Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Wednesday, February 22, 2012

Strauss-Kahn ahusishwa katika ngono tena

Strauss-Kahn anahojiwa na polisi kwa tuhuma za biashara ya ngono
Aliyekuwa mkuu wa Shirika la Fedha Duniani Bwana Strauss-Kahn, anahojiwa na polisi nchini Ufaransa kama mshukiwa wa sakata ya biashara ya ngono.
Bwana Strauss-Kahn ambaye pia aliwahi kuwa mstari wa mbele katika kuwania urais nchini humo, amezuiliwa katika kituo cha polisi mjini Lille kaskazini mwa Ufaransa.
Polisi wamehoji makahaba kadhaa waliodai kuwahi kuwa na uhusiano wa kingono na bwana Strauss-Kahn.
Hata hivyo amesisitiza kuwa hakufahamu ikiwa wanawake hao walikuwa makahaba.
Bwana Strauss-Kahn alijiuzulu wadhifa wake kama mkuu wa Shirika la Fedha duniani mwezi Mei mwaka 2011 baada ya kukabiliwa na tuhuma za jaribio la kumbaka mfanyakazi wa hoteli mjini New York Marekani.
Hata hivyo baadaye kesi hiyo ilitupiliwa mbali.
Katika uchunguzi huu polisi nchini Ufaransa tayari wanawachunguza wanaume wawili kwa makosa ya kuunda mitandao ya ukahaba na kufuja pesa za shirika la IMF kwa kulipia biashara za ngono.

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.