Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Friday, August 19, 2022

Umuhimu wa Sensa

 Kupanga ni kuchagua ukizingatia idadi ya unaowapangia kutegemeana na malighafi uliyonayo

Maisha ya uyaya na changamoto zake

Maisha ya uyaya na changamoto zake
12 Mei, 2014
Binti wa Kazi
Saa 10 Alfajiri huku mhazini akinadi kuwaamsha walio waamini kuelekea kusali, naye jimbi akiwika akiwa na nia ya kuujulisha umma kuwa kumekucha. Pengine ishara zote mbili azana na kuwika kwa jogoo zikiwa ni kiashiria tosha cha kuukatisha usingizi wa binti wa kazi ambaye anayetakiwa kuyaanza kuyatekeleza majukumu yake ya kila siku.

Hapo awali kulikuwa na msemo kuwa mayaya huamka Kombora na kulala Lala salama wakilinganisha na vipindi vya redio hii wakati ule wa redio Tanzania Dar es Salaam. Basi msomaji leo hii katika makala haya maalumu ya siku ya wafanyakazi Duniani inayofanyika Mei Mosi ya kila mwaka tunayajibu maswali haya:Yaya anapatwa na matatizo gani akiwa kazini? Wana haki zipi na Je hali mayaya huko ughaibuni ikoje?

Miaka ya hivi karibuni tumeshudia huitaji mkubwa wa mayaya majumbani, mikahawani na ata katika maofisi ya kibalozi. Hilo linatokana na nchi kusonga mbele, kwani katika nchi zinazoendelea hivi sasa kati ya asilimi 4 mpaka 10 ya watu wa mataifa haya likiwamo taifa letu wanajishughulisha na kazi za majumbani.

Mwaka 2008 yaani miaka sita iliyopita shirika la kazi Duniani ILO lilibainisha kuwa watu Milioni 100 duniani kote , mkono huenda kinywani kwa kazi hizo. ILO inapambanua kuwa kuongezeka kwa majukumu ya majumbani, kukosekana kwa sera sahihi na zenye mizani kwa wafanyakazi wenye majukumu mengi ofisini mathalani ujauzito na likizo na kukuwa kwa maendeleo ni ithibati tosha ya kuongezeka kwa mahitaji ya mayaya majumbani.

Maoni ya viongozi wa CHODAWU

CHODAWU ni chama chenye dhamana ya wafanyakazi hawa nchini Tanzania na Bi Deoglasia Vuluwa ni miongoni mwa maafisa waandamizi wa chama hiki.

“Mfanyakazi wa kazi za ndani anapaswa kuheshimika kama mfanyakazi mwingine kwakulipwa mshahara stahiki mathalani mfanyakzi wa kawaida anatakiwa kulipwa elfu arobaini kwa mwezi kama anaishi nyumbani kwako na anaishi nyumbnai kwake mshahara wake unatakiwa kuwa zaidi.”Anasema Bi Vuluwa

Jamii za kiafrika wakati na ata baada ya ujima zimekuwa na mgawanyiko wa kazi, kuna majukumu ya wanawake na ya wanaume . Wanaume wakijishugulisha na kuzalisha mali huku akinamama wakitekeleza na mambo ya uzazi na nyumbani.

Mintarafu ya majukumu hayo ya kimaumbile, mahitaji kwa sasa yameongezeka sana hasa ya kuwatunza watoto na kazi nyingine majumbani. Wanawake wa leo wanafanya kazi ambazo zinaiongezea kipato kaya husika. Nako majumbani majukumu yakiongezeka mzigo huo wanatishwa wafanyakazi wa majumbani kwa hivyo soko la huhitaji wa mabinti lipo juu.

“Wafanyakazi wa majumbani wanapaswa kuheshimiwa mno na siyo kuwalisha makombo na kuwapa ujira mdogo, nimeshudunia kuna familia wanalipwa elfu ishirini yaani elfu kumi kumi mbili tu tunapaswa kuheshimu kazi hizi.”Anabainisha mdau mmoja Mkoani Dar es Salaam.

Kutokana na mtazamo kuwa majukumu ya nyumbani ni ya wanawake kumefanya jamii nyingi kuona kuwa ata haki ya umiliki wa mali zote za majumbani ni za wanaume hili linaoneka ata hii leo katika hatua mbalimbali za maamuzi ya mahakama mathalaini pale migogoro ya ndoa inapotokea. Mchango wa mwanmke kulea na kutunza nyumba hauna thamani. Mathalani katika kesi ya ndoa ya Omari Chikamba dhidi ya Fatuma Malunga shauri nambari 39 la mwaka 1989 la mahakama kuu palionekana mtazamo huu. Ninaweza kusema kuwa hilo ndilo linalosababisha ata uthamani wa kazi za majumbani kutopewa hadhi ya juu.

