Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Thursday, March 1, 2012

Mkutano Wa Mawaziri Kigoma



Na Lulu Mussa

Mkutano wa Tano wa Mawaziri wa Mamlaka ya ziwa Tanganyika ulifanyika jana mkoani

Kigoma, ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya mkataba uliounda mamlaka hiyo.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dk.

Terezya Huvisa amesema kuwa ili kulinusuru Ziwa Tanganyika jitahada za Nchi zote nne ni

muhimu katika kukabiliana na changamoto zinazolikabili ziwa hilo kwa sasa kwa kutumia

fursa zilizopo.

Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uchafuzi mkubwa wa mazingira ikiwa ni

pamoja na kujaa kwa taka za majumbani na zile za viwandani, uvuvi haramu kutokana

na ongezeko la watu, kilimo na ufugaji usio endelevu. Hata hivyo Waziri Huvisa

amewakumbusha wajumbe wa Mkutano huo kuwa Ziwa Tanganyika linaunganisha Nchi zote

nne badala ya kuzitenganisha, hivyo ni muhimu kuwa na mikakati endelevu ya kuhifadhi ziwa

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa katika Mkutano huo ni pamoja na Utekelezaji wa

Mpango Mkakati wa Kitaifa ambao kwa sasa unafanya kazi katika nchi zote pamoja na

Mkakati wa kukusanya fedha kwa ajili ya kuwa na usimamizi endelevu wa Ziwa Tanganyika

baadaya ya mwaka 2013 ambapo fedha za wafadhili zitafikia kikomo.

Katika Mkakati huo wa kukusanya fedha Nchi zote nne zimetia saini makubaliano ya

kuchangia fedha ili hifadhi ya Ziwa hilo iwe endelevu, ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa

miradi mbalimbali.

Mkutano huo umefanyika Tanzania kwa mara ya pili, mkutano mwingine kama huo ulifanyika

jijini Dar es Salaam mwaka 2007. Mamlaka hiyo ya Ziwa Tanganyika inaundwa na nchi za

Zambia, Burundi, Congo (DRC) na mwenyeji Tanzania.
 
 
Mjengwablog

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.