Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Wednesday, January 18, 2012

MAELFU WAJITOKEZA MAPOKEZI YA MH.REGIA MTEMA IFAKARA







Maelfu ya wananchi wa mji wa Ifakara wakiwa barabarani ambako walizuia ambulance iliyobeba mwili wa marehemu.Kwa mujibu wa wenyeji, haijawahi kushuhudiwa mapokezi kama haya katika msiba wowote ule katika historia ya mji huu.Mwenyekiti wa CHADEMA taifa alilazimika kuwaomba vijana kutulia kwani walikuwa wamejawa na jazba na taharuki.Baada ya mwili kuingizwa katika nyumba ya familia kwa muda, ulihamishiwa hospitali hadi baadaye utakapotolewa kwa ratiba nyingine.Msafara kutokea Dar es salaam uliwasili Ifakara saa 4 usiku na maandamano yaliuchelewesha kufika nyumbani kwa marehemu.wageni kutoka Dar es salaam walifika ndani saa 5 usiku.Msafara kutoka Dar es salaam ulikuwa na magari yapatayo 60, ambayo mwandishi wa habari hii aliweza mwenyewe kuhesabu.Tutaendelea kuwahabarisha kutokea Ifakara.


Chanzo: Mjengwablog

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.