Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Friday, March 2, 2012

Wanaume kujichubua hakuongezi ubora wa filamu

Shabani Matutu

KARIBUNI katika safu hii ya ‘Vunja vunja’ ambayo hukuijia kila Ijumaa ikiwa maalumu kwa ajili ya kuchambua filamu za nyumbani lengo likiwa kuboresha na kuzifanya zifikie levo za kimataifa.
Leo tumekuwa na mada ambayop nahisi itakuwa ikizungumzia kuhusu waigizaji wetu wa kiume takriban wote kuingia katika mkumbo wa kujichubua ngozi huku wengi wakidhani huenda kunaongeza ubora wa filamu.
Sababu kubwa ya kuandika mada hiyo imetokana na wimbi kubwa lililoibuka kwa wasanii wengi waigizaji wa kiume wa hapa nyumbani kutumia mkorogo maarufu kama ‘Karolaiti’.
Suala hili si geni kwa watazamaji wa tasnia hii ya filamu ambao wamekuwa mashuhuda wakiwashuhudia baadhi ya waigizaji walioanza wakiwa weusi tena wa kuvutia kuwatazama lakini hivi sasa wamejikoroga na kushindwa kuwatambua aina ya rangi zao kama ni weupe, njano au wekundu.
Kutokana na katabia hako walikojijengea wanaume kwa kufanya mambo ambayo hufanywa na mabinti imenifanya nikose uvumilivu kama mdau.
Swali jingine linaloniumiza kichwa kuhusu tabia hii ni kwamba, wanafikiria kwamba wanapojichubua ndipo filamu zao zitaongeza ubora au kupiga bao nje ya nchi?
Swali jingine ninalojiuliza ni kwamba wanafanya hivyo ili wawe kama Wazungu ambao ndio wamefanikiwa katika fani hii ya uigizaji?
Napenda kuwashauri kuwa kujipodoa hakukatazwi lakini kitu cha muhimu ambacho wasanii hawa wanapaswa kuangalia ni kuepuka kujichubua ngozi zao.
Pia wao kama kioo cha jamii wakumbuke kuwa mbali ya kwenda kinyume na tamaduni za mtoto wa kiume matumizi ya mikorogo ni hatari kwa ngozi ya binadamu.
Wasanii wa hapa nyumbani wanatakiwa kuachana na dhana mgando za kutumia mikorogo kwa kutaka pengine kufanana na Ramsey.
Si vibaya kwa mtoto wa kiume kujipamba lakini si busara wala hekima kwa mwanamume kujichubua ngozi yako.
Waigizaji wa hapa nyumbani wanatakiwa wajifunze madhara ya kujichubua kupitia kwa mfalme wa Pop duniani, Michael Jackson kwa yaliyompata ya ngozi kutoka.
Wanachopaswa kujua wasanii wetu ni kwamba kuiga mambo yanayoelimisha ambapo pia hayaathiri mila na tamaduni zetu hakuna wasiwasi.
Kinachosikitisha ni kwa wasanii hawa kupenda kuiga bila kujua faida au athari ya kile anachoiga kutoka kwa mastaa mbalimbali duniani.
Wasanii hao wanachotakiwa ni kujali kufanya kazi kwa bidii kitendo ambacho kinaweza kuwaletea umaarufu katika fani hiyo.
Kuna nyota kama Danzel Washington, Bill Branks wamefanikiwa kupata umaarufu sana katika tasnia hiyo wakiwa na ngozi zao za asili sasa kama ubora ungekuwa unapatikana katika kubadili rangi wangefanya hivyo kwa kuwa kwao ni bei rahisi.

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.