Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Sunday, February 26, 2012

Mugabe atimiza miaka 88

 Sherehe za kuadhimisha Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe kutimiza umri wa miaka 88, zimefanywa katika mji wa Mutare, mashariki mwa nchi, na maelfu ya watu wamehudhuria.
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe

Matawi ya chama cha ZANU PF cha Rais Mugabe, yalichanga kugharimia sherehe hizo ambazo piya zilikuwa na mashindano ya warembo na mechi ya mpira.
Aliwaambia wafuasi wake kwamba wale wanaopinga msimamo wake dhidi ya wapenzi wa jinsia moja na ndoa kati yao, wapotelee mbali.
Bwana Mugabe alikanusha kuwa ni mgonjwa, na mapema juma hili alisema yeye kakazana kama kigongo na anaweza kuongoza nchi..
Umri wake pamoja na taarifa kuwa Rais Mugabe anauguwa saratani ya kibofu, imezusha wito mwengine kuwa Zanu PF inafaa kubadilisha uongozi.
Lakini chama chake kimemuunga mkono agombee tena urais mwaka huu.

BBC

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.