Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Wednesday, January 25, 2012

Mkulima afa kwa kunyweshwa tindikali

  


MKULIMA wa kijiji cha Kibwigwa kata ya Mwayaya wilayani Kasulu, Gaudence Kibiriti, ameuawa na wananchi wa kijiji hicho kwa kunyweshwa tindikali aina ya Caustic.

Wananchi hao walifanya mauaji hayo mwanzoni mwa wiki hii wakimtuhumu kumkingia kifua baba yake, anayetuhumiwa kufanya vitendo vya kishirikina.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa Kigoma, Fraiser Kashai, aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa jana, kwamba baada ya kumwua mkulima huyo, wananchi hao walimshambulia baba yake mzazi, Kibiriti Shingwa, na kumjeruhi kwa kummwagia tindikali hiyo pia.

Alisema awali wananchi hao walivamia nyumbani kwa Gaudence na kurusha mawe juu ya paa la nyumba yake.

Baada ya hali hiyo, Gaudence alitoka nje ili kunusuru maisha yake, ndipo wananchi walipomkamata na kumnywesha tindikali hiyo na nyingine kummwagia mwilini na
kumsababishia kifo hicho.

Katika tafrani hiyo kwa mujibu wa Kamanda Kashai, wanakijiji hao walivamia shamba la migomba la marehemu lenye ukubwa wa robo heka na kufyeka mazao yote.

Pia waliharibu nyumba zake mbili na kumjeruhi Shingwa sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kummwagia tindikali.

Alisema majeruhi amelazwa katika Hospitali ya Misheni ya Heri katika tarafa ya Manyovu, Kasulu kwa matibabu na juhudi za Polisi kuwatafuta watuhumiwa zinaendelea na hadi jana hakuna mtu ambaye alishakamatwa.

Katika tukio lingine, Kamanda Kashai alisema Polisi inamshikilia mkulima wa kijiji cha Bweranka, Kasulu, Ngenzi Maliyatabu, kwa tuhuma za kukutwa na vipande 13 vya meno ya tembo vikiwa kwenye magunia ya mchele.

Mtuhumiwa alikamatwa juzi Kasulu akiwa kwenye basi la Adventure lililokuwa likitoka Mpanda, Rukwa kuja hapa na alikamatwa baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema.

Tukio la mkulima huyo kunyweshwa na kumwagiwa tindikali limekuja siku chache baada ya mfanyabiashara wa Zanzibar Alvind Asawla na mkewe Bimal, kupigwa risasi na kumwagiwa tindikali kwa sababu ambazo awali zilielezwa ni kutokana na kuuza pombe.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi Zanzibar lilisema mashambulizi hayo yaliyofanywa na watu wasiojulikana, hayahusiani na uuzaji pombe, bali ni ujambazi uliofanywa na watu waliokuwa wanataka fedha za mauzo ya mfanyabiashara huyo.

Wanafamilia hao walivamiwa Jumatano wiki jana, wakiwa njiani kurudi nyumbani. Bimal alishambuliwa na risasi tumboni na kumwagiwa tindikali huku akiwa na ujauzito wa miezi minne.

Mumewe alipigwa risasi ya uso iliyotokea upande wa pili shingoni na wote walijeruhiwa na wamelazwa hospitalini Dar es Salaam.

Septemba mwaka jana mfuasi wa CCM, Mussa Tesha (25), alimwagiwa tindikali na watu wasiojulikana, wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni Igunga, Tabora.

Baada ya tukio hilo, Tesha alipelekwa Hospitali ya Igunga na baadaye Muhimbili Dar es Salaam na kisha India, ambako alipata matibabu zaidi na hivi sasa amerejea nchini akiwa na makovu makubwa usoni.

 Na Habari Leo

SPEECH BY WILLIAM NGELEJA, MINISTER FOR ENERGY AND MINERALS DURING THE SIGNING CEREMONY OF PETROBRAS, HERITAGE AND MOTHERLAND PRODUCTION SHARING AGREEMENTS ON 24TH JANUARY, 2012


Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja

Today the Government of the United Republic of Tanzania through the Ministry of Energy & Minerals and TPDC is signing three Production Sharing Agreements (PSAs) with three Oil Exploration Companies, namely Petrobras Tanzania Ltd (Petrobras), Heritage Rukwa (TZ) Limited (Heritage) and Motherland Industries Ltd (Motherland). This is a testimony to the fact that TPDC and the Ministry continue to successfully attract further investment in petroleum upstream which is important in the development of the energy sector and our economy as a whole.
The term of the PSAs is eleven (11) years divided into three sub-periods namely: Initial Exploration Period of 4 Years; First Extension Period of 4 Years and the Second Extension Period of 3 Years. The PSAs provide an option for back-off at each stage and a mandatory surrender of 50% at the end of each period.
Today’s occasion of signing three PSAs is an important milestone towards exploration of hydrocarbons in Tanzania and East Africa at large. The Petrobras PSA is for hydrocarbon exploration in Block-8 deep offshore Tanzania, the Heritage PSA is for exploration in the Kyela Basin (northern and onshore portion of Lake Nyasa) and the Motherland PSA is for exploration in the Malagarasi Basin North West part of the country.
For Petrobas and Tanzania this is the beginning of another opportunity to explore the under-explored deep sea basins offshore Tanzania. For Heritage, Motherland and Tanzania, this opens another Chapter of exploration for hydrocarbons in the Inland Rift Basins. May I remind you of recent hydrocarbon discoveries made in analog deep-sea and inland rift basins in Angola, Mozambique, Ghana, Uganda and Sudan. These results have brought high optimism to our countries that have similar geology. The PSAs we are going to sign today is a testimony to that effect.
I have been informed that all three PSAs have been negotiated in good faith. In case of discovery, the Agreements offer a win-win situation for all parties. This is a very important aspect for Tanzania and exploration companies as well. A balanced Agreement to all Parties, the Nation and investors, rewards and smoothens operations throughout the life of exploitation, development and exploitation of the field in the case of a discovery.
In the PSA, each Party that is signing today has obligations to fulfill. I wish to assure all of you that the Government and TPDC are committed to fully cooperate with all parties in fulfilling the agreed terms of these PSAs. The Government of Tanzania adheres to the rule of law and operates in a transparent manner. Therefore, feel free to consult TPDC and other respective authorities including my office for advice and facilitation. In the same manner the Government and TPDC expect you to fulfill your Work Program and Budget commitments as per PSA.
Ladies and Gentlemen, at this point I would like to stress the importance of local contents in the Oil Exploration and Production as stated in the Agreements. By Local contents implies use of Tanzanian goods and services as well as human resources. I wish to commend Petrobras and Heritage who have employed a good number of Tanzanians in their offices. However, in the rig operations the employment to indigenous is still to pick-up. I request all of us present here today to observe this and work together to change this trend. We would like to have a good number of Tanzanians working in the rigs as well.
I request the three companies signing today to give preference to the purchase of Tanzanian goods, services and materials provided such goods, services and materials are available with the right quantity and quality. This will be in line with the Government’s efforts of job creation and empowerment.
Ladies and Gentlemen, may I mention a little bit about environment and Mother Nature. We all know that poorly planned petroleum exploration and production activities may turn out to be detrimental to the land, water, animals and plants through pollution. Some of the negative effects of pollution are irreversible. We also know that Petroleum Resources are non renewable. It will be to our disadvantage and disadvantage of our future generations if we undertake poorly planned exploration activities that will pollute the environment and probably halt other economic activities. I insist that every one of us has a responsibility of ensuring that Petroleum activities are carried out in a sustainable and environmentally friendly manner. In addition we need to have contingent plans ahead in case of oil spills.
Ladies and Gentlemen, exploration for oil and gas is capital intensive, risky and takes a long time. Attracting risky capital is not an easy task. Delivery of such capital is not an easy task too. I am therefore delighted to witness signing of these three agreements with Petrobas, Heritage and Motherland today. These three PSAs bring the number of exploration licenses in Tanzania to twenty (28) and number of exploration companies operating in Tanzania to 18, the highest number since exploration of oil and gas started in the country in the 1950s and indeed in the whole of eastern African countries. Other companies that are currently exploring in Tanzania include:-
• Maurel et Prom of France exploring in Bigwa and Mafia;
• Ndovu Resources of Australia exploring in Nyuni, East of SongoSongo and Ruvuma Basin located in Mtwara and Lindi Regions;
• Pan African Energy of UK producing gas at the SongoSongo Island;
• Dominion Oil and Gas of UK exploring in Block No. 7 in the deep water;
• Petrodel Oil and Gas of UK exploring in Dar es Salaam platform and Latham;
• Afren of UK exploring in Tanga;
• Petrobras of Brazil exploring in the deep water Block 5 and 6;
• BG of UK and Ophir Energy Company of Australia exploring in the deep water blocks 1, 3 and 4;
• Statoil of Norway exploring in the deep water Block 2;
• Dodsal Resources of UAE exploring in the Ruvu Block;
• RAK GAS of UAE exploring at Pande, East of Kilwa;
• Beach Petroleum of Australia exploring in south Lake Tanganyika; and
• Hydrotanz of Mauritius exploring in North of Mnazi Bay.
Apart from the aforementioned companies, there are a number of companies inquiring to explore in the open acreages available in the country. The Government is committed to continue promoting exploration for oil and gas in the country. This being one of the main objectives of our National Energy Policy which aims at ensuring that the country taps a reliable supply of energy and energy services to all parts of the country at a least cost and with due regard to the environment.
In promoting exploration for oil and natural gas, the Government will ensure that the Production Sharing Terms are competitive enough to secure the Nation’s interests and provide adequate incentives to investors.
I therefore wish to take this opportunity to invite more companies both local and foreign to invest more in exploration for oil and natural gas, and establish service companies in the country as well as invest in other areas in the energy sector.
Ladies and Gentlemen, I would like to commend Petrobras, Heritage and Motherland for their decision to come to Tanzania as their destination of choice for investing in petroleum upstream activities. It is our hope that you will be good corporate citizens and that you will carry out your activities in accordance with good industry practice. We do expect that as part of your corporate responsibility you will assist the communities in your various Contract Areas whenever possible within manageable limits.
Once again, let me thank you all for taking your time to come to this great occasion.
THANK YOU


