Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Monday, February 27, 2012

ORIJINO KOMEDI KWISHAAAA


Musa Mateja na Shakoor Jongo
KUNDI la wachekeshaji la Orijino Komedi linaloundwa na mastaa, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’, Lucas Mhuvile ‘Joti’, Joseph Shamba ‘Vengu’, Slivery Mujuni ‘Mpoki’, Alex Chalamila ‘MacRegan’ na Isaya Mwakilasa ‘Wakuvwanga’ chini ya Sekioni David ‘Seki’, linadaiwa kwisha huku kila mmoja akijiingiza katika fani nyingine ili kujipatia mkate wa siku.

UPEKUZI WA IJUMAA WIKIENDA WABAINI SIRI NZITO
Kwa muda mrefu sasa, Ijumaa Wikienda limekuwa likipokea malalamiko ya mashabiki wa mastaa kuwa michezo yao mipya haionekani kama zamani huku wakidaiwa kurudiarudia ya zamani.
Kwa mujibu wa vyanzo makini vilivyozungumza na gazeti hili, kundi hilo linaloruka hewani kupitia Runinga ya TBC 1, linadaiwa lilimaliza mkataba wake tangu Januari Mosi, mwaka huu na kusitisha uandaaji wa vipindi vipya.

INASIKITISHA
Ilidaiwa kuwa vijana hao watafutaji wamekuwa kwenye wakati mgumu kimaisha kwani walitarajia kulamba mkataba mpya hivyo baada ya kuona kimya, kila mmoja akaanza kusaka ‘ngawira’ katika fani nyingine.
 MASANJA
Ilielezwa kwamba Masanja amejikita kwenye muziki wa Injili akiwa kwenye ‘tizi’ la uchungaji, utangazaji na ushereheshaji.

MPOKI
Kama ilivyo kwa Masanja, pamoja na kwamba alianza muziki wa Kizazi Kipya akiwa bado anachekesha kideoni, Mpoki sasa amejikita katika Bongo Fleva na utangazaji huku akiuza nyago kwenye video za wasanii wa muziki Bongo.

VENGU
Kwa upande wake Vengu yuko kwenye matibabu nchini India baada ya kusumbuliwa na maumivu sehemu ya kichwa kwa muda mrefu.

JOTI
Joti kwa sasa anajihusisha

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.