Bibi Chungu Wagala na Kiongozi wa CHODAWU Mkoa wa Dar es salaam anazitaja haki zaidi za mayaya kuwa ni kwenda likizo, kupewa kazi nyepesi akiwa mjamzito na kuheshimu sheria zote za kazi kama mfanyakazi mwingine.

Kazi hizi mara zote zinafanywa na vijana ambao ndiyo kwanza wnayaanza maisha na mara nyingi wanakuwa wamemaliza elimu yao ya msingi na wachache sana huwa wamepata elimu ya sekondari.

Mwaka 2006 , Benki ya Dunia ilisema kuwa katika nchi nyingi zinazoendelea kusini mwa jangwa la Sahara idadi ya watu inaongezeka kwa kasi. Inabainishwa zaidi kuwa idadi ya vijana ifikapo mwaka 2050 vijana kati ya umri wa miaka 15-24 itakuwa kubwa mno barani Afrika na Asia. Ingawa idadi hiyo ikiongezeka hakuna hima inayofanyika kuongeza ajira ya vijana hawa ambapo kwa nchi ya Kenya vijana kati ya miaka 15-30 ambao ni asilimia 32 ya wakenya wote inakadiliwa asilimia 25 tu ndio wanaopata ajira ambazo nyingi ni za kawaida kama za wakaka na wadada wa kazi.

Hapa nyumbani Tanzania vijana wa kati ya miaka 15—34 ni asimiia 56 ya Watanzania wote ambapo theluthi ya hao wapo vijiweni wakizamia katika kazi za majumbani kama vijana wenzao wa Kenya.

Kisa cha dada Mfilipino

Hali imekuwa na ahuweni kwa wasichana kuliko wavulana kutokana na mtu anayeweza kufanya kazi za nyumbani ni mwanamke tu kuliko mwanaume kwani wasichana wengu hupata kazi hizi. Hali hii inasababisha baadhi ya vijana hao kukimbilia ng’ambo ili wakiamini kuwa huko kazi zina nafuu. Lakini hali ya huko si salama kweli Kama anavyothibitisha dada huyo mfilipino aliyekimbilia Katari.

“Kufanya kazi majumbani nchini Katari ni pagumu sana, nimekuja mwaka 2008 miaka kadhaa iliyopita wakati nafanya kazi na mwajiri wangu wa awali, hakunipa chakula, mishahara ilicheleweshwa na hakukuwa na muda wa kupumzika. Kwa siku nilifanya kazi saa 14 kazi nikianza saa 12 asubuhi.

Ukilala, kama wao wameamka wakitaka uwatayarishie chochote huna budi kuamka na kutekeleza hilo, huku majukumu mengine ya kupika na kupokea simu zao kila mara wanapohitaji kuuliza jambo hapo nyumbani, sasa kwanini yaya afanye kazi bila ya kula na hakuna muda wa kupumzika na kulala. Ata mikataba haitiliwi maanani. Katika mkataba wangu natakiwa kulipwa dola 400 lakini nalipwa dola 200 tu . Mbaya zaidi ata kibali changu cha kusafiria kilichukuliwa na mwajiri wangu.

Niliruka jivu na kukanyaka moto, mwajili wangu wa pili alikuwa hatari zaidi, yeye alitaka kunibaka ndani ya chumba changu. Alinipa pesa ambayo niliikataa na kukataa kufanya nae ngono. Kwani kufanya hivyo halikuwa jukumu lililonipeleka . Nilifika hapa kufanya kazi kwa manufaa ya familia yangu na siyo michezo hiyo Kukataa kwangu kulisababisha kuondoka kwake niliacha kila kitu changu isipokuwa nguo zangu na pesa ya nauli ya Taxi tu iliyoweza kunipeleka kwa mwajiri mwingine.

Sasa kila nimuonapo mwanaume wa hapa katari naogofya mno, nadhani watanikamata, kunifunga na kunirejesha kwetu Ufilipino

Sasa nikirudi huko, Je familia yangu watakula nini? Kwa hiyo haina budi nijifiche tu na kufanya vibarua vya muda ili nipate pesa ya kupeleka kwetu. Kwa kweli hapa Katari ukiondoka kwa bosi wako ni tatizo kubwa kwani utakosa uhalali wa kufanya kazi na vibali vyako vyote vitapotea. Unaweza kupata kazi ya muda lakini wakigundulika wamekupa kazi wanalipishwa faini na mie nitarudishwa kwetu.