Entering into Production Sharing Agreements (PSAs) with Petrobras Tanzania Limited, Heritage Rukwa Tanzania Limited and Motherland Industries Limited
MINISTER William M. NGELEJA SIGNS THREE NEW PRODUCTION SHARING AGREEMENT
The Government of the United Republic of Tanzania and the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) have signed three Production Sharing Agreements (PSAs) with three petroleum exploration companies. The signing ceremony took place on 24th January 2012 in the Ministry of Energy and Minerals offices in Dar es Salaam.
The Government was represented by the Minister for Energy and Minerals Hon. William M. Ngeleja (MP) and TPDC was represented by its Chairman of the Board of Directors Mr. Michael Mwanda and the Managing Director Mr. Yona Killagane.
The counterparts in the signing were represented as follows: Mr. Samuel Miranda, Managing Director for Petrobras Tanzania Limited (Petrobras); Mr. Julian Heawood, General Manager for Heritage Rukwa (TZ) Limited (Heritage); and Mr. V.K. Sood, Director of Operations for Motherland Industries Ltd (Motherland).
Speaking during the ceremony, Minister Ngeleja informed the audience that, signing of the three PSAs was an important milestone towards exploration of hydrocarbons in Tanzania and East Africa in general. The Petrobras PSA is for exploration of hydrocarbons in Block-8 deep offshore Tanzania, the Heritage PSA is for exploration in the Kyela Basin (northern basin of onshore Lake Nyasa) and the Motherland PSA is for exploration in the Malagarasi Basin east of Lake Tanganyika in Northwest Tanzania.
The duration of the signed PSAs as per Petroleum Exploration and Production Act, 1980 will be eleven (11) years divided into three sub-periods namely: Initial Exploration Period of 4 Years; First Extension Period of 4 Years and the Second Extension Period of 3 Years. The PSAs provide an option for back-off at each stage and a mandatory surrender of 50% at the end of each period.
For Petrobas and Tanzania this is the beginning of another opportunity to explore the under-explored deep sea basins offshore Tanzania. For Heritage, Motherland and Tanzania, the signing opens another chapter of exploration for hydrocarbons in the Inland Rift Basins.
Recently there have been discoveries of oil and gas in similar deep-sea and inland rift basins in Angola, Mozambique, Ghana, Uganda and Sudan., These results have brought high optimism to Tanzania which has similar geology.
The Minister informed that, each Party that signed the Agreement has obligations to fulfill. The Minister assured the three companies that the Government and TPDC are committed to fully cooperate with all parties in fulfilling the agreed terms of the signed PSAs. He further said that the Government of Tanzania adheres to the rule of law and operates in a transparent manner. The Minister told the investors to feel free to consult TPDC and other respective authorities including the Minister’s office for advice and facilitation. The Minister informed the investors that the Government and TPDC look ahead to the Companies fulfilling their Work Programs as committed in the various PSAs.
The Minister requested the three companies to give preference to the purchase of Tanzanian goods, services and materials, in line with the Government’s efforts of job creation and empowerment.
The Minister further informed that, poorly planned petroleum exploration and production activities may turn out to be detrimental to the land, water, animals and plants through pollution. Some of the negative effects of pollution from oil are irreversible. He also reminded that Petroleum Resources are non renewable. He urged that for our advantage and advantage of future generations it is necessary to undertake well planned exploration activities that will not pollute the environment. Pollution of the environment may halt other economic activities. The Minister added that, it is necessary to have contingent plans ahead in case of oil spills.
The signed three PSAs bring the number of exploration licenses in Tanzania to twenty (28) and a number of exploration companies operating in Tanzania to 18, the highest number since exploration of oil and gas started in the country in the 1950s and indeed in the whole of eastern Africa countries. Other companies that are currently exploring in Tanzania include:-
• Maurel et Prom of France exploring in Bigwa and Mafia as well as producing gas at Mnazi Bay;
• Ndovu Resources of Australia exploring in Nyuni, East of Songo Songo and Ruvuma Basin located in Mtwara and Lindi Regions;
• Pan African Energy of UK producing gas at the Songo Songo Island;
• Dominion Oil and Gas of UK exploring in Block No. 7 in the deep water;
• Petrodel Oil and Gas of UK exploring in Dar es Salaam platform and Latham;
• Afren of UK exploring in Tanga;
• Petrobras of Brazil exploring in the deep water Block 5 and 6;
• BG of UK and Ophir Energy Company of Australia exploring in the deep water Blocks 1, 3 and 4;
• Statoil of Norway exploring in the deep water Block 2;
• Dodsal Resources of UAE exploring in the Ruvu Block;
• Ophir and RAK GAS of UAE exploring the East Pande block in Kilwa;
• Beach Petroleum of Australia exploring in South Lake Tanganyika; and
• Hydrotanz of Mauritius exploring in North of Mnazi Bay.
Apart from the aforementioned companies, there are a number of companies inquiring to explore in the open acreages in the country. The Government is committed to continue promoting exploration for oil and gas in the country. This being one of the main objectives of our National Energy Policy which aims at ensuring that the country taps a reliable supply of energy and energy services to all parts of the country at a least cost and with due regard to the environment.
In promoting exploration for oil and natural gas, the Government will ensure that the Production Sharing Terms are competitive enough to secure the Nation’s interests and provide adequate incentives to investors.
The Minister took the opportunity to invite more companies both local and foreign to invest more in exploration for oil and natural gas, and establish service companies in the country as well as invest in other areas in the energy sector.
He commended Petrobras, Heritage and Motherland for their decision to come to Tanzania as their destination of choice for investing in petroleum upstream activities. The Minister expects that as part of their corporate responsibility the three companies will assist the communities in their various Contract Areas whenever possible within manageable limits.

Tuesday, January 24, 2012

Mjamzito Anaswa kwa Ukahaba







Na Richard Bukos
MREMBO Sikujua Hassan, mwenye ujauzito unaokadiriwa kuwa na umri wa miezi sita, alinaswa akifanya ukahaba, Buguruni, Dar es Salaam.
Sikujua, alinaswa na polisi kisha kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Sokoine Drive, Dar es Salaam ambapo alikiri kosa la kujihusisha na ukahaba.
Baada ya kukiri kosa, Hakimu Mkazi, William Mutaki, alimhukumu kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi 20,000.
Hata hivyo, Sikujua hakuweza kulipa faini, kwa hiyo aliamriwa kwenda gerezani pamoja na ujauzito wake.
Sikujua amepangiwa kutumikia adhabu hiyo kwenye Gereza la Segerea, Dar.
Watu mbalimbali waliokuwepo mahakamani hapo, walimsikitikia Sikujua kutokana na hali yake.

JK akutana na mjumbe maalum wa Cuba



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Januari 24, 2012, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Masula ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Cuba, Bwana Alberto Velazco San Jose.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete na Bwana San Jose wamezungumzia masuala yanayohusu uhusiano kati ya Tanzania na Cuba, masuala ya kanda ya Afrika na masuala mbalimbali ya kimataifa likiwamo lile la vikwazo ambazo Marekani iliiwekea Cuba tokea miaka ya 1960 na inaviendeleza.

“Uhusiano mzuri, wa karibu na wa miaka mingi ni kielelezo halisi cha jinsi nchi mbili ndogo na zinazoendelea zinavyoweza kushirikiana na kusaidiana kama ndugu,” Rais Kikwete amesema katika mazungumzo hayo na kuongeza, “Nipende pia kuishukuru Cuba na wananchi wa Cuba kwa kuunga mkono jitihada za maendeleo za nchi yetu miaka yote hii pamoja na kwamba mmeendelea kupambana na vikwazo vikubwa vya kila aina.”



Kwa miaka mingi, Tanzania na Cuba zimekuwa zinashirikiana katika masuala mengi na kusaidiana katika masuala ya kimataifa, na Cuba imeunga mkono jitihada za maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali zikiwamo za afya, elimu na michezo.

Bwana Alberto Valazco San Jose amemjulisha Rais Kikwete kuhusu mageuzi ya kiuchumi ambayo nchi hiyo inayafanya kwa kufungua uchumi wake kutoka uchumi wa dola na kuuelekeza kwenye uchumi wa soko ambako watu binafsi wanapata nafasi kushiriki katika uchumi wa nchi yao.

“Tunafanya mageuzi makubwa katika uchumi wetu kwa kuutoa kwenye uchumi wa dola na kuruhusu sekta binafsi kushiriki kwenye ujenzi wa uchumi huo. Tunafanya mageuzi lakini hatuna haraka kwa sababu hatutaki kufanya makosa katika jambo hili,” amesema Mkurugenzi huyo.

