Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Wednesday, January 18, 2012

RAIS KIKWETE AZINDUA MADARAJA MOROGORO KUSINI


Rais Jakaya Kikwete na ujumbe wake na wenyeji wakipita juu ya daraja jipya la Mtombozi, Matombo, Morogoro kusini alilolizindua jana.
Rais Jakaya Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Joel Bendera wakimaliza kuvuka daraja jipya la Magogoni katika barabara ya Kiganila-Mvuha, Morogoro Kusini mara baada ya Rais Kikwete kulizindua jana.
Rais Jakaya Kikwete akiongea baada ya kuzindua daraja la mto Mtombozi tarafa ya Matombo wilaya ya Morogoro kusini jana.
Rais Jakaya Kikwete mwenye mwamvuli mkononi akielekea jukwaani kuhutubia wananchi huku mvua ikinyesha baada ya kuweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa soko la kijiji cha Mtamba, Morogoro na baadae kuzindua madaraja mawili makubwa katika mto Mtombozi, Matombo, na mto Magogoni katika barabara ya Kiganila-Mvuha na kukagua ujenzi wa barabara sehemu ya Kisaki, Msalabani.

 Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akihutubia huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha.
Wananchi wenye mapenzi na Rais wao walikubali kunyeshewa na mvua ili mradi kumsikiliza nini rais kawafanyia na nini anawahakikishia wananchi wake.

Chanzo: magangaone

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.