Hivi sasa nimepanga nina chumba kidogo na najinunulia chakula .Pia nina Kigali kidogo ila kikikaguliwa na polisi ni tatizo kubwa. Bado nahitaji kuishi huku . Nahitaji kufanya kazi ili nipate kibali cha kuishin huku kutoka uhamiaji.

Ninadhani kibali changu kipo Basmutaba eneo ambalo nilikaguliwa vidole vyangu hapo awali. Ninajaribu kutafuta msaada kutoka idara ya CID lakini hawajanipatia kibali changu hadi leo

Kibali hili kilitoka 2011 ili nikipate natakiwa kulipa rila 6500 na rila 6000 kupata mwajiri mwengine halali. Natakiwa kulipia tiketi ya kwenda na kurudi nyumbani na kulipa faini ya rila 10 kila siku tangu mwaka 2008 mpaka leo hii. Kwa hiyo natakiwa kulipa rila 19500 wakati nafanya kazi ya muda mfupi tu huo mshahara wenyewe, vipi familia yangu Ufilipino sijui watafanya nini

Kulingana na ripoti Human Right watch ya Aprili 23 mwaka inabainisha kuwa hali ni mbaya katika taifa hili linalojiandaa na kufanyika kwa Kombe la dunia la mwaka 2022. Nchini nyengine zenye hali hii ni Saudi Arabia na Imarachi ambapo mfanyakzi wa ndani kwa juma zima anafanya kazi zaidi ya saa 100 ambapo ni sawa kwa siku anafanya kazi saa 17 ambapo kihalali mfanyakazi anatakiwa kufanya kazi saa 8 kwa siku ama kama kutakuwa na ziada ya kazi basi kutakuwepo na malipo ya ziada kwa muda unaongezeka.

Tume ya usuluhishi na mahakama ya kazi

Panapokuwepo na unyanyasaji wowote nchini petu sheria ya kazi ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007 zinatoa nafasi ya muhusika kupeleke suala hilo Kwenye Tume ya Usuluhishi na uamuzi yaani CMA ata mayaya wana nafasi hiyo kisheria lakini ni ukweli ulio wazi kuwa mayaya wengi wamekuwa hawana mikataba ya kazi ambayo inaweza kuwasaidia pale hali inapokuwa tofauti. Kwani mkataba ndiyo uthibitisho pekee wa mtu kufanya kazi sehemu fulani na ndipo sehemu pekee panapoweza kubainisha haki na wajibu wa kila mmoja . Chakusikitisha kwa muda mrefu uajiri wa wafanyakazi za ndani inatumia mitindo ya kijamaa na kidugu huku wengine wakiwaita binti na kaka wa wa kakazi kaka,/dada , wakimaanisha kuwa ni sehemu ya familia zao lakini vitendo vimekuwa kinyume. Ukweli uliowazi kuwa yaya au kaka wa kazi si ndugu ni mwajiriwa sehemu husika hivyo ni wajibu wa kila mmoja kutenda haki stahiki.

Mashauri ya mayaya mahakamani

Kwa hakika hali ya unyanyasaji wa mayaya imekuwa ni tatizo kubwa dunia ebu soma kisa hiki cha binti Mtanzania. “Mahakama ya kazi nchini Uingereza ilitoa hukumu ya ushindi kwa binti yaya Mtanzania Bi Elizabeth Kawongo kwa kulipwa Paundi 58,583 sawa na milio 130 kwa wakati huu kutokana na kutolipwa mishaharayake , kutopewa nafasi ya kupumzika na kufanywa mtumwa.

Watuhumiwa walikabiliwa na tuhuma nyingine za kibaguzi kwa mfanyakzi huyo. Mahakama hiyo ya Watford ilitoa uamuzi wake dhidi ya Ramadhani Dhanji na mkewe Kudra Dhanji waliokuwa ni wazazi wa Zainab Alibhai Muingereza aishie nchini Tanzania. Bi Zainabu Alibhai alimchukuwa binti Elizabeth Kiwango na kumpeleka Uingereza kufanya kazi ya uyaya.
Binti wa Kazi
Wakati wa kusikiliza ushahidi wa pande zote ilibainika kuwa kulikuwa na makos kadhaa yaliyofanyika na walalamikiwa dhidi ya yaya Elizabeti, ilibainika kuwa mara baada ya kutendewa ubaya huo aliyekuwa Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Uingereza wakati huo Bi Radhia Msuya na chama cha Wanawake walimsaidia Elizabeth kupatia ushauri wa kisheria na kufungua kesi. Kulingana na mlolongo wa shitaka hilo Elizabeth alipelekwa London Julai 2006 na mmoja wa waaajiri wake ili kumsaida wakati alipoenda kufanyiwa matibabu ya mguu lakini alipofika huko London Mama Alibhai alimshurutisha Elizabeth kufaya kazi kwa wazazi wake kama yaya. Baadaye alipokonywa kibali chake cha kusafiri. Ilibainika kuwa Elizabeti alifanya kazi hadi saa 15 kwa kwa siku moja kila siku ya juma bila mapumziko. Chakushangaza mama Alibhai alibaki Uingereza kwa majuma mawili tu bila ya kupata matibabu yoyote ya kiungo chochote cha mwili wake ila alikwenda kuhudhuria harusi ya binti yake.