Naye Rais Kikwete ametumia nafasi hiyo kumjulisha Mkurugenzi huyo kuhusu jitihada za Serikali yake katika kujenga mazingira ya kuwaletea maisha bora Watanzania kwa kumweleza jitihada za Serikali kupambana na ugonjwa wa malaria, kuongeza uzalishaji wa sukari, kuongeza uzalishaji wa umeme, kupanua na kuboresha elimu na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Cuba ni moja ya mataifa yanayoongoza duniani kwa uzalishaji wa sukari, na imekuwa inajenga kiwanda cha dawa ya kuua mbu katika jitihada zake za kuisaidia Tanzania kukabiliana na ugonjwa wa malaria.

Rais Kikwete pia amemweleza mgeni huyo kuhusu jitihada za Serikali yake katika kuboresha miundombinu nchini kwa kuboresha usafiri wa reli, kukabiliana na matatizo katika usafiri wa anga, upanuzi na uboreshaji wa bandari za Tanzania na uendelezaji wa ujenzi wa barabara za lami nchini.


Bwana Alberto Valelazco San Jose yuko katika ziara za nchi za Afrika akiwa njiani kwenda Addis Ababa, Ethiopia kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (AU) utakaofanyika Januari 29-30 mwaka huu.

Wakati huo huo, Rais Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Kundi la Makampuni ya Frontline Development Partners ya Dubai inayotaka kuwekeza katika masuala ya maji, kilimo cha miwa na uzalishaji wa sukari, usafirishaji wa reli na uzalishaji wa umeme.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

24 Januari, 2012

GLOBAL AFUNGA NDOA NA MAITI YA MCHUMBA WAKE HUKO THAILAND


Dave akitimiza dhamira kwa kumvisha pete kidoleni.
Dave akiibusu maiti ya aliyekuwa mchumba wake.
MKURUGENZI wa kituo kiumoja cha televisheni nchini Thiland aitwaye Chadil Deffy au Deff  Yingyuen, akitaka kuonyesha upendo wake kwa mchumba wake wa siku nyingi aliyekuwa akiitwa Sarinya au “Anne” Kamsook, aliyefariki karibuni katika ajali ya gari, aliamua kufunga ndoa na maiti yake.
Baada ya kufanya hivyo, alizituma picha za tukio hilo kwenye mtandao wa Facebook na YouTube, kitendo ambacho kiliwashangaza watu wengi duniani.
Ndoa hiyo ya ajabu ilifanyika wakati mmoja na mazishi ya maiti ya bi harusi huko Amphur Muang, jimbo la Surin, nchini Thailand ambapo pia palifanyika mazishi ya mchumba huyo aliyekuwa na umri wa miaka 29 sehemu hiyo hiyo.
Deffy ambaye jina lake la utani ni “Dave” alikutana na Sarinya wakati wanasoma Chuo Kikuu cha Asia Mashariki miaka kumi iliyopita na wakapanga kuoana, lakini mwanamke huyo akafariki Januari 3 mwaka huu.

Wakati wa mazishi hayo, bwana harusi alionekana akiwa amevalia suti nyeusi na akimvisha mchumba wake huyo pete.

Tukio hilo lilishirikiwa na marafiki na jamaa wengi wakiwemo wacheza sinema, waimbaji na wanafunzi wenzao wa chuo kikuu hicho ambao walishiriki kwa kuwapa pongezi na kutoa maua.

GLOBAL PUBLISHERS

Mrembo Avua Nguo Kortini








Richard Bukos na Makongoro Oging’

ELIZABETH Florian ‘Eliza’, Mkazi Dar es Salaam, wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela baada ya kukutwa na hatia ya kuvua nguo…




Richard Bukos na Makongoro Oging’
ELIZABETH Florian ‘Eliza’, Mkazi Dar es Salaam, wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela baada ya kukutwa na hatia ya kuvua nguo mahakamani.
Eliza, alifanya kitendo hicho kama sehemu ya kupinga mashtaka dhidi yake ambayo alisomewa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Sokoine Drive, Dar es Salaam.
Mrembo huyo, alisomewa mashtaka ya ukahaba kisha akakiri kosa, alipohukumiwa kulipa faini ya shilingi 20,000, alivua nguo na kubaki mtupu.
Kutokana na kutenda kosa hilo waziwazi, tena mbele yake, Hakimu Mkazi, William Mutaki, alimhukumu kwenda jela miezi sita.
Binti mwingine, Evonia William (anaonekana ukurasa wa kwanza akilia), aliibua hekaheka ya aina yake mahakamani.
Evonia, baada ya kusomewa mashtaka ya ukahaba, alikana kosa, hivyo akatakiwa apate wadhamini.
Hata hivyo, baada ya kukosa wadhamini, aliamriwa kwenda mahabusu Gereza la Segerea, Dar, mpaka Januari 31, mwaka huu.
Kutokana na amri hiyo, Evonia aliangua kilio, hivyo kuibua hekaheka ya aina yake, ingawa askari wa mahakama hiyo walifanikiwa kumtuliza baada ya muda mrefu.

From: Global Publishers

LIBYA DAMU UPYA









Luqman maloto na vyanzo  vya kimataifa
YALIYONENWA kuhusu damu kuendelea kumwagika Libya yameanza kudhihirika kwa vitendo, amani ya nchi hiyo ni msamiati mgumu kutokana na machafuko yaliyoibuka wiki iliyopita ambayo almanusra yasababishe vifo vya viongozi wakuu wapya wa nchi hiyo.
Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Taifa (NTC), Mustafa Abdul Jalil ambaye ni kiongozi mkuu wa nchi hiyo kwa sasa na makamu wake, Abdul Hafiz Ghoga, walinusurika kuuawa Jumamosi iliyopita.
Jalil, aliponea chupuchupu baada ya walinzi wake kumtoroshea mlango wa nyuma, kuwakwepa waandamanaji waliovamia Makao Makuu ya NTC, Benghazi na kuvunja ofisi hizo za serikali ya muda.
Baada ya Jalil kuokolewa na walinzi wake, waandamanaji hao wakiwa na hasira, walilivamia gari lake na kulivunjavunja kabla ya kuliacha nyang’anyang’a.
Kwa upande wa Ghoga, alizingirwa na wanafunzi wa vyuo vikuu mjini Benghazi lakini aliokolewa kabla hawajamdhuru.
Jalil ndiye aliyekuwa na wakati mgumu zaidi, kwani alitupiwa vitu mbalimbali ambavyo hata hivyo, havikumjeruhi.

