Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Sunday, November 27, 2011

Lowassa Ni Msafi, Hahitaji Kusafishwa ( Jibu)

Mjengwa naomba tena, jukwaani nirejee
Niliyoandika jana, napenda niyatetee
Mkuranga kimanzichana, Lowassa aendelee
Nkwazi hujaelewa, umefakamia mada

Mhango kajichanganya, kujibu asichojua
Kauropoka unyanya, pasipo kulitambua
Si hasi wala si chanya, Nkwazi kasimamia
Mhango wajipotosha, kujibu usichojua

Lowassa ni mtu safi, tegua kitendawili
Angelikuwa ni ni fisi, mahakama mhimili
Hojazo ni mufilisi, wewe ndumilakuwili
Nkwazi rudi shuleni, kaisome CCM

Mhango wanishangaza, ukweli kutofahamu
Waonekana kilaza, rejea Dar es salaamu
Kwa hoja ntakuchakaza, wewe mwana wa Adamu
CCM huijui, fitina wamezoea

Lowassa ni kiongozi, hili unalitambua
Achana na upuuzi, ule walomzushia
Usijifanye dandizi, kudandia usojua
Nkwazi mwana Mhango, uliza nakusikia


Beti sita natuama, nimefikia tamati
Lowassa mtu wa maana, hodari wa mikakati
Nkwazi soma kwa sana, tambua hizi nyakati
Lowassa ni mtu safi, hahitaji kusafishwa.

Nova Kambota
Tanzania, East Africa

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.