Ndugu Wakurugenzi wa Bodi;
Ndugu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii;
Menejimenti ya Bodi ya Utalii;
Waandishi wa Habari;
Mabibi na Mabwana;
Ni furaha kubwa kwangu kujumuika nanyi leo katika uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania. Napenda kuchukua fursa hii kukupongeza Balozi Charles Sanga kwa kuteuliwa kwako na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania ambacho ni chombo muhimu sana katika maendeleo ya sekta ya utalii hapa nchini. Uteuzi huu ni uthibitisho wa imani kubwa aliyonayo Mh. Rais kwako. Aidha nawapongezeni pia Wakurugenzi wote mlioteuliwa kuongoza Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Hongereni sana!
Ndugu Mwenyekiti,
Kama mnavyofahamu utalii ni moja ya sekta ambazo ni mhimili mkuu wa uchumi ya nchi yetu hivi sasa. Serikali imekusudia kuendeleza sekta hii ili iongeze mchango wake kwenye pato la taifa na maendeleo ya nchi kwa ujumla.
Tangu kuundwa kwa Bodi ya Utalii takriban miaka 18 iliyopita, imeweza kuchangia kuleta mafanikio makubwa katika maendeleo ya sekta ya utalii nchini. Mifano michache ya mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la mapato yanayotokana na utalii kutoka dola za kimarekani milioni 146.84 mwaka 1993, hadi kufikia dola za kimarekani bilioni 1.3 mwaka 2010. Aidha idadi ya watalii imeongezeka kutoka 230,166 mwaka 1993 hadi kufikia watalii 867,994 mwaka 2011. Haya ni baadhi tu ya matunda ya kazi nzuri inayofanywa na Bodi ya Utalii Tanzania, sambamba na taasisi nyingine za umma na binafsi. Napenda kuchukua nafasi hii Kwa niaba ya serikali kuipongeza Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa kazi nzuri inayofanya ya kuitangaza Tanzania kama moja ya nchi zenye vivutio vikubwa na vya pekee barani Afrika na duniani kwa ujumla.
Ndugu Mwenyekiti,
Serikali itaendelea kutoa kipaumbe katika kuhudumia sekta hii, ikiwa ni pamoja na kujenga miundo mbinu, kuongeza bajeti ya utangazaji, kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji, kuboresha huduma kwa watalii kama vile malazi, chakula, usafiri na kadhalika. Nataka nisisitize kuwa ubora wa huduma kwa watalii sambamba na kuimarika kwa utangazaji wa utalii ndani na nje ya nchi ni masuala muhimu katika kuvutia watalii wengi zaidi kuja hapa nchini.
Kwa kuzingatia hilo, Serikali hivi sasa iko katika hatua za awali za kuiunda upya Bodi ya Utalii Tanzania ili kuifanya Mamlaka ya Utalii Tanzania ambapo pamoja na jukumu lake kuu la utangazaji utalii, itawajibika pia kudhibiti huduma na kusimamia shughuli zinazohusiana na utalii, ikiwa ni pamoja na kusajili kampuni za kitalii.
Hatua hii inalenga kukiboresha chombo hiki, kukiimarisha na kukipa nguvu zaidi katika utekelezaji wa majukumu yake.
Ndugu Mwenyekiti,
Ninafahamu kuwa hivi sasa Bodi ya Utalii Tanzania kwa kushirikiana na sekta binafsi ipo katika mchakato wa kutayarisha mkakati mpya wa utangazaji utalii wa taifa. Napenda kuwatia shime katika hili na ninaamini kabisa utekelezaji wa mkakati huu utasaidia sana katika kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchi yetu.
Serikali inatambua changamoto zinazoikabili Bodi ya Utalii na hasa ufinyu wa bajeti katika kutekeleza majukumu yake. Kwa sasa Bodi inategemea kwa asilimia mia moja ruzuku kutoka serikali kuu ambayo haitoshelezi mahitaji ya Bodi. Kwa kiasi kikubwa ufinyu huu wa bajeti unatokana na serikali kuelemewa na majukumu mengine katika sekta nyingine kama vile afya, elimu, usafiri, kilimo, na kadhalika. Ni matumaini yangu kuwa changamoto hii itapungua kwa kiasi kikubwa pale utaratibu wa tozo ya kitanda siku utakapoanza.
Ndugu Mwenyekiti na
Ndugu Wakurugenzi,
Mafanikio ya Bodi ya Utalii Tanzania na mengineyo mengi ambayo sikuyataja yametokana na ushirikiano mzuri baina ya Wakurugenzi wa Bodi zilizopita, Menejimenti ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na wafanyakazi wote kwa jumla. Kwa mantiki hiyo, ndugu Mwenyekiti na Bodi yako, ninyi ndio wadau wakuu na chachu ya mafanikio na maendeleo ya Bodi hii. Hivyo naomba nitumie fursa hii kuwakumbusha baadhi ya wajibu na majukumu mliyonayo kwa chombo hiki:
(i) Kuidhinisha mikakati na mipango ya muda mfupi na mrefu ya kutangaza utalii na kuona inatekelezwa ipasavyo;
