Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Tuesday, January 24, 2012

MZUNGU AFIA HOTELINI DAR


 Musa Mateja na Richard Bukos SIRI ya mwanaume Mzungu (jina halikupatikana mara moja) aliyefariki dunia Januari 21, mwaka huu akiwa ndani ya chumba alichopanga kwenye hoteli moja iliyopo Sinza, jijini Dar es Salaam imefichuka, Ijumaa Wikienda limeinyaka.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho kinafanya kazi kwenye hoteli hiyo, usiku wa kifo chake, mwanaume huyo alitoka kwenda matembezini, aliporudi alikuwa ameongozana na msichana wa Kitanzania aliyekuwa akizungumza Kiingereza vizuri.
“Usiku yeye alitoka, sijui alikwenda wapi? Aliporudi alikuwa na msichana mzuri tu, naamini ni Mtanzania maana alisalimia Kiswahili, lakini pia alikuwa akiongea Kiingereza vizuri na marehemu,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa wawili hao walionekana kuwa na amani muda wote wa mazungumzo yao lakini cha kushangaza, asubuhi mwanaume huyo alikutwa amefariki dunia chumbani akiwa peke yake.
Aidha, nje ya hoteli hiyo, baadhi ya watu waliokuwa wakishuhudia mwili wa marehemu ukiingizwa ndani ya gari la polisi, Land Rover lenye namba za usajili T 760 ADY walisikika wakisema huenda mrembo aliyekuwa na mtasha huyo alimwekea madawa ya kulevya kwenye kinywaji ili amwibie fedha.
“Kama alikuwa na hawa mademu wetu wa Kibongo, usikute alimwekea madawa ya kulevya ili amwibie hela zake, sasa kila mtu na afya yake, mwingine analewa tu, mwingine anakufa kabisa,” alisema shuhuda mmoja baada ya kusikia minong’ono ya kuwepo kwa mwanamke usiku wa tukio.

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.