MADAI YA WAANDAMANAJI
Waandamanaji nchini Libya, wamegawanyika kwenye makundi matatu na kila upande una sababu zake ambazo unataka zisikilizwe na kufanyiwa kazi.
Makundi yote, yanaungana kwenye pointi moja kuwa ni lazima uongozi wa NTC ung’oke kwa sababu umeshindwa kutekeleza mahitaji yao.

KUNDI LA KWANZA
Ni wananchi wanaotaka uwazi kuhusu rasilimali za Libya. Wanadai kuwa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo, Muammar Gaddafi, aliacha fedha na mali nyingi kwa ajili ya Walibya lakini zinatumika bila mpangilio wala maelezo.
Wanadai kuwa maisha yamekuwa magumu, wakati enzi za Gaddafi kulikuwa na hali nzuri. Vilevile wanailaumu NTC kwa kuunda sheria ya uchaguzi bila kuwashirikisha wananchi.

KUNDI LA PILI
Ni wapiganaji walioshiriki kumng’oa Gaddafi. Wanadai kuwa NTC imewatenga katika muundo wa serikali ya mpito na hata fedha walizopewa kama mgawo, hazitoshelezi mahitaji yao na hazilingani na nguvu waliyotumia.
Wapiganaji hao ambao wengi wao walivamia ofisi za NTC wakiwa na majeraha yaliyotokana na vita, wanaishutumu NTC kwa kushirikisha baadhi ya watumishi wa umma waliokuwepo tangu enzi za Gaddafi.

KUNDI LA TATU
Ni wanaharakati wa Islamic Brotherhood ambao wanadai Libya ni nchi ya Kiislam, kwa hiyo ni lazima iongozwe kwa sharia, hivyo wanataka NTC ing’oke kupisha muundo wa serikali utakaofuata misingi ya Uislam.

NI LAANA YA GADDAFI?
Kabla ya Benghazi, wananchi wa Jiji la Sirte walikuwa wa kwanza kulalamikia kuwa maisha ya Libya yamekuwa mabovu tangu kupinduliwa na hatimaye kuuawa kwa Gaddafi.
Wananchi hao walilalamika kuwa Gaddafi aliwasaidia kujenga nyumba lakini NTC walibomoa, kadhalika alilinda maisha yao ila baraza hilo la mpito liliua raia wakati wa vita wakisaidiwa na Jeshi la Kujihami la Nchi za Magharibi (Nato).

Wananchi wa Sirte walitoa msimamo kuwa Libya haitakalika mpaka damu ya Gaddafi ifidiwe, pia kaburi alilozikwa liwekwe wazi ili kila raia wa Libya ajue mahali lilipo.
Leo ni siku ya 96 tangu Gaddafi alipokamatwa na kuuawa Oktoba 20, 2011. Kabla hajafa aliwauliza wapiganaji wa NTC: “Je, mnaujua ukweli katika uongo?”
Kulikuwa na mpiganaji aliyekuwa mstari wa mbele kumsulubu, akamuuliza: “Kama wewe, nimekukosea nini?”

Awali, ilionywa na wachambuzi wa siasa za kimataifa kuwa kupinduliwa kwa Gaddafi haiwezi kuwa suluhu ya amani Libya, badala yake inaweza kuchochea machafuko ya muda mrefu.
Inaelezwa kuwa kumekuwa na machafuko ya chini kwa chini ambayo yamekuwa yakiwaachia majeraha wananchi, wakiwemo wanawake na watoto.
PICHA ZOTE NA AFP


Chanzo: Global Publishers

MZUNGU AFIA HOTELINI DAR


 Musa Mateja na Richard Bukos SIRI ya mwanaume Mzungu (jina halikupatikana mara moja) aliyefariki dunia Januari 21, mwaka huu akiwa ndani ya chumba alichopanga kwenye hoteli moja iliyopo Sinza, jijini Dar es Salaam imefichuka, Ijumaa Wikienda limeinyaka.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho kinafanya kazi kwenye hoteli hiyo, usiku wa kifo chake, mwanaume huyo alitoka kwenda matembezini, aliporudi alikuwa ameongozana na msichana wa Kitanzania aliyekuwa akizungumza Kiingereza vizuri.
“Usiku yeye alitoka, sijui alikwenda wapi? Aliporudi alikuwa na msichana mzuri tu, naamini ni Mtanzania maana alisalimia Kiswahili, lakini pia alikuwa akiongea Kiingereza vizuri na marehemu,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa wawili hao walionekana kuwa na amani muda wote wa mazungumzo yao lakini cha kushangaza, asubuhi mwanaume huyo alikutwa amefariki dunia chumbani akiwa peke yake.
Aidha, nje ya hoteli hiyo, baadhi ya watu waliokuwa wakishuhudia mwili wa marehemu ukiingizwa ndani ya gari la polisi, Land Rover lenye namba za usajili T 760 ADY walisikika wakisema huenda mrembo aliyekuwa na mtasha huyo alimwekea madawa ya kulevya kwenye kinywaji ili amwibie fedha.
“Kama alikuwa na hawa mademu wetu wa Kibongo, usikute alimwekea madawa ya kulevya ili amwibie hela zake, sasa kila mtu na afya yake, mwingine analewa tu, mwingine anakufa kabisa,” alisema shuhuda mmoja baada ya kusikia minong’ono ya kuwepo kwa mwanamke usiku wa tukio.

Kibaki awataka Wakenya kuwa watulivu


Rais wa Kenya Mwai Kibaki
RAIS wa Kenya, Mwai Kibaki amewataka raia wote wa nchi hiyo kuwa watulivu hasa baada ya uamuzi wa Mahakama ya Jinai Kimataifa (ICC) kuwatia hatiani wakenya wanne kati ya sita waliyokuwa wakikabiliwa na uhalifu wa kibinadamu.
“Nchi hii yetu tukufu imekuwa na changamoto kubwa,” Mwai Kibaki alisema katika taarifa yake. Kenyatta mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya na mtu aliyeorodheshwa kama mmoja wa watu matajiri nchini humo ni miongoni mwa wanaokabiliwa na mashtaka pamoja na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Francis Muthaura.
Wawili hao, washirika wa rais, wanashutumiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu, ikiwemo mauaji na mateso. Wengine ni Waziri wa zamani wa Elimu, William Ruto na mwandishi wa habari, Joshua arap Sang wanakabiliwa na mashtaka katika kesi tofauti, kwa kuwa walikuwa wapinzani wa Kibaki wakati wa uchaguzi wa mwaka 2007.
Mahakama ya mjini the Hague iliamua hakuna ushahidi wa kutosha wa kuanzisha kesi dhidi ya maafisa wengine wawili. Zaidi ya watu 1,200 waliuawa katika wiki kadhaa za vurugu na watu takriban 600,000 wakalazimishwa kukimbia makazi yao. Wengi bado wanakaa katika makambi ya muda.
Wagombea wawili wa urais nchini Kenya wana kesi ya kujibu juu ya uhalifu dhidi ya binadamu kufuatia vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, Mahakama ya Kimataifa ya Jinai imeamua.
Naibu Waziri mkuu Uhuru Kenyatta na aliyekuwa Waziri William Ruto wote wanakabiliwa na mashtaka. Ni miongoni mwa wakenya wanne mashuhuri – wote ambao wamekanusha madai hayo – wanaokabiliwa na mashtaka.
-BBC

