Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Monday, February 20, 2012

JE BIBLIA ILIUFAGILIA UBEPARI? MAJIBU


NADHARIA YA MWENYE NACHO KUONGEZEWA
Hivi karibuni mwanautambuzi mwenzangu Kamala katutolea fungu moja katika biblia akidai kwamba Biblia inaufagilia ubepari.
Ingawa fungu lenyewe alilinukuu kwa kiingereza, nimeona nilitafsiri kwa Kiswahili ili niweze kumjibu vizuri.
Fungu lenyewe ni kutoka katika kitabu cha Marko mtakatifu, 4 fungu la 24 mpaka 25.Nitanukuu fungu hilo:

‘akawaambia angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa.
Kwa maana mwenye kitu atapewa, naye asiye na kitu hata kile alicho nacho atanyang’anywa’
Mwisho wa kunukuu.

Je fungu hili linamaanisha kile alichosema Kamala, Kwamba Biblia Iliupendelea ubepari?

Kwa mujibu wa Mwanasaikolojia mmoja aitwae Dr. Sigmund Freud katika mojawapo ya tafiti zake aliwahi kusema kuwa watu wamegawanyika katika makundi mawili,
Kundi la kwanza ni lile la watu walioshindwa katika maisha na kundi la pili ni lile la watu walifanikiwa.
Dr Sigmund Freud anazidi kubainisha kwamba tofauti iliyopo katika makundi hayo mawili ni namna kila kundi linavyofikiri.

Kundi la wale walioshindwa katika maisha linakuwa ni la watu wanofikiri juu ya kushindwa, ni kundi la watu wasioamini katika kufanikiwa,.
Watu wanoangukia katika kundi hili kufanikiwa kwao ni jambo lisiliwezekana kutokana na namna wanavyofikiri.
Kundi hili ndio lile la asiyekuwa nacho kupokonywa hata kile kidogo alichonacho kama lilivyozungumziwa katika biblia na bwana Yesu.
Kwa nini hata kile kidogo alichokuwa nacho anyang’anywe?
Kwa kawaida kama unafikiri na kuamini katika kushindwa, sio tu kwamba kufanikiwa kwako itakuwa ni msamiati mgumu, bali pia kutofanikiwa huko kutakugharimu, kwa sababu, utakuwa kila unachojaribu kufanya ambacho umetumia gharama katika kukianzisha hakifanikiwa na hivyo ile gharama uliyotumia kupotea.
Ndio kunyang’anywa kwenyewe hata kile kidogo ulichonacho.

Kundi la watu waliofanikiwa ni lile la watu ambao mawazo yao yote yapo katika kufanikiwa, kundi hili ni la watu makini ambao kwao anguko moja ni kama ngazi ya kuelekea katika kufanikiwa.
Kundi hili ni la watu wenye moyo wa kuthubutu, halijali kuhatarisha mitaji yao, kwa kuhofia kupata hasara.
Watu wanaoangukia katika kundi hili hawachoki kujaribu hata wanapopata maanguko kadhaa hujipa moyo na kusonga mbele, hawana muda wa kukaa na kunung’unika, kwa kuwaza kuhusu maanguko yaliyopita, kwao huo ni mzoga ulishakufa na kuoza.
Watu wa namna hii pia wanayo sifa ya kuwa na subira, na hii ndio nguzo muhimu sana wanayoitumia, ndio sababu wanafanikiwa.
Kundi hili ndilo lile la walionacho kuongezewa, kama ilivyoandikwa katika biblia.

Kama unafikiri katika kufanikiwa utafanikikiwa na kuwa tajiri kwa jinsi unavyotaka na kama unafikiri katika maanguko, basi wewe utavuna umasikini wa kutosha, na usimlaumu mtu.
Yesu hakuwa mnafiki, alikuwa muwazi, alijitahidi sana kuwafundisha wafuasi wake namna ya kufanikiwa, lakini tafsiri iliyokwenda vichwani mwao ilikuwa ni tofauti.

Ndio sababu watu wengi walipotoshwa na mojawapo ya mafundisho ya Yesu aliposema kwamba tajiri kuuona ufalme wa mbinguni ni sawa na ngamia kupenya katika tundu la sindano.
Fungu hili lilipotoshwa na wahubiri wengi kiasi cha kuwafanya waumini wao kuuogopa utajiri.

Naomba kuwasilisha.


http://kaluse.blogspot.com/2008_12_15_archive.html

No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.