Mahakama ilijulishwa kuwa baadaye Elizabeth aliambiwa kuwa hatorudi naye Tanzania atabaki uingereza akiwa yaya kwa Mama wa Alibhai. Elizabeth alitumikishwa sana na alipomwomba mama Alibhai waweze kurudi wote Tanzania, Ombi hilo lilipokelewa na sikio lisilo sikivu. Badala yake ya kufanya kazi kwa wazazi wa Bi Alibhai, Binti Elizabeth alipelekwa nyumbani kwa ndugu mwingine wa familia hiyo akifanya kazi za ndani kama vile kufua kupika na kufanya usafi.

Mtu kwake na mkataa kwao mtumwa, alipofika huko kila alipouliz na kuomba kurudi nyumbani Tanzania aliambiwa kuwa kuwepo Ulaya kwake ni ngekewa, ingawaje binti huyo alilazwa jikoni tena sakafuni na wakati wa baridi kali. Akila makombo na vyakula vilivyopita muda wake.

Mungu bahati, siku moja aliomba ruhusa ya kwenda kusali , alilopata ruhusa hiyo alipofika kanisani aliwaeleza jamaa wengine kwa yaliyomsibu ndipo walipoweza kufanikisha kuonana na ubalozi wa Tanzania na chama cha utetezi wa wanawake na kufanikisha kupata kibali chake cha kusafiri na kurudi nyumbani Tanzania lakini ndugu Dhanji aliomba suala hilo limalizika kimya kimya kwa kumpa Elizabeth paundi 380 ambapo Eliza alizikatata hadi suala lake lilipomalizwa na mahakama.”

Wakati wafanyakazi wote wakisherekea siku hii ni wajibu wa kila mmoja wetu kuthamini mchango wa mabinti na kaka wa kazi majumbani kwetu . Basi kwa Kisa hicho ndiyo naufunga ukurasa wa makala haya ya siku ya wafanyakazi duniani. Kumbuka Leo hii tulitupia jicho suala la wafanyakazi wa majumbani 

~Ngugi wa Thiong'o wrote:



Raila had refused to eat.He was on hunger strike. .He grew thin and pale.His right palm had gone dark,the arm had pimples and boils as well. He was receiving extraordinary punishment. He stood for his words. Dictators had to go. Moi had to go. 


I had been initially jailed for a year by the Kenyatta's regime. For criticising the government acts on my book,, "l will marry when I want". I had set up a revolutionary theatre ,this provoked the dictatorial regime. I was jailed for a year. 


Odingas's was involving. Seven years already in jail. He kept his words. Kenya needed a fresh air. He was willing to pay the price. I felt touched by his story. When I came to see him, he was denied a chance to talk to me. However he wisely did it in a writing. "Tell lda to ask the doctor to prescribe me these drugs, am slowly dying ".


Soon his mother died.His other relatives including his aunt followed. He would never be allowed to attend any of the burrials. It was painful. It was Real torture. 


He remained in detention without trial. The government would not allow  it. Soon he was transfred to Kamiti maximum prison. He was taken the torture corner. The isolation block. The detention camp. A prison within a prison. Here he was daily served with half cooked ugali with vegetable water with a few limp leaves floating around. And for the first time in two weeks, he was served with food. 


The blows to his head dazed him.He fell on the floor and lay there. Rono,a GSU officer, and others jumped from his head to his genitals.His left leg twisted and was confirmed broken. He was either going to speak the truth or become a dead meat. He waited for the end, but it did not come. But still Odinga refused to give in. ...


