Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Thursday, March 1, 2012

Majina Ya Wajumbe Wa Tume Ya Katiba

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

S.L.P 70069, DAR ES SALAAM

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Jumatano, Februari 29, 2012

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete amevialika vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, jumuiya za
kidini, asasi za kiraia na makundi mengine ya watu wenye malengo yanayofanana
kuwasilisha kwake orodha ya majina ya watu watakaoteuliwa kuwa Wajumbe wa
Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi kuhusu Mabadiliko ya Katiba.

Mheshimiwa Rais ametoa mwaliko huo kupitia Tangazo la Serikali Na. 66 la tarehe
24 Februari, 2012 kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 6(6) cha Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011.

Kifungu cha 6(6) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, 2011 kinamtaka Mheshimiwa
Rais kualika vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, jumuiya za dini, asasi za
kiraia, jumuiya, taasisi na makundi mengine ya watu wenye malengo yanayofanana
kuwsilisha kwa Rais orodha ya majina ya watu kwa ajili ya kuteuliwa kuwa
wajumbe wa Tume.

Kwa mujibu wa Tangazo hilo la Serikali, kila chama cha siasa chenye usajili wa
kudumu, jumuiya ya kidini, asasi ya kiraia na kila kundi lenye watu wenye malengo
yanayofanana itapaswa kuwasilisha orodha ya majina yasiyozidi matatu ambayo
itaonyesha umri, jinsia, uzoefu, sifa na mahali anapoishi kila mtu aliyemo katika
orodha.

Aidha, orodha hiyo inatakiwa iwasilishwe kwa Mheshimiwa Rais kwa maandishi
ama moja kwa moja kwa mkono au kwa rejista ya posta kupitia anuani ifuatayo:

i.

ii.

Ama: Katibu Mkuu Kiongozi,
Ikulu,
S.L.P. 9120,
DAR ES SALAAM

Au:

Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi,
Ofisi ya Rais,
S.L.P. 4224,
ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.