(ii) Kuidhinisha bajeti za Bodi ya Utalii na kushauri Wizara/Serikali kuhusu mbinu za kuboresha bajeti ya utangazaji utalii;
(iii) Kuishauri serikali juu ya mipango ya kukuza utalii na kuona jinsi Bodi ya Utalii inavyoweza kutoa mchango wake;
(iv) Kuishauri serikali katika masula yanayohusu sera ya utalii, sheria na kanuni zinazohusu ukuzaji na utangazaji utalii;
(v) Kuiongoza Menejimenti katika kukuza maslahi bora ya wafanyakazi waBodi ili kuongeza ari ya kufanya kazi kwa ustadi na ufanisi; na
(vi) Kuwa mlinzi msimamizi (watchdog) katika masuala mbalimbali yanayohusu kukuza utalii na kwa hiyo kukuza pato kutokana na utalii.
Ndugu Mwenyekiti,
Pamoja na majukumu hayo niliyoyataja, ningependa kuwapa majukumu mahsusi katika miaka hii mitatu ya utumishi wenu,msimamie maeneo yafuatayo:
(i) Ningependa kuona kwamba wigo wa utalii unapanuka, zaidi ya utalii wa wanyamapori (wildlife tourism);
(ii) Katika mkakati mpya wa utangazaji utalii, Ni vema suala la 'branding nchi' yetu lisimamiwe na kukamilisha mwaka huu.
(iii) Kuwepo mbinu mpya na za kisasa za utangazaji utalii hii ikiwa ni pamoja na ukamilishaji na utekelezaji wa mkakati wa utangazaji na ukuzaji utalii wa miaka 5 ijayo (TOURISM MASTER PLAN 2012-16) ikihusisha matumizi ya njia za kielektroniki kutangaza (e-Marketing);Lengo liwe ni kufikia watalii million 1 mwishoni mwa 2013 na kuhakikisha utalii unaendelea kukua kwa asilimia 8-10 kwa mwaka na hivyo kufikia walau watalii milioni 1.2 ifikapo 2015.
(iv) Kuboresha mkakati wa uendelezaji na utangazaji utalii wa ndani (Domestic Tourism Marketing Strategy);
(v) Kuiongoza Bodi ya Utalii iwe na vyanzo binafsi vya fedha kupitia vitega uchumi mbalimbali;
(vi) Kuikuza Bodi kama kitaasisi ili kuwa na uwakilishi (mawakala) kwenye Nchi ambazo ni vyanzo muhimu vya watalii. Aidha, ni vema Bodi kusaidia kuanzishwa Bodi ndogondogo za Utalii za Kimikoa na kuwa na maofisa wawakilishi (liason officers) kwenye maeneo hayo ya mikoa. Na,
(vii) Kusimamia vizuri ‘migration’ ya Bodi ya Utalii kutoka ilivyo sasa kama Bodi ya Utangazaji Utalii kwenda kuwa Mamlaka kwa kushirikiana na Idara ya Utalii.
Ndugu Mwenyekiti,
Majukumu haya mnayokabidhiwa leo ni makubwa. Ni matarajio yangu binafsi na serikali kwamba kwa kutumia uzoefu na maarifa mliyonayo na kwa kushirikiana na Menejimenti ya Bodi ya Utalii, mtaweza kukiongoza vema chombo hiki, na mtakuwa kiungo madhubuti baina ya Wizara, Bodi ya utalii, sekta binafsi na sekta ya umma kwa ujumla.
Aidha, naelewa uzoefu, umahiri na weledi mlionao wewe Mwenyekiti na wakurugenzi wengine, ninawafahamu, sijabahatisha kuwateua, hivyo, mkidhamiria hamtaniangusha mimi wala taifa na sina shaka kabisa mtakuwa msaada mkubwa sana kwa Bodi ya Utalii Tanzania. Nyote kwa ujumla mtatumia ujuzi na uzoefu wenu katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili Bodi ya Utalii.
Ni matarajio yangu makubwa pia kuwa chini ya uongozi wako ndugu Mwenyekiti, Bodi itaendelea kuimarisha mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Bodi ya Utalii na wadau wengine katika sekta ya utalii nchini yataendelea kuimarishwa zaidi kwa manufaa ya sekta hii na Taifa kwa ujumla.
Napenda nikuhakikishie ndugu Mwenyekiti kwamba Wizara yangu itaendelea kutoa ushirikiano kwa Bodi yako ili iweze kutekeleza majukumu haya niliyoyataja hapo juu kikamilifu.
Ndugu Mwenyekiti,
Naomba sasa nitumie nafasi hii kabla sijahitimisha hotuba yangu kuishukuru Menejimenti na wafanyakazi wote wa Bodi ya Utalii Tanzania kwa ushirikiano walioipa Bodi ya Wakurugenzi iliyopita. Ushirikiano wao uliwezesha kufanikisha kwa kiasi kikubwa malengo ambayo walipewa katika kutekeleza majukumu ya kutangaza utalii. Ni matumaini yangu kwamba Menejimenti na wafanyakazi wote wataendelea kutoa ushirikiano huo kwako wewe Mwenyekiti na Wakurugenzi wa Bodi ili majukumu yaliyo mbele yenu yaendelee kutekelezwa ipasavyo.
Ndugu Mwenyekiti na Wakurugenzi wa Bodi, baada ya kusema hayo ninayo furaha kutamka rasmi kuwa, Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania sasa imezinduliwa rasmi.
Mhe Ezekiel Maige (MB)
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII
5 Aprili 2012

WAJUMBE WA TUME YA KATIBA

TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
(Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83,
Toleo la 2012, Vifungu 5, 6 na 7)
______________________________
UONGOZI WA JUU
1.
Mhe. Jaji Joseph Sinde WARIOBA
- Mwenyekiti
2.
Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino
RAMADHANI
- Makamu Mwenyekiti
WAJUMBE KUTOKA TANZANIA - BARA
1.
Prof. Mwesiga L. BAREGU

2.
Nd. Riziki Shahari MNGWALI

3.
Dr. Edmund Adrian Sengodo MVUNGI

4.
Nd. Richard Shadrack LYIMO

5.
Nd. John J. NKOLO

6.
Alhaj Said EL- MAAMRY

7.
Nd. Jesca Sydney MKUCHU

8.
Prof. Palamagamba J. KABUDI

9.
Nd. Humphrey POLEPOLE

10.
Nd. Yahya MSULWA

11.
Nd. Esther P. MKWIZU

12.
Nd. Maria Malingumu KASHONDA

13.
Mhe. Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb)

14.
Nd. Mwantumu Jasmine MALALE

15.
Nd. Joseph BUTIKU

WAJUMBE KUTOKA TANZANIA- ZANZIBAR
1.
Dkt. Salim Ahmed SALIM

2.
Nd. Fatma Said ALI

3.
Nd. Omar Sheha MUSSA

4.
Mhe. Raya Suleiman HAMAD

5.
Nd. Awadh Ali SAID

6.
Nd. Ussi Khamis HAJI

7.
Nd. Salma MAOULIDI

8.
Nd. Nassor Khamis MOHAMMED

9.
Nd. Simai Mohamed SAID

10.
Nd. Muhammed Yussuf MSHAMBA

11.
Nd. Kibibi Mwinyi HASSAN

12.
Nd. Suleiman Omar ALI

13.
Nd. Salama Kombo AHMED

14.
Nd. Abubakar Mohammed ALI

15.
Nd. Ally Abdullah Ally SALEH

UONGOZI WA SEKRETARIETI
1.
Nd. Assaa Ahmad RASHID
- Katibu
2.
Nd. Casmir Sumba KYUKI
- Naibu Katibu