Raila Odinga  genuinely fought for our second liberation,

(Copy and paste)

Nionyeshe rafiki nitakueleza tabia zako


Saturday, June 7, 2014

MASHABIKI MILIONI 3.5 KUTAZAMA MECHI 64 ZA KOMBE LA DUNIA BRAZIL

 

Na James Truman, brotherdanny5.blogspot

Sao Paulo, Brazil

JUMLA ya mashabiki 3,531,211 wanatarajiwa kuingia viwanjani kutazama mechi 64 za fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazil kuanzia Juni 12, mwaka huu.
Mashabiki hao watatinga kwa nyakati tofauti katika viwanja 12 vitakavyotumika katika fainali hizo za 20, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kulinganisha na fainali za mwaka 2010 zilizofanyika nchini Afrika Kusini.
Hata hivyo, Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) limetenga jumla ya tiketi 3,334,524 kwa ajili ya fainali hizo, lakini ikiwa mashabiki wataingia kwa idadi halisi ya viwanja hivyo, jumla yake watakuwa 3,531,211.
Sehemu kubwa ya tiketi zilizotengwa na FIFA zitagawiwa kwa makundi kama ya wafanyabiashara washirika, wanahabari na wageni maalum. Tiketi zitakazouzwa zinakadiriwa kuwa 1.1 milioni ambapo 400,000 kati yake ni kwa ajili ya Wabrazili na 700,000 kwa mashabiki kutoka nje. Kwa kila mechi, asilimia 8 ya mauzo ya tiketi itakwenda kwa timu zinazoshiriki.
Hadi kufikia Agosti 20, 2013 jumla ya tiketi 2.3 milioni zilikuwa zimeuzwa ndani ya saa 24 tu na hadi kufikia Oktoba 2013 kulikuwa na maombi ya tiketi milioni 6. Bei ya tiketi hizo inaanzia Dola 12.50 kwa mechi za awali wakati mechi ya fainali tiketi zitauzwa kwa Dola 990.
Estadio do Maracana

Taarifa zinaonyesha kwamba, uwanja wa Maracana ulioko jijini Rio de Janeiro umekarabatiwa upya kwa ajili ya fainali za mwaka huu zinazofanyika miaka 64 tangu zilipofanyika nchini humo mwaka 1950. Uwanja huo unaotumiwa na klabu kongwe nchini humo za Fluminense na Flamengo na ulifunguliwa Juni 2013 kwa mechi baina ya Brazil na England.
Estadio do Maracana ulitumiwa kwenye mechi ya fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1950, ambapo mashabiki 174,000 waliingia na kuishuhudia Uruguay ikiichapa Brazil 2-1.
Uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza watazamaji 73,531 ndio utakaotumika kwa mechi ya fainali Julai 13, 2014, lakini pia utahusisha mechi nyingine sita na hivyo kufanya jumla ya watazamaji watakaoingia uwanjani hapo kuwa 514,717.
Mechi nyingine zitakazochezewa hapo ni mechi za Kundi F baina ya Argentina na Bosnia&Herzegovina (Juni 15, 2014); Hispania na Chile (Juni 18, 2014); Ubelgiji na Russia (Juni 22, 2014); Ecuador na Ufaransa (Juni 25, 2014); Mshindi Kundi C na Mshindi wa Pili Kundi D (Juni 28, 2014); na Robo Fainali (Julai 4, 2014).
Arena de Sao Paulo (Corinthians)

Uwanja huu uko jijini hapa Sao Paulo, ambako ndiko soka ilikozaliwa kwa nchi ya Brazil. Unatumiwa na klabu kongwe ya Corinthians na una uwezo wa kuingiza watazamaji 65,000. Sao Paulo ni mji ulioko Kusini Mashariki ma Brazil na unafahamika kama Terra da Garoa kutokana na mvua kunyesha mara kwa mara.
Katika uwanja huu jumla ya mechi sita zitachezwa na kuingiza watazamaji 390,000 katika fainali hizo.
Mechi zitakazochezewa hapo ni ile ya ufunguzi baina ya wenyeji Brazil na Croatia (Juni 12, 2014); Uruguay na England (Juni 19, 2014); Uholanzi na Chile (Juni 23, 2014); Korea Kusini na Ubelgiji (Juni 26, 2014); Mshindi Kundi F na Mshindi wa Pili Kundi E (Julai 1, 2014); na Nusu Fainali (Julai 9, 2014).
Estadio Nacional Mane Garrincha

