Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Tuesday, January 24, 2012

Mjamzito Anaswa kwa Ukahaba







Na Richard Bukos
MREMBO Sikujua Hassan, mwenye ujauzito unaokadiriwa kuwa na umri wa miezi sita, alinaswa akifanya ukahaba, Buguruni, Dar es Salaam.
Sikujua, alinaswa na polisi kisha kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Sokoine Drive, Dar es Salaam ambapo alikiri kosa la kujihusisha na ukahaba.
Baada ya kukiri kosa, Hakimu Mkazi, William Mutaki, alimhukumu kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi 20,000.
Hata hivyo, Sikujua hakuweza kulipa faini, kwa hiyo aliamriwa kwenda gerezani pamoja na ujauzito wake.
Sikujua amepangiwa kutumikia adhabu hiyo kwenye Gereza la Segerea, Dar.
Watu mbalimbali waliokuwepo mahakamani hapo, walimsikitikia Sikujua kutokana na hali yake.

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.