Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Saturday, January 14, 2012

NYOKA WENYE MAPEMBE WAGUNDULIWA TANZANIA


WATAALAMU wanaoshughulika na hifadhi ya mazingira nchini Tanzania wamegundua
kipiribao (nyoka mwenye sumu kali) mwenye pembe ambaye wanasema yuko katika hatari ya kutoweka.

Nyoka huyo mwenye rangi za kupendeza za njano na nyeusi ameelezwa kufanana na nyoka
anayepatikana katika milima ya Usambara na hata Uluguru anayekwenda kwa jina la Usambara.

Nyoka huyo mpya ambaye makazi yake bado kuelezwa kiusahihi anapatikana katika nyanda za juu kusini mwa Tanzania na alibainika wakati wa tathmini za kibaiolojia kwa mwaka 2010 na 2011 katika maeneo hayo.

Wataalamu wanaohusika na utafiti huo wamekataa kuelezea eneo halisi wanakopatikana nyoka hao kwa hofu ya wapenzi wa wanyama kwenda kuwawinda na kuwatwaa wakati viumbe hao inaonekana wapo katika kundi la wanaotoweka duniani.

Kipiribao huyo ambaye alielezwa kwa undani katika jarida la utafiti la Zootaxa la Desemba 6,2011 anaonekana kama mwindaji wa usiku na chakula chake kikuu ni vyura ambao huwapata kandoni mwa mito.
Kwa mujibu wa maelezo nyoka huyo anafanana na kipiribao mwingine anayejulikana kama Usambara ambaye inaaminika hupatikana pia katika milima ya Uluguru.


No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.