Uwanja huu wenye uwezo wa kuingiza jumla ya watazamaji 68,009 kwa wakati mmoja, uko jijini Brasilia, mji mkuu wa Brazil tangu mwaka 1960 uliochukua nafasi ya Rio de Janeiro.
Jina la uwanja huo limetokana na nyota wa zamani wa klabu ya Botafogo na Brazil, Manuel ‘Mane’ Garrincha, ambaye alikuwa mmoja wa wanasoka mahiri nchini humo katika miaka ya 1950 na 1960.
Ndani ya uwanja huo mpya kutachezwa mechi 7 na jumla ya mashabiki 476,063 anatarajiwa kuhudhuria mechi hizo.
Mechi zitakazochezwa hapo ni baina ya Uswisi na Ecuador (Juni 15, 2014); Colombia na Brazil (Juni 19, 2014); Cameroon na Brazil (Juni 23, 2014); Ureno na Ghana (Juni 26, 2014); Mshindi Kundi E na Mshindi wa Pili Kundi F (Juni 30, 2014); Robo Fainali (Julai 5, 2014); na Mechi ya kutafuta mshindi wa tatu (Julai 12, 2014).
Estadio Castelao

Uwanja huu uko jijini Fortaleza, Kaskazini Mashariki mwa Brazil, na una uwezo wa kuingiza watazamaji 58,704. Klabu zinazoutumia uwanja huu ni Ceara SC na Ferroviario AC na ndio utakaotumika kwa mechi ya pili ya Brazil ya hatua ya makundi.
Fortaleza ni maarufu kwa utalii, fukwe nzuri na vyakula vya aina yake na unatajwa kuwa na hali ya Kitropiki.
Jumla ya mechi sita zitachezwa hapa na mashabiki 352,224 wanatarajiwa kuingia uwanjani. Mechi hizo ni Uruguay na Costa Rica (Juni 14, 2014); Brazil na Mexico (Juni 17, 2014); Ujerumani na Ghana (Juni 23, 2014); Ugiriki na Ivory Coast (Juni 24, 2014); Mshindi Kundi B na Mshindi wa Pili Kundi A (Juni 29, 2014); na Robo Fainali (Julai 4, 2014).
Estadio Mineirao

Huu ni uwanja unaotumiwa na klabu ya Cruzeiro. Uko katika Jiji la Belo Horizonte, umbali wa saa moja tu kutoka Jiji la Rio de Janeiro na ni mji usio na gharama kubwa sana kwa mashabiki wa kigeni.
Hapa ndipo mwanasoka mahiri duniani, Ronaldo de Lima, alipoanza kung’ara akiwa na klabu ya Cruzeiro.
Uwanja huu una uwezo wa kuingiza watazamaji 57,483 ambao utachezewa pia mechi ya nusu fainali.
Jumla ya mashabiki 344,898 wanatarajiwa kuingia kwenye uwanja huu katika mechi sita zitakazochezwa hapa.
Mechi zitakazochezwa ni baina ya Colombia na Ugiriki (Juni 14, 2014); Ubelgiji na Algeria (Juni 17, 2014); Argentina na Iran (Juni 21, 2014); Costa Rica na England (Juni 24, 2014); Mshindi Kundi A na Mshindi wa Pili Kundi B (Juni 28, 2014); na Nusu Fainali (Julai 8, 2014).
Estadio Beira-Rio

Uwanja huu uko jijini Porto Alegre na una uwezo wa kuingiza watazamaji 48,849 ambapo pia unatumiwa na klabu mbili za Internacional na Gremio. Upo kando ya Mto Guaiba.
Porto Alegre ni mji wenye mvua kipindi cha Juni na Julai na visiwa kadhaa, kimojawapo ni Lago de Patos kilichozungukwa na miti karibu milioni moja.
Hapa patachezewa mechi tano na hivyo watazamaji 244,245 wanatarajiwa kuingia uwanjani.
Mechi zitakazochezewa hapo ni Ufaransa na Honduras (Juni 15, 2014); Australia na Uholanzi (Juni 18, 2014); Korea Kusini na Algeria (Juni 22, 2014); Nigeria na Argentina (Juni 25, 2014); na Mshindi Kundi G na Mshindi wa Pili Kundi H (Juni 30, 2014).
Arena Pernambuco

Huu ni uwanja ulioko jijini Recife na unatumiwa na klabu maarufu za Nautico, Santa Cruz na Port ukiwa na uwezo wa kuingiza watazamaji 44,248.
Recife ni mji ulioko kwenye Pwani ya Kaskazini Mashariki ya Brazil, ulitumika mara ya mwisho katika mechi ya Kombe la Dunia 1950.
Huu ni mji maarufu kwa uchumi wa Brazil, lakini wakazi wake ni mashabiki wa soka waliopitiliza.
Jumla ya mechi tano zitachezwa hapa na mashabiki 221,240 wanatarajiwa kushiriki. Mechi hizo ni kati ya Ivory Coast na Japan (Juni 14, 2014); Italia na Costa Rica (Juni 20, 2014); Croatia na Mexico (Juni 23, 2014); Marekani na Ujerumani (Juni 26, 2014); na Mshindi Kundi D na Mshindi wa Pili Kundi C (Juni 29, 2014).
Arena Fonte Nova

