Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Saturday, February 25, 2012

OSHA WAFUNGA KIWANDA


 Wafanyakazi wa Kiwanda hicho cha AM STEEL AND IRON MILL LIMITED wakizungumza na waandisha wa habari kiwandani hapo
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA ndugu Alex Ngata, akizungumza na wamiliki wa kiwanda hicho na kuwapa taarifa juu ya kusimamisha baadhi ya maeneo ya udhalishaji kwenye kiwanda hicho mpaka hapo watakaporekebisha sehemu ambazo zimefungiwa
Kaimu Mtendaji Mkuu ndugu Alex Ngata akiwa na mmoja wawamiliki wakiwanda hicho akikagua baadhi ya maeneo hayo ambayo yamefungiwa.


Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi (OSHA) imekifungikiwa kiwanda cha AM STEEL AND IRON MILL LIMITED kilichopo Mbagala Industrial Area, mpaka hapo watakaporekebisha baadhi ya maeneo ya uzalishaji katika kiwanda hicho, Kutokana na Kukiuka sheria Na 5 ya mwaka 2003 ya usalama na Afya Mahali Pa Kazi, kwa kutowapatia wafanyakazi wao vifaa vya kuwakinga ili wasiweze kuumia wakiwa katika maeneo hayo ya kazi, na mazingira yasioridhisha ya kiwanda hicho.
 
Afisa habari-OSHA

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.