WAFANYABIASHARA YA POMBE WAPIGWA RISASI ZANZIBAR


Mfanyabiashara Alvind Asawla aliyepigwa risasi katika paji la uso ikatokea shingoni na kumwagiwa tindikali Zanzibar, akiwa na mkewe Bimal katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jumatano iliyopita. (Na Yusufu Badi).

WAFANYABIASHARA wawili mtu na mkewe, wamepigwa risasi na kumwagiwa tindikali huko Zanzibar kwa kuuza pombe.

Katika uvamizi huo uliofanyika Jumatano iliyopita mwanamke Bimal Alvind (36) alinusurika kupoteza ujauzito wake wa miezi minne baada ya kupigwa risasi ya tumbo na kumwagiwa tindikali.

Risasi hiyo ilitolewa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili bila kuathiri ujauzito huo lakini tindikali hiyo ilimjeruhi mwilini kuanzia usoni, kifuani kwenye matiti, mikono yote miwili na tumboni.

Mumewe, Alvind Asawla (42) alipigwa risasi kichwani kwenye paji la uso katikati ya macho iliyotokea nyuma chini ya shingo na sasa amepooza upande mmoja.

Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwa ndugu yake Upanga wiki hii, Asawla alisema walivamiwa Jumatano iliyopita saa 10:30 jioni katika Mtaa wa Hurumzi Mji Mkongwe.
Alisema wakati wakivamiwa, yeye na mkewe aliyeishi naye kwa miaka 17 sasa na kujaliwa watoto wawili; Priyanka (14) na Nidh (12), walikuwa wakitoka katika biashara yao wakirudi nyumbani eneo la Kiponda.

Alisema ghafla watu wawili walimvamia mkewe na kummwagia tindikali na yeye alipokuwa akijaribu kumsaidia, watu hao walimmwagia tindikali usoni.

Kwa mujibu wa Asawla, wakati wakitaharuki kwa hali hiyo, ghafla alitokea mtu mwingine na kumpiga risasi katika paji la uso akadondoka chini huku damu zikimtoka.

Alisema alijaribu kujikongoja kwa nia ya kuendelea kumsaidia mkewe lakini mtu huyo wa tatu alimpiga risasi ya pili mgongoni na mkewe akapigwa risasi ya tumbo.

Kwa nini Nyerere alitoa Machozi Mwaka 1958...

Swali hili nimemwuliza Mama Mosi Tambwe aliyekuwepo kwenye mkutano wa Tabora mwaka 1958. Angalia jibu hapo chini.
Ni baada ya kuyasema haya. Tabora, Januari, mwaka 1958.
Kwa mujibu wa Mama Mosi Tambwe niliyeongea nae nyumbani kwake hapa Tabora jioni ya leo. Mosi Tambwe alipata kuwa kiongozi wa juu ndani ya TANU na CCM akianzia na Uenyekiti wa Tawi. Mwaka 1958 alikuwa TANU Bantu Group akiwa na miaka 18 tu.

DKT,WANYACHA AENDELEA NA ZIARA YAKE YA KUKAGUWA MADARAJA- DSM

 Daraja la Goba likiwa kwenye ukarabati
 Baadhi ya wachimba mmchanga wakiendelea na kuchimba pamoajna kshuguli nyengine za kijamii zikiendelea
 Mhandisi kutoka tanroads Joseph Njau (kushoto) akitoa maelezo jinsi mafuriko yalivyoharibu daraja -mbezi kwa media9kush) mK
 Mk wa Mfuko wa Bodi ya Barabara Dkt, James Nyachia (kush) akimskiliza mhandis Ndukimana kutoka Tanrods (kulia) huko Segerea 
 
Na Mjengwablog

MAMA UWOYA ANENA MAZITO






Irene Uwoya.

Hamad Ndikumana ‘Kataut’.…

Monday, January 23, 2012

MAKAMU WA RAIS MKOANI LINDI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na mkewe Mama Zakhia Bilal, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Lindi, wakati akikagua Daraja la Mingumbi baada ya kuzindua daraja hilo lililopo Kilwa, akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya mkoa wa Lindi jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi Jengo jipya la Bwalo la Shule ya Sekondari ya wasichana Ilulu, iliyopo Kilwa, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Chumo Namkamba, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi, alipozindua Daraja la Mingumbi lililopo Kilwa, wakati akiwa kwenye ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila.

MSAHAFU MKUBWA DUNIANI NCHINI AFGHANISTAN


Ukiwa umefunikwa kwa unadhifu kabla ya kufunguliwa.
Mashekh mbalimbali wakifanya dua kabla ya kuufungua msahafu huo.
Bismillah unaanza kufunguliwa msahafu.
OOOoooopss waaaww!!!
 Maustadhi wakifanya dua maalumu.
Mash`Allah msahafu mzuri sana.

From; Maganga one

Chadema, Rais Kikwete waliteta saa nane


 Send to a friend

NI KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA MPYA JUZI, KAMATI KUU YAJIFUNGIA KUJADILI, NCCR- MAGAUZU WATOA TAKMO LAO
Fidelis Butahe
MKUTANO kati ya Rais Jakaya Kikwete na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) uliofanyika juzi Ikulu, Dar es Salaam ulichukua saa nane kutokana na uzito wa hoja zilizokuwa zimetolewa na pande zote mbili.

