Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Saturday, February 25, 2012

BILAL ATEMEBELEA BANDARI YA KISANGA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika moja ya jengo kati ya mawili ya Maghala ya kuhifadhia Bidhaa yaliyopo katika Bandari ya Kasanga, kijiji cha Lusambo Wilaya ya Sumbawanga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Luteni Godfrey Semiono (Mkuu wa Kambi) kukagua kikosi cha Ulinzi wa Mipaka cha Kasanga kilichopo katika kijiji cha Lusambo, pembezoni mwa Wilaya ya Sumbawanga, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuzindua maghala ya kuhifadhia bidhaa katika Bandari ya Kasanga jana Februari 23, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki katika Soko la Samaki la Kasanga, baada ya kuweka jiwe la msingi katika soko hilo akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa, jana Februari 23,  2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kuwaaga wananchi wa Kijiji cha Lusambo waliojitokeza katika mapokezi yake alipofika kuweka jiwe la msingi katika Soko la Kasanga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012
 Picha na Muhidin Sufiani-OMR

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.