Huu uwanja uko kwenye Jiji la Salvador ukiwa na uwezo wa kuingiza watazamaji 52,048 na unatumiwa na klabu za Bahia na Vitoria. Uwanja huo utashuhudia mechi sita kwenye fainali hizo. Waandaaji wanasema uwanja huo mpya umejengwa kisasa na una migahawa, makumbusho ya soka, maduka, hoteli na kumbi za sherehe.
Mji wa Salvador ni uko Kaskazini mwa Brazil na ndio uliokuwa mji mkuu wa kwanza wa nchi hiyo.
Mechi zitakazochezwa hapo ni kati ya Hispania na Uholanzi (Juni 13, 2014); Ujerumani na Ureno (Juni 16, 2014); Uswisi na Ufaransa (Juni 20, 2014); Bosnia&Herzegovina na Iran (Juni 25, 2014); Mshindi Kundi H na Mshindi wa Pili Kundi G (Julai 1, 2014); na Robo Fainali (Julai 5, 2014).
Jumla ya watazamji 312,288 wanatarajiwa kushuhudia mechi hizo uwanjani hapo.
Arena Pantanal

Uwanja huo upo kwenye mji wa Cuiaba, Magharibi mwa Brazil, Kusini mwa Misitu ya Amazon. Unafahamika kama ‘Green City’ na ni maarufu kwa utalii licha ya kwamba kwa kipindi cha Juni hadi Julai hali ya hewa inakuwa tatizo kutokana na joto kufikia nyuzi 40.
Uwanja huo uliboreshwa kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia na utatumika kwa ajili ya mechi nne. Una uwezo wa kuingiza watazamaji 42,968. Ni nyumbani kwa klabu za Cuiaba na Mixto.
Hapa jumla ya mashabiki 171,872 wanatarajiwa kushuhudia mechi hizo nne za Chile na Australia (Juni 13, 2014); Russia na Korea Kusini (Juni 17, 2014); Nigeria na Bosnia&Herzegovina (Juni 21, 2014); na Japan na Colombia (Juni 24, 2014).
Arena Amazonia

Uwanja huu uko mjini Manaus, mji ambao upo katikati ya misitu ya Amazon. Una uwezo wa kuingiza watazamaji 42,374.
Mji huo unaelezwa kwamba siyo mahali pazuri sana kwa soka kutokana na kuwa katikati ya misitu, hata hivyo waandaaji wameamua fainali za Kombe la Dunia zichezwe kila kona ya nchi baada ya kuzikosa kwa miaka 64.
Huenda baada ya michuano ya Kombe la Dunia uwanja huo utageuka kuwa mahali pa wanyama.
Inatazamiwa kwa mashabiki 169,496 watahudhuria mechi nne zitakazochezwa hapo.
Mechi hizo ni baina ya England na Italia (Juni 14, 2014); Cameroon na Croatia (Juni 18, 2014); Marekani na Ureno (Juni 22, 2014); na Honduras na Uswisi (Juni 25, 2014).
Estadio das Dunas

Huu ni uwanja ulioko jijini Natal ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 42,086. Unatumiwa na klabu ya America na umemalizika kujengwa kwa ajili ya Kombe la Dunia.
Estadio das Dunas utatumika kwa mechi nne za makundi katika fainali hizo. Natal ni mji unaofahamika kama Cidade do Sol (Sun City) kwa sababu umekuwa na joto linalokaribia nyuzi 28. Fukwe zilizopo Kaskazini Mashariki mwa jiji hilo zinalifanya jiji hilo lizidi kupendeza.
Jumla ya mashabiki 168,344 wanatarajiwa kuingia kutazama mechi baina ya Mexico na Cameroon (Juni 13, 2014); Ghana na Marekani (Juni 16, 2014); Japan na Ugiriki (Juni 19, 2014); na Italia na Uruguay (Juni 24, 2014).
Arena da Baixada