Novemba mwaka jana, Chadema ilikutana na Rais Kikwete kwa mara ya kwanza Ikulu na kumkabidhi kabrasha lililokuwa na mapendekezo mbalimbali kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba ambayo pamoja na mengine, kilitaka mchakato huo urejeshwe upya bungeni na kumtaka mkuu huyo wa nchi asitie saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambao ulipitishwa na Bunge. Hata hivyo, siku moja baada ya mazungumzo hayo, Rais alitia saini muswada huo na kuwa sheria.

Vyanzo vya habari kutoka Ikulu, vililiambia gazeti hili jana kwamba Chadema ilipewa ratiba hiyo kuanzia saa 10:30 hadi saa 5:45 usiku ili kutoa wigo mpana wa majadiliano hayo yenye nia ya kupata Katiba kwa njia za amani na umoja.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, katika chumba cha mazungumzo kulitawaliwa na majadiliano ya kina ambayo wakati mwingine, yaliambatana na utani wa hapa na pale kwa mfano, Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willbrod Slaa alimwambia Rais: “Watu wanasema nakukwepa Rais.”
Ilielezwa kwamba katika mazungumzo hayo, wajumbe wa pande zote mbili walijadili kwa uhuru mkubwa na mkuu huyo wa nchi namna ya kupata Katiba bora bila mikwaruzano.

“Mazungumzo yalikuwa ni mazuri tu, pande zote mbili zilizungumza na kutoa hoja zake, kulikuwa na utani wa hapa na pale. Yale ambayo yalionekana kuwa magumu kidogo kila upande uliomba kuyachukua na kwenda kuyafanyia kazi zaidi kabla ya kufikia uamuzi wa mwisho.”

Novemba 28 mwaka jana, Rais Kikwete alisaini muswada huo na kukamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limeupitisha.

Tangu wakati huo Rais Kikwete amekuwa akitutana, kusikiliza na kuchukua maoni na mawazo ya wadau mbalimbali kutoka vyama vya siasa, asasi za kijamii na makundi mengine ya kijamii kuelekea mchakato wa kupata Katiba Mpya.

Mchakato huo umekuwa ukipingwa na kwa hoja mbalimbali zikiwamo za kuundwa kwa tume ya kuratibu mchakato huo, hadidu za rejea, mamlaka ya uundaji  wa tume na uteuzi wa wajumbe na wapi tume itapaswa kuwajibika.

Kauli ya Ikulu
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na kusainiwa na Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais, Premi Kibanga ilisema Rais Kikwete alisema licha ya nchi kuwa na Katiba ambayo imelilea vizuri taifa,  inahitajika Katiba mpya inayokwenda na wakati.
Alisema baada ya kumalizika kwa kikao na viongozi wa NCCR-Mageuzi, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Chadema, ikiwa ni mwendelezo wa mazungumzo yao yaliyoanza mwishoni mwa  Novemba, 2011 kuhusu Katiba Mpya.

“Katika mazungumzo haya na vyama vya siasa, Rais amesisitiza kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa hatimaye Watanzania wote watakiri kuwa Katiba Mpya ni yao wote na hatimaye ifikapo mwaka 2015 nchi iweze kufanya uchaguzi wake na Katiba Mpya,” alisema Kibanga.

Chadema wajifungia Dar
Kwa upande wa Chadema, jana Kamati Kuu (CC) chini ya Mwenyekiti wake Freeman Mbowe ilikuwa katika Hoteli ya Protea Dar es Salaam kujadili mkutano huo na Rais, Ikulu juzi.

Katika kikao hicho, Kamati Maalumu ya Chadema kuhusu mchakato huo wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, iliwasilisha taarifa yake.

Taarifa ya chama hicho, iliyotolewa na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika ilisema uamuzi wa CC kuhusu mkutano na Rais  Kikwete utatolewa baada ya kikao hicho kumalizika.

Akizungumzia mkutano wa Ikulu, Mnyika alisema kamati hiyo maalumu ya Chadema iliyokutana na Rais Kikwete ikiongozwa na Mbowe, ilitaarifiwa hatua ambayo imefikiwa na Serikali katika kuanza kuiboresha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, ili ikidhi mahitaji ya kuaminiana na muafaka wa kitaifa kwa mawasiliano na ushauri wa wadau mbalimbali.

Kauli ya NCCR-Mageuzi
NCCR-Mageuzi kwa upande wake, kilitoa taarifa kwa vyombo vya habari kikidai kwamba Rais Kikwete amekubali kuifanyia marekebisho  sheria hiyo.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ambaye aliongoza na ujumbe wa watu sita kwenda Ikulu Dar es Salaam juzi, alisema jana kwamba baada ya kuwasilisha ajenda zao mbili kuhusu katiba na umeme, waliambiwa sheria hiyo itafanyiwa marekebisho katika kikao kijacho cha Bunge.

Mbatia aliwaambia waandishi wa habari kwamba pamoja na sheria hiyo kurudishwa bungeni, pia walimwomba Rais Kikwete aifanyie marekebisho Ibara ya 98 ya Katiba ya sasa kwa kuwa inachangia kukwamisha mabadiliko ya Katiba.

“Lengo la kuanzishwa kwa NCCR-Mageuzi ni Watanzania kuwa na Katiba yao na hata Rais wa Awamu ya Tatu (Benjamin Mkapa), tuliwahi kumweleza kwamba Katiba ni ya kudumu na lazima iundwe kwa maslahi ya wananchi na ndicho tulichomweleza Rais Kikwete,” alisema Mbatia.

Alisema tangu wakati huo nchi imekuwa na katiba yenye mfumo wa chama kimoja, licha ya kuwa ilipitishwa sheria ya kuwa na vyama vingi.

Mbatia alisisitiza kwamba, katika msafara wa chama hicho Ikulu, Mkuu wa Idara ya Katiba na Sheria wa chama hicho, Dk Sengondo Mvungi alitumia zaidi ya saa moja kumfafanulia Rais Kikwete na timu yake jinsi mchakato wa kuandika Katiba Mpya unavyotakiwa kuwa.

Alisema walimweleza Rais Kikwete kwamba  suala la Katiba ni la kisiasa, hivyo si vyema Tume itakayoundwa ikaachwa chini ya uangalizi wa wanasheria pekee.

“Katika tume hii wanatakiwa kutumiwa wataalamu mbalimbali hata kama watakuwa wanasiasa… kinachotakiwa ni kuangalia uwezo wao,” alisema Mbatia.

