Blog yenu ya wananchi yenye habari motomoto za kijamii, Blog yenye kuelimisha, kuburudisha na kufurahisha. Wapenzi na wasomaji wetu tunaomba ushirikiano wenu ili kuendeleza Blog yetu, kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Tuesday, February 21, 2012

GAP KATI YA WACHUNGAJI NA WAUMINI

HAYA MENGINE TENA


 Usafiri wa Mchungaji.
Usafiri wa Muumini.

Na Makongoro Oging' na Haruni Sanchawa
RIPOTI nzito inayohusu utajiri wa kutisha kwa baadhi ya viongozi wa dini wakiwemo wachungaji na maaskofu na kuweka utofauti mkubwa wa maisha baina ya waumini, umezua gumzo kubwa katika makanisa mbalimbali nchini.
Waumini wengi waliozungumza na gazeti hili wamewashitukia baadhi ya viongozi hao wa dini kutokana na kile walichodai kuwa wamezidi kujilimbikizia mali huku wakiwahimiza (waumini) kutoa sadaka na michango mbalimbali ya mara kwa mara.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya waumini wamekuwa wakihama kutoka kanisa moja kwenda lingine huku wakiamini kuwa Mungu atawasaidia wabadilike kimaisha au kumaliza matatizo yao.
Kutokana na mgongano huo baina ya viongozi wa makanisa na waumini, baadhi ya wachungaji na maaskofu waliozungumza na gazeti hili walikuwa na michango yao juu ya hali hiyo na walizungumza kama ifuatavyo:

Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Dk. Valentino Mokiwa akizungumza na gazeti hili kuhusu suala hilo la viongozi wa dini kujitajirisha alishauri kwamba makanisa ya watu binafsi ambayo viongozi wao wamejipatia mali nyingi zenye utata wachunguzwe kwa karibu.
“Viongozi wa dini au muumini kuwa tajiri siyo jambo baya kwani hata sisi katika makanisa yetu ya Anglikana kuna maaskofu matajiri na maskini na hakuna sheria inayomkataza kiongozi wa dini kuwa tajiri bali inategemea jinsi alivyoupata, ambao haijulikani utajiri wao umetoka wapi, wachunguzwe,” alisema Askofu Mokiwa.


No comments:

Post a Comment

Msomaji wetu hakikisha unaheshimu mila na tamaduni za mwafrika,lugha zenye utata au kumkashifu mtu haitapendeza kuonekana kwenye post.Kumbuka vigezo na masharti ya comments kuzingatiwa.Asanteni sana kwa kuwa nasi kwenye blog yenu.