Uwanja huu uko jijini Curitiba ambao kwa mara ya kwanza ulijengwa mwaka 1914 lakini ukafanyia ukarabati maka 1999 na umerekebishwa zaidi baada ya Brazil kupata fursa ya kuandaa fainali za Kombe la Dunia.
Unatumiwa na klabu ya Atletico Paranaense na una uwezo wa kuingiza watzamaji 41,456.
Jumla ya mechi nne zitachezwa hapa na mashabiki 165,824 wanatarajiwa kutinga.
Mechi hizo ni Iran na Nigeria (Juni 16, 2014); Honduras na Ecuador (Juni 20, 2014); Australia na Hispania (Juni 23, 2014); na Algeria na Russia (Juni 26, 2014).
Curitiba ni mji wa aina yake ndani ya Brazil na unatajwa kuwa na uchumi mkubwa. Hali yake ya hewa inafanana na Rio de Janeiro na Belo Horizonte.

MWENZI WA MAISHA YAKO! TAFUTA KITABU HIKI KIKUONGOZE KUMPATA ANAYEKUFAA, KINAZINDULIWA KESHO MWANZA


Unataka kumjua yupi anayekufaa kwa maisha? Unatangatanga kila siku ukichagua mwenza? Pengine unakosea kwa kutokujua sifa muhimu badala yake unaangalia umbile na sura. Usipate tabu, wacha kutazama muonekano wa nje. Muombe Mungu akuongoze. Kitabu cha MWENZI WA MAISHA ambacho kinazinduliwa kesho jijini Mwanza kina majibu yote na ni msaada mkubwa kwako wewe na mwingine.
Kama unahitaji nakala yako gonga namba hizi: 0767 681078/0784 707551

Wednesday, June 4, 2014

MASKINI TEMBO WETU, WAMEKOSA NINI JAMANI?


Ndugu zangu,
Ujangili umeendelea kushika kasi nchini Tanzania, hasa wa tembo, licha ya jitihada
kadhaa zinazofanywa na mamlaka husika.
Tembo kama huyu pichani anauawa kinyama na wendawazimu wachache ambao wanaangalia maslahi yao ya kuuza meno yake bila kujali hatma ya baadaye ya rasilimali zetu.
Zimekuwepo operesheni nyingi nchini, miongoni mwazo ni ile ya Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa mwaka 2013, ambayo ilisitishwa baada ya kudaiwa kwamba wasimamizi wake waliendesha vitendo vya utesaji kwa wale walioshukiwa kujihusisha na ujangili.
Lakini pamoja na kusitishwa huko, bado kikwazo kikubwa kinaonekana kipo serikalini, kwani tunaelezwa kwamba wapo maofisa wakubwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, na wanatengeneza mamilioni ya fedha.
Ndugu zangu, lazima tuwe wazalendo, tuungane kwa pamoja kupinga unyama na ujambazi huu ambao kama hatukisimama imara unaweza kuwapukutisha hayawani wote nchini na tukabaki na picha za wanyama kwenye vitabu vyetu vya historia. Tembo ndiye mnyama mkubwa kabisa aliyesalia duniani katika jamii zile za dinosaur, hivyo ni urithi mwingine kwa vizazi vyetu.

Ndugu yenu,

Daniel Mbega,

Iringa - Tanzania
Ndugu zangu,
Ujangili umeendelea kushika kasi nchini Tanzania, hasa wa tembo, licha ya jitihada kadhaa zinazofanywa na mamlaka husika.
Tembo kama huyu pichani anauawa kinyama na wendawazimu wachache ambao wanaangalia maslahi yao ya kuuza meno yake bila kujali hatma ya baadaye ya rasilimali zetu.
Zimekuwepo operesheni nyingi nchini, miongoni mwazo ni ile ya Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa mwaka 2013, ambayo ilisitishwa baada ya kudaiwa kwamba wasimamizi wake waliendesha vitendo vya utesaji kwa wale walioshukiwa kujihusisha na ujangili.
Lakini pamoja na kusitishwa huko, bado kikwazo kikubwa kinaonekana kipo serikalini, kwani tunaelezwa kwamba wapo maofisa wakubwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, na wanatengeneza mamilioni ya fedha.
Ndugu zangu, lazima tuwe wazalendo, tuungane kwa pamoja kupinga unyama na ujambazi huu ambao kama hatukisimama imara unaweza kuwapukutisha hayawani wote nchini na tukabaki na picha za wanyama kwenye vitabu vyetu vya historia. Tembo ndiye mnyama mkubwa kabisa aliyesalia duniani katika jamii zile za dinosaur, hivyo ni urithi mwingine kwa vizazi vyetu.
Ndugu yenu,
Daniel Mbega,
Iringa - Tanzania
source: MASKINI TEMBO WETU & www.mjengwablog.com