Katika kikao hicho cha Rais na NCCR-Mageuzi, viongozi wa Serikali waliokuwapo ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi na ujumbe wa chama hicho uliwajumuisha pia Makamu Mwenyekiti wake, Zanzibar, Ambary Hamisi, Naibu Katibu Mkuu George Kahangwa, Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali, Mweka Hazina Taifa, Mariam Mwakingwe, na Mbunge wa Kasulu Vijijini, Zaituni Buyogela.

Mwananchi.co.tz

Sunday, January 22, 2012

SIRI NZITO MGOGORO WA KKKT IRINGA ,WACHOCHEZI WALIPONA BAKORA

Askofu Dr Mdegella akizungumza na mtandao huu baada ya mgogoro kutangazwa kumalizika
Nimewasamehe bure wote waliohusika kunichafua
Askofu Dr Mdegella akitoa baraka kwa waumini wa kanisa hilo usharika wa kanisa kuu ,pembeni ni askofu Dr Shayo
Askofu Dr Shayo akiendesha ibada hiyo kwa niaba ya askofu Dr Mdegella
Waumini wa kanisa hilo wakisikiliza kwa makini taarifa ya mgogoro huo ulivyokuwa


SIRI nzito yaibuka sakata la mgogoro mkubwa uliokuwa ukilikabili kanisa hilo na kuwa kama si busara za viongozi wa juu wa kanisa katika kumaliza mgogoro huo uliokuwa ukilikabili kanisa hilo la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa kati ya askofu wake Dr Owdernburg Mdegella na baadhi ya waumini wake bakora zingetembezwa kwa wahusika.
Akitangaza kumalizika kwa mgogoro huo mbele ya waamuni wa kanisa hilo usharika wa kanisa kuu Iringa mjini mapema jumapili iliyopita ,askofu wa kanisa la kilutheri Dayosisi ya Makete Dr Hance Mwakabona ambaye ndio alikuwa msemaji mkuu wa kamati maalum iliyoundwa na askofu mkuu wa kanisa hilo Dr Alex Malasusa .
Kabla ya kamati hiyo maalum iliyoundwa kutoka makao makuu ya kanisa hilo ili kuchunguza kiini cha mgogolo huo kwa kufanya mazungumzo ya na pande zote mbili kutangaza kuumaliza mgogolo huo vijana na kanisa hilo na baadhi ya waaumini ambao walikuwa hawapendezwi na kikundi hicho cha watu wachache kumshambulia askofu wao waliapa kuwachalaza bakora wao huo wachochezi.
Mmoja kati ya vijana ambao walikuwa wamechukizwa na mwenendo wa baadhi ya wazee maarufu katika kanisa hilo kwa kuchapisha vipeperushi vya kumtukana askafu Dr Mdegella alisema kuwa wamevumilia vya kutosha na walikuwa hawapo tayari kuendelea kuwavumiliwa watu hao waliokuwa wakiongozwa na mmoja kati ya wazee maarufu katika kanisa hilo kuona wanaendelea na kampeni zao chafu za kuchafua kanisa .
Alisema kuwa mhusika wa mgogoro huo kati ya askofu wao Dr Mdegella na kanisa hilo anafahamika na kuwa wanachopinga na kuchukia ni hatua ya kutumia vipeperushi kama mambo ya siasa katika kulichafua kanisa ni kufanya wamumini wote wanaoabudu katika kanisa hilo kuonekana hawana maana mbele ya jamii.
“Uvumilivu wetu ulikuwa umefika mwisho kama kamati hii kutoka makao makuu ingeshindwa kumaliza suala hili sisi vijana tungelimaliza kwa kuwaadhibu kwa bakora wahusika wa suala hili ambao walikuwa wakichapisha vipeperushi na kusambaza mitaani”
Alisema kuwa ni vipeperushi vya aibu sana ambavyo watu hao walikuwa wakisambaza na katika vipeperushi hivyo kulikuwa na matusi ya makubwa ya nguoni ambayo hayapaswi kusomwa wala kuwekwa bayana katika chombo chochote cha habari .
Kwani walisema kuwa hata kama waliyoyachapisha katika vipeperushi hivyo yangekuwa na ukweli ama uongo njia sahihi haikuwa hiyo ambayo waliitumia ya kuchapisha vipeperushi hivyo na kuvisambaza mitaani bali walipaswa kutumia njia nzuri za kufikisha ujumbe wao hata kukutana na viongozi wa juu wa kanisa kuliko kulidharirisha kanisa la bwana.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati hiyo askofu Dr Mwakabona katika taarifa yake kwa waumini wa kanisa hilo alisema kuwa kamati hiyo ilikutana na makundi yote na hata wahusika wa suala hilo na kuwahoji kwa siri katika mahojiano yaliyodumu kwa takribani siku mbili na kuishi usiku wa manane.
Alisema kuwa mkuu wa kanisa hilo aliunda kamati hiyo yenye wajumbe zaidi ya wanne akiwemo askofu wa Dr Martine Shayo wa Moshi , Askafu Elisha Buberwa na katibu mkuu wa KKKT Brighton Killewa ili kuweza kuja mkoani Iringa kupata ukweli wa mgogoro huo na kuumaliza ili kazi ya kanisa kuendelea.
Kwani alisema kuwepo kwa mgogoro katika moja ya Dayosisi za KKKT nchini si tu madhara yanakuwepo katika dayosisi hiyo pekee bali ni kwa KKKT nzima na kuwa ndio sababu ya kufika na kumaliza mgogoro huo ili kuuanza mwaka 2012 kwa hali ya upendo na mshikamano zaidi .
Hivyo alisema kuwa kwa sasa mgogoro huo umemalizika na wahusika wote wa mgogoro huo wamesamehewa bure na kuwa maazimio ya kamati hiyo baada ya kupokea maoni kutoka katika pende zote ni kuona kuwa wahusika wanasamehewa na kuwa kwa yale ambayo ni makubwa zaidi yenye vithibiti yanafanyiwa kazi taratibu ili kupata ukweli zaidi .
Kwa upande wake askofu Dr Mgedella alisema kuwa yaliyosambazwa na watu hao katika vyombo mbali mbali vya habari likiwemo gazeti maarufu ya kila wiki linalosambazwa kote nchini ni uongo mtupu na kuwa kwa upande wake amesamehe na kama wataendelea kueneza uongo huo basi atalifikisha mahakamani gazeti hilo na kulitaka kumlipa fidia

Na Francis Godwin