Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Monday, February 27, 2012

Usiku Wa Hip Hop Kufanyika Tarehe 4 Machi 2012


 Meneja Mkuu wa Global Publishers na Mratibu Msaidizi wa tamasha hilo, Abdallah Mrisho akizungumza katika mkutano huo.
 Profesa J akitoa vionjo katika mkutano wa jana.
 Joh Makini naye akithibitisha kufanya makamuzi ambayo hayajawahi kutokea.
 Mapaparazi wakifanya kazi yao.

Wadau mbalimbali wa muziki wa Hip Hop hapa nchini, Jumapili ya Machi 4 mwaka huu wanatarajiwa kufurika ndani ya ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam kuhudhuria onesho kabambe la Hip Hop. Katika usiku huo wadau mbalimbali waliochangia muziki huu kufikia hapa ulipo watatunukiwa tuzo. Wakali wa muziki huo Profesa J na Joh Makini wamewawakilisha wasanii wenzao wa muziki huo katika mkutano wa kuthibitisha kushiriki tamasha hilo uliofanyika mchana huu ndani ya ofisi za Global Publishers zilizopo Mwenge jijini Dar.


PICHA : RICHARD BUKOS  / GPL  

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.