Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Wednesday, June 4, 2014

MASKINI TEMBO WETU, WAMEKOSA NINI JAMANI?


Ndugu zangu,
Ujangili umeendelea kushika kasi nchini Tanzania, hasa wa tembo, licha ya jitihada
kadhaa zinazofanywa na mamlaka husika.
Tembo kama huyu pichani anauawa kinyama na wendawazimu wachache ambao wanaangalia maslahi yao ya kuuza meno yake bila kujali hatma ya baadaye ya rasilimali zetu.
Zimekuwepo operesheni nyingi nchini, miongoni mwazo ni ile ya Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa mwaka 2013, ambayo ilisitishwa baada ya kudaiwa kwamba wasimamizi wake waliendesha vitendo vya utesaji kwa wale walioshukiwa kujihusisha na ujangili.
Lakini pamoja na kusitishwa huko, bado kikwazo kikubwa kinaonekana kipo serikalini, kwani tunaelezwa kwamba wapo maofisa wakubwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, na wanatengeneza mamilioni ya fedha.
Ndugu zangu, lazima tuwe wazalendo, tuungane kwa pamoja kupinga unyama na ujambazi huu ambao kama hatukisimama imara unaweza kuwapukutisha hayawani wote nchini na tukabaki na picha za wanyama kwenye vitabu vyetu vya historia. Tembo ndiye mnyama mkubwa kabisa aliyesalia duniani katika jamii zile za dinosaur, hivyo ni urithi mwingine kwa vizazi vyetu.

Ndugu yenu,

Daniel Mbega,

Iringa - Tanzania
Ndugu zangu,
Ujangili umeendelea kushika kasi nchini Tanzania, hasa wa tembo, licha ya jitihada kadhaa zinazofanywa na mamlaka husika.
Tembo kama huyu pichani anauawa kinyama na wendawazimu wachache ambao wanaangalia maslahi yao ya kuuza meno yake bila kujali hatma ya baadaye ya rasilimali zetu.
Zimekuwepo operesheni nyingi nchini, miongoni mwazo ni ile ya Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa mwaka 2013, ambayo ilisitishwa baada ya kudaiwa kwamba wasimamizi wake waliendesha vitendo vya utesaji kwa wale walioshukiwa kujihusisha na ujangili.
Lakini pamoja na kusitishwa huko, bado kikwazo kikubwa kinaonekana kipo serikalini, kwani tunaelezwa kwamba wapo maofisa wakubwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, na wanatengeneza mamilioni ya fedha.
Ndugu zangu, lazima tuwe wazalendo, tuungane kwa pamoja kupinga unyama na ujambazi huu ambao kama hatukisimama imara unaweza kuwapukutisha hayawani wote nchini na tukabaki na picha za wanyama kwenye vitabu vyetu vya historia. Tembo ndiye mnyama mkubwa kabisa aliyesalia duniani katika jamii zile za dinosaur, hivyo ni urithi mwingine kwa vizazi vyetu.
Ndugu yenu,
Daniel Mbega,
Iringa - Tanzania
source: MASKINI TEMBO WETU & www.